Saturday, November 4, 2017

THAMANI YAKO IPO TU UKIWA HAI..

Kwakuwa lipo tumaini kwa yule aliyeambatana na wote walio hai; (maana ni afadhali mbwa aliye hai kuliko simba aliyekufa);
 Mhubiri 9:4

Kwa maana linalowatukia wanadamu linawatukia wanyama; jambo moja lawatukia; anavyokufa huyu ndivyo anavyokufa huyu; naam, wote wanayo pumzi moja; wala mwanadamu hana kitu cha kumpita mnyama; kwa maana yote ni ubatili.
 Mhubiri 3:19

MUHIMU: Kuishi sawa sawa na neno la Mungu..maana uhai wa kila kiumbe upo mikononi mwake.

ZINGATIA: Mwanadamu anakufa sawa sawa na mnyama ila liko tumaini kwa mwadamu ikiwa tu atayatoa maisha yake kwa Yesu.. Huyu Yesu ndo mwenye uwezo wa kukufanya uishi tena baada ya kifo inamaana yeye ni ufufuo na uzima.

KUMBUKA: Mwanadamu anamzidi mnyama kwa kuwa amenunuliwa kwa damu ya thamani ya Yesu Kristo.. Mchague Yesu sasa na umfanye kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako.

HAKIKA: UTAISHI TENA.

YESU ANAPITA KWAKO LEO.


LUKA 17:11-14
11. Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, Yesu alikuwa akipita katikati ya Samaria na Galilaya.
12. Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,
13. wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!
14. Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.
Najua Mpo wengi leo mnapitia changamoto za aina mbalimbali.
Nakukumbusha kuwa Yesu anapita kwenye mji wako leo, anapita kwenye biashara yako, anapita kwenye ugonjwa wako, anapita kwenye ndoa yako.

Nishida gani inakusumbua? Mwambie Yesu.
Sema maneno haya EE YESU BWANA MKUBWA UNIREHEMU.

Wale wote waliokucheka kwa sababu ya shida yako sasa jionyeshe kwao, ili nao wasimulie matendo makuu ya Mungu aliyo kutendea.

Bwana akupe hitaji la moyo wako.

KIBONZO


Dawa ya nguvu za kiume hii hapa👇🏻👇🏻 Sasa wewe endelea kuzurura kutwa nzima kuwatafuta wamasai na waganga ili wakupatie dawa ya nguvu za kiume.
Ukiona mke wako anakwambia huna nguvu za kiume ujue mfuko umetoboka😁😁😁hakuna upungufu wa nguvu za kiume kwenye pesa na hakuna dawa ya kuongeza nguvu za kiume duniani..my friend utamaliza soli ya kiatu bure kwa kuwatafuta wamasai badala yake fanya kazi kwa bidii ili ule chakula chenye rishe kamili, pia itakupunguzia mawazo na msongo wa maisha.
Na nyie akina mama mmmmmh Mungu anawaona, punguzeni midomo, kumsakama mtoto wa mwanamke mwenzako kutwa nzima, badala uwe faraja kwake wewe unakuwa chanzo cha stress.
Kama pesa ni rahisi kuipata mbona wewe huna? Kutwa nzima unamsumbua mbaba wa watu kwa nini asipate upungufu wa nguvu za kiume..

Mawazo + kukosa hela/maisha magumu = upungufu wa nguvu za kiume.

Saturday, August 19, 2017

HAKUNA MKAMILIFU

Hakuna familia isiyo na mapungufu, Hatuna wazazi wasio na mapungufu, sisi pia si wakamilifu, hatuoi au kuolewa na mtu asiye na mapungufu, kadhalika watoto wetu nao si wakamilifu.
Tunayo manung'uniko au malalamiko kila mmoja dhidi ya mwenzake. Tumevunjana moyo na kukatishana tamaa. Kwa hiyo, hakuna ndoa iliyokamilika wala familia iliyoboreka bila kuwa na mazoea au utamaduni wa kusameheana.
Msamaha ni nguzo au msingi wa utulivu wa akili na uhai wa roho zetu. Kama hakuna msamaha, familia inakuwa uwanja wa migogoro na mlipuko wa ugomvi. Panapokosekana msamaha, familia inaugua. Msamaha unahuisha moyo, kwa kusafisha fikra na kuufanya moyo kuwa huru. Binadamu asiyesamehe hana amani moyoni na wala hana urafiki au muunganiko na Mungu.
Maumivu ni sumu inayodhuru na kuua. Hebu kiponye kidonda hicho cha moyo endapo kuna dalili za kujiumiza. Mtu asiyesamehe anajisababishia mwenyewe ugonjwa wa mwili, kiakili na kiroho. Ndiyo maana familia inapaswa kuwa sehemu ya uhai na si kifo; eneo la uponyaji na sio mahali pa magonjwa; jukwaa la msamaha na si la uovu.
Msamaha huleta furaha pale uchungu ulipoleta maumivu, huleta uponyaji hata pale ambapo maumivu yalisababisha magonjwa.

YEREMIA, MSEMAJI WA MUNGU

Ni vema mtu autarajie wokovu wa Bwana Na kumngojea kwa utulivu. Maombolezo 3:26.

Kati ya wale waliotumaini kuwa na uamsho wa kudumu wa kiroho ikiwa matokeo ya matengenezo chini ya Yosia alikuwa Yeremia, aliyeitwa na Mungu ili aingie katika nafasi ya kuwa nabii akiwa bado kijana…
Ndani ya kijana Yeremia, Mungu aliona mtu ambaye angeaminika na ambaye angesimama katika haki dhidi ya upinzani mkubwa… Bwana akamwambia mjumbe wake aliyemchagua; “Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru.”….
Kwa miaka arobaini ilimpasa Yeremia kusimama mbele za taifa kama shahidi ya ukweli na uadilifu. Katika wakati wa uasi usio na kifani ilimpasa aoneshe ibada ya Mungu pekee wa kweli katika mfano wa maisha na tabia. Wakati wa utekwaji wa kutisha wa Yerusalemu ilimpasa awe msemaji wa Yehova.
Akiwa kwa asili na silika ya kuwa mwoga na mwenye kunywea, Yeremia alitamani amani na utulivu wa maisha ya kujitenga, ambapo asingelazimika kushuhudia maendeleo ya mioyo migumu ya taifa lake alilolipenda. Moyo wake ulikamuliwa kwa maumivu kutokana na uharibifu ulioletwa na dhambi….
Uzoefu aliopitia Yeremia siku za ujana wake na pia katika siku za mbeleni za huduma yake, ulimpa fundisho kwamba “njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu. Ee Bwana, unirudi kwa haki; si kwa hasira yako, usije ukaniangamiza” (Yeremia 10:23, 24).
Alipoitwa kukinywea kikombe cha mateso na huzuni na alipojaribiwa wakati wa shida yake kusema, “Nguvu zangu zimepotea, na tumaini langu kwa Bwana,” alikumbuka majaliwa ya Mungu kwa ajili yake na kwa kushangilia akasema, “Ni huruma za Bwana kwamba hatuangamii, kwa kuwa rehema zake hazikomi…Bwana ndiye fungu langu, husema nafsi yangu, kwa hiyo nitamtumaini yeye.”

Friday, May 26, 2017

NI KWA JINSI GANI YESU KRISTO ALIITIMIZA TORATI NA MANABII?


Yesu alipozungumzia “torati na manabii” alimaanisha mafundisho ya Agano la Kale, ambayo kwa wakati huo ndiyo yaliyokuwa kiini cha imani ya wacha-Mungu. Yesu anasema hakuna kuondoa au kubatilisha/kufuta mamlaka ya Agano la Kale. Hakuja kupindua, kubatilisha, wala kufuta bali kuendeleza au kuitekeleza.

Yesu aliitimiza torati na manabii kwa kujisalimisha Yeye binafsi kuwa mtii wa sheria (Yohana 15:10), kwa kuipatia utoshelevu kamili uliohitajika kulingana na haki ya Mungu. Haki ya Mungu ilidai mauti ya mwasi wa sheria Yake. Kristo aliitimiza kwa kufa kwa niaba ya mdhambi. Aliitimiza sheria kwa kuifanya sheria iwe kanuni Yake ya mwenendo na maisha, kwa kuifundisha kwa watu kikamilifu, kuipatia maana halisi. 

Yesu alikuja kutimiza kusudi husika la torati na manabii. Alikuja kukuza vidokezo na hazina za kweli, kugeuza kanuni na maagizo yaliyokuwa yamewekwa na wanadamu mahali pa Amri za Mungu (rejea Mathayo 15:9; Marko 7:7-9). Alikuja kutimiza haki yote (Mathayo 3:15) kwa njia ya utii kamili wa kanuni za Sheria ya Mungu. Alikuja kutimiza chochote kilichokuwa kielelezo au mfano Wake. Yeye ndiye alikuwa “mwili” halisi (Wakolosai 2:17). Sheria ya Musa iliundwa kwa mfumo wa kafara na taratibu za kidini zilizokusudiwa kumwakilisha Kristo na kuelekeza katika ujio Wake. Hizi zilitimizwa wakati alipojitoa nafsi Yake Kafara kwa Mungu.

Kristo alithibitisha na kusisitiza sheria ya Mungu kwa kina zaidi, katika maana yake pana na ya ndani zaidi. Kwa wenge, ilifahamika kwamba kuua ni kufanya tu tendo husika la kuondoa uhai, lakini Yesu alifundisha kwamba hata chuki tu dhidi ya mtu ni sawa na uuaji. Pia kuhusu zinaa na uasherati alisema vinahusisha uendekezaji wa mawazo na fikra chafu za tamaa ya mwili. Alionesha kwamba utekelezaji kamili wa sheria huanzia moyoni. Utii wa andiko la sheria kwa nje huanza na utii utokanao na nia ya rohoni.

Hivyo ni hatari kabisa kudhani kwamba Kristo amewaruhusu watu Wake kutupilia mbali maagizo yoyote ya sheria Yake takatifu ya Mungu. Kuvunja amri moja ni sawa na kuwa mkosaji wa zote (Yakobo 2:10, 11). Haki ya Kristo, inayohesabiwa kwetu bure kwa imani pekee, huhitajika na kila mmoja anayeingia katika ufalme Wake wa neema au utukufu; kiumbe kipya aliyefanyika katika Kristo huwa na badiliko kamili la maisha liendanalo na utii wa Amri Zake.

“Na katika hili twajua ya kuwa tumemjua Yeye, ikiwa tunashika amri Zake. Yeye asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri Zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani yake. Lakini yeye alishikaye neno Lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika kweli kweli. Katika hili twajua ya kuwa tumo ndani Yake. Yeye asemaye ya kuwa anakaa ndani Yake, imempasa kuenenda mwenyewe vile vile kama Yeye alivyoenenda.” 1 Yohana 2:3-6.

Thursday, May 25, 2017

MAKUNDI MAWILI YATAKAYOFUNGA HISTORIA YA MWISHO WA DUNIA

 Na Pr. Joackim Msembele.

Malaika wakipeleka ukweli wa Mungu wa sasa wa onyo la mwisho kwa dunia inayoangamia kwa sababu ya makosa na dhambi za wakazi wa dunia hii.
 

JE! UNAJUA KINACHOTOKEA SASA HIVI NA KINACHOTAKA KUTOKEA HIVI KARIBUNI? ENDELEA KUSOMA UJUMBE HUU KWA MAKINI.
“Tena kutakuwa na ishara katika jua na mwezi, na nyota na katika nchi dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake: watu wakivunjika mioyo kwa hofu na kwa kutazamia mambo yatakayoupata ulimwengu. Kwa kuwa nguvu za mbinguni zitatikisa. Hapo ndipo watakapomwona Mwana wa Adam akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu mwingi.
Basi mambo hayo yaanzapo kutokea changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia” (Luka 21:25-28).
 

KUNDI LA KWANZA
“ “Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa, maana BWANA amenena neno hilo. Dunia inaomboleza, inazimia; ulimwengu unadhoofika, unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika. Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa; kwa maana wameziasi sheria, wameibadili amri, wamevunja agano la milele. Ndiyo sababu laana imeila dunia hii, na hao wanaoikaa wameonekana kuwa na hatia. Ndiyo sababu watu wanaoikaa dunia wameteketea, watu waliosalia wakawa wachache tu.” (Isaya 24:3, 4, 5, 6)
Kuomboleza na kuzimia kwa dunia ni pamoja na – Majanga ya asilii yanayotokea, kama vile; mabadiliko ya tabia ya nchi yanayosababisha ongezeko la joto duniani na kuleteleza; mafuriko, ukame, kuyeyuka kwa barafu kaskazini mwa ncha ya dunia na hata katika mlima wa Kilimanjaro, vimbunga na matetemeko ya ardhi, nk.
 

Kudhoofika na kuzimia kwa ulimwengu ni pamoja na kuvunjika kwa maadili; kama vile kubaka hata watoto, kuua albino, kuoana jinsia moja, machafuko ya siasa, migomo ya wafanyakazi, nk.
Kudhoofika kwa watu wakuu wa dunia:
Kila kiongozi wanchi hatawali kwa raha, misongo mingi; kukosolewa kwingi; maandamano ya raia kila mahali. Uchaguzi ukipita hakuna anayeridhika. Tuhuma nyingi za wizi wa kura; na wengine hata kung’ang’ania madaraka hata kama kura zimetangazwa na kuonekana wameshindwa. Hayo yote yanawalenga watu wakuu wa dunia. Ni unabii wa kufungwa kwa histaoria ya mwisho wa dunia.

Haya yote yanatokea ni kwa sababu wameziasi sheria, wameibadili amri, wamelivunja agano la milele. Katika amri 10 za Mungu, ulimwengu umeasi amri ya 1 hadi ya 4 ambazo Yesu alisema ndiyo amri kuu tena ni ya kwanza (Mathayo 22:35-38). Ulimwengu umeasi amri zifuatazo: ya-
Usiwe na miungu mingine ila mimi.
Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni wala kilicho chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.
Usilitaje bure jina la BWANA, Mungu wako, maana BWANA hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure.
Ikumbuke siku ya sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; lakini siku ya saba ni sabato ya BWANA Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.
Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya sabato akaitakasa.” (Kutoka 20:3-11)
Amri hizi haziko kwenye vitabu vya sheria vya mahakama za nchi zote duniani. Na watu wengi hawana habari. Ndiyo sababu laana imeila dunia hii.


MWISHO WAKE UTAKUWAJE?
“Dunia kuvunjika, imevunjika sana; dunia kupasuka, imepasuka sana dunia kutikisika inatikisika sana; dunia inalewa-lewa kama mlevi, nayo inawaya-waya kama machela; na mzigo wa dhambi zake utailemea; nayo itaanguka,wala haitainuka tena.” (Isaya 24:19-20)

Dhambi ni nzito kuliko bomu la nyuklia. Mabomu ya nyuklia yanafanyiwa majaribio, lakini dunia haitikisiki ila dhambi haitaitikisa tu dunia bali itaiangusha dunia na haitainuka tena.
Dhambi ni uasi wa sheria za Mungu ambazo ni pamoja na amri nne (4) zilizotajwa hapo juu. Ndiyo maana Mungu anataka watu wote wazitii amri zote za Mungu ambapo ndani yake inasema pia watu wote waitakase sabato na kutokuabudu na kutumikia sanamu. Hebu soma maneno yafuatayo uone namna ambavyo Mungu anajifunua kwa wajawake.
“BWANA asema hivi, shikeni hukumu, mkatende haki; kwa maana wokovu wangu u karibu kuja, na haki yangu kufunuliwa. Heri afanyaye haya, na mwanadamu ashikaye sana; azishikaye sabato asizivunje, auzuiaye mkono wake usifanye uovu wowote. Wala mgeni, aambatanaye na BWANA, asisema hivi, Hakika yake BWANA atanitenga na watu wake; wala towashi asiseme, Mimi ni mti mkavu. Kwa maana BWANA awaambia hivi matowashi, wanazishika sabato zangu, na kuyachagua mambo ya nipendezayo, na kulishika sana agano langu; Nitawapa hawa nyumbani mwangu, na ndani ya kuta zangu, kumbukumbu na jina,lililo jema kuliko kuwa na wana na binti; nitawapa jina lidumlo milele, lisilokatiliwa mbali. Na wageni, walioandamana na BWANA ili wa mhudumu, na kulipenda jina la BWANA, kuwa watumishi wake: kila aishikae sabato asiivunje, na kulishika sana agano langu; Nitawaleta hao nao hata mlima wangu mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala; makafara yao na dhabihu zao zitakubaliwa juu ya madhabahu zangu; kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote. Bwana MUNGU, akusanyaye waliofukuzwa katika Israeli asema, pamoja na hao nitamkusanyia na wengine zaidi ya hao walio wake waliokusanywa.” (Isaya 56:1-8).
“Basi, imesalia raha ya sabato kwa watu wa Mungu.” (Waebrania 4:9) “Yeye asemaye Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli kweli haimo ndani yake.” (1Yoh. 2:4).hii ni kundi la kwanza, limeziasi sheria 4 za kwanza.


KUNDI LAPILI – kundi hili ni kwa watu gani?
“Piga kelele, usiache, Paza sauti yako kama tarumbeta; uwahubiri watu wangu kosa lao. Na nyumba ya Yakobo dhambi zao.” (Isaya 58:1) watu wake ni akina nani?
“Zitakaseni sabato zangu; zitakuwa ishara kati ya mimi na ninyi mpate kujua ya kuwa mimi ndimi BWANA Mungu wenu.” (Ezekiel 20:20).
Lakini hawa watu wake wanaozitakasa sabato pia wana makosa na dhambi.
Dhambi yao kubwa ni kutokuwaambia wengine ujumbe muhimu wa Mungu wa wakati huu.

HAYA MAKUNDI MAWILI NI YAPI?
Makundi mawili yanayofunga historia ya mwisho wa dunia ni:

Kundi la 1. AWASIOTUNZA SABATO YA BWANA MUNGU.
Kundi la 2. WANAOITUNZA SABATO YA BWANA MUNGU.
Kila kundi litakuwa na watu watakao kwenda mbinguni na watakaoshindwa kwenda mbinguni.
Rehema ilishawahi kufungwa mara nne katika kipindi cha nyuma cha historia ya dunia hii. Nyakati hizo ni;
Wakati wa Nuhu
Wakati wa Sodoma na Gomora
Katika mwaka wa 70 B.K.
Katika mwaka1844
Kila wakati mlango wa rehema ulipotaka kufungwa, Mungu alikuwa akitoa alama ya kuokolewa kabla ya tukio kama ifuatavyo:


KIPINDI CHA:- ALAMAYA KUOKOLEWA NI KWA:-
Nuhu ---------- kuingia ndani ya Safina
Sodoma na Gomora ----- Kukimbilia Mlimani au Soari
Katika mwaka wa 70 B.K. -------- Kukimbilia Mlimani
Katika mwaka wa 1844 ---------- Kukimbilia Mlimani.


NI NINI ALAMA YA KUOKOLEWA KATIKA KIPINDI HIKI CHA KUFUNGA HISTORIA YA DUNIA?
Alama ya kuokolewa kwa wasiotunza sabato za BWANA Mungu, ni kutii sabato ya BWANA Mungu, na amri na amri zingine zilizoachwa.
Alama ya kuokolewa kwa wanaozitunza sabato za BWANA Mungu, ni kuwa taarifu wengine kwa bidii juu ya wajibu na ujumbe huu muhimu.
Kila mtu aliye hai ana nafasi ya kuokolewa au kupotea. Mpendwa msomaji, kumbuka kuwa kuna BWANA Mungu aliyekuumba wewe na kuna Shetani ambaye hakukuumba wewe. Katika pande hizi mbili unapiga kura yako kwa nani? Ndugu msomaji nakusihi kwa neema yake Yesu piga kura yako kwa BWANA Mungu nawe utaokolewa na kuishi milele. Hii ndiyo thamani ya ubinadamu.
“Amini, nawaambieni, kizazi hiki hakitaPIta hata hayo yote yatimie. Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo; Kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima.
Basi, kesheni ninyi kila wakati, mkiomba ili mpate kuokoka katika hayo yote yatakayotokea, na kusimama mbele za mwana wa Adam” (Luka 21:32-36).
“Hapa ndipo penye subira ya watakatifu hao wazishikao amri za Mungu, na imani ya Yesu” (Ufunuo 14:12).
Usitatanike kuelewa siku ya sabato ni ipi; hebu soma, Math 28:1-6, Marko 15:42-47; 16:1-6, Luka 23:44-56; 24:1-3 na Yoh 19:31-42; 20-1.
Yesu hakubadilisha sabato (Math 5:17-19 na Zab 89:34), ila mfalme Konstantino wa Rumi ndiye aliibadilisha sabato ya Biblia ya siku ya saba ya juma (jumamosi) na kuipelekea siku ya kwanza ya juma (jumapili) mnamo tarehe 7 Machi, 321, B.K. (Historia ya Kanisa la Kikristo, Toleo la 7 la mwaka 1902, Gombo la 3, uk. 380). Kufanya ibada siku ya kwanza ya juma (jumapili) ni mapokeo ya mfalme Konstantino wa Rumi, na kinyume na Biblia. (Soma; Mathayo 15:3-9 na Marko7:6-9).
Kuabudu siku ya jumapili BWANA Mungu anasema ni mapokeo “Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami, Nao waniabudu bure, wakifundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu …. Ninyi mwaiacha amri ya Mungu na kuyashika mapokeo ya wanadamu, Akawaambia, Vema Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu”. (Mathayo 15:8-9; Marko 7:8-9).
 

MUNGU ASEMA MWONGO NI NANI? “Yeye asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani yake.” (1Yohana 2:4).
Wewe unataka kuwa mkristo wa aina gani? Mkristo mwongo ambaye hataki kutii amri za Mungu au mkristo wa kweli ambaye anatii amri zote za Mungu? Chaguo lako ni lipi leo? Yesu leo anakusihi chagua kuwa mkristo wa kweli na thamani ya maisha yako itakuwa ya kudumu milele.
Ujumbe huu unatakiwa upelekwe kwa kila mkazi wa dunia hii. Na kwa hiyo tafadhali mpendwa msomaji, zalisha nakala nyingi kadiri iwezekanavyo na kumpa kila mtu unayekutana naye kwa ajili ya utukufu wa Mungu.

Wednesday, May 10, 2017

BWANA AKAMKUMBUKA


“Samsoni akamwita Bwana, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba.” Waamuzi 16:28

♻Katika mateso na kudhalilishwa, kukejeliwa na Wafilisti, Samsoni alijifunza zaidi kuhusu udhaifu wake kuliko alivyojua hapo awali; na maumivu hayo yakamwongoza kwenye toba. Kadiri nywele zake zilivyokua, nguvu zake taratibu zilirejea; ila adui zake wakimtambua kama mfungwa asiye na msaada; wakawa hawana hofu naye.

♻Wafilisti walishangilia kwamba ushindi wao umetokana na miungu yao; nao wakasherehekea, wakimtukana Mungu wa Israeli. Sherehe iliandaliwa kwa heshima ya Dagoni, mungu mwenye umbo la samaki; mlinzi wa baharini”. Toka kila kijiji na mji wa bonde lote la Wafilisti watu na wakuu wao walihudhuria. Umati wa watu ulilijaza hekalu lao kubwa na wengine wakawa orofani. Lilikuwa tukio la kucheza na kustarehe. Kulikuwepo utoaji wa kafara, nyimbo na ngoma. Ndipo, katika hitimisho la kutukuza ukuu wa Dagoni, Samsoni alisogezwa mbele. Kelele za kejeli zilitawala ukumbi wote. Watu na watawala walimbeza Samsoni na kumtukuza mungu wao ambaye amempindua “mtesi wa taifa lao.”

♻Baada ya muda, akijifanya kana kwamba ni mchovu, Samsoni aliwasihi wamruhusu aegemee kwenye nguzo mbili zinazoshikilia jengo. Kwa kimya aliomba ombi, “Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti.” Baada ya ombi hilo akainama, akazishikilia nguzo hizo mbili, kwa nguvu zake zote; ile nyumba ikawaangukia hao wakuu, na watu wote waliokuwa ndani yake. “Basi wale watu aliowaua wakati wa kufa kwake walikuwa wengi kuliko wale aliowaua wakati wa uhai wake.”

♻Sanamu hiyo pamoja na waumini wake, kuhani na mtu wa kawaida, shujaa kwa mwungwana, walizikwa chini ya magofu ya hekalu la Dagoni. Na miongoni mwao alikuwepo shujaa mkuu ambaye Mungu alimchagua apate kuwakomboa watu wake.

♻ Shindano, badala ya kuwa kati ya Samsoni na Wafilisti, likawa baina ya Yehova na Dagoni, na hivyo BWANA alijitetea mwenyewe akidhihirisha uweza na mamlaka yake juu ya dunia.

UTAVUNA ULICHOPANDA


📖Mwanangu, wenye dhambi wakikushawishi, Wewe usiku-bali.” Mithali 1:10

👉🏼Samsoni wakati wa matatizo makuu yaliyomsibu alikuwa na chimbuko lile lile la nguvu kama ilivyokuwa kwa Yusufu. Angaliweza kuchagua jema au baya kama apendavyo. Badala ya kushikilia nguvu za Mungu, aliruhusu tamaa yake mbaya imtawale. Uwezo wa kufikiri ulipotoshwa, uwezo wa kimaadili ulichafuliwa. Mungu alikuwa amemwita Samsoni kwa wadhifa wa jukumu kubwa, heshima, na manufaa; ila kwanza angalipaswa kujua uongozi kwa kujifunza utii kwa sheria za Mungu.

👉🏼Yusufu alikuwa mtu huru mwenye maamuzi huru. Mema na mabaya yalikuwa mbele yake. Angaliweza kuchagua njia ya usafi, utakatifu, heshima, au njia ya uasherati na vitendo vya aibu. Alichagua njia sahihi, naye Mungu alitukuzwa. Samsoni, chini ya majaribu ya jinsi iyo hiyo, ambayo alijisababishia yeye mwenyewe, alijiachia akatekwa na tamaa mbaya. Njia aliyoichagua ilimfanya aishie kwenye aibu, majanga, na hatimaye kifo. Kuna utofauti gani ukilinganisha na maisha ya Yusufu.

👉🏼BWANA katika Neno lake alikuwa ameweka wazi kuwa watu wake hawapaswi kujifungamanisha na wale wasiompenda au kumcha. Watu wa jinsi hiyo hawataridhika kupewa heshima na upendo ule waustahilio pekee. Bali watadumu kutafuta kupata kutoka kwa mke au mume mcha Mungu upendeleo maalumu utakaohusika kupotoka na kuyaacha mapenzi ya Mungu.

👉🏼Kwa mwanamume mcha Mungu, na kwa kanisa alilojifungamanisha nalo, mke au rafiki wa kidunia ni mpelelezi kwenye kambi hiyo, ambaye atakuwa akitafuta daima kila fursa kusaliti mtumishi wa Kristo, na kumfichua kwa mashambulizi ya adui.

👉🏼Historia ya Samsoni hutoa fundisho kwa wale ambao tabia zao hazijaundwa, ambao hawajaingia kwenye jukwaa la maisha ya shughuli. Vijana wanaoingia kwenye shule zetu na vyuo watapata kila darasa la kuulisha ubongo. Iwapo wanatamani michezo na mizaha; iwapo wanachagua kuacha mema na kukumbatia uovu, wanayo fursa hiyo. Dhambi na utakatifu vipo mbele yao, na uchaguzi ni wao. Ila hebu wakumbuke kuwa “Kile mtu apandacho, ndicho atakachovuna.”

SIRI NI HII


📖“Lakini hakujua ya kuwa BWANA amemwacha.” Waamuzi 16:20
______________
Siku kwa siku Delila alimsumbua kwa maswali, hadi “roho yake ikadhikika hata kufa;” hata hivyo mvuto fulani ulimnasa asimudu kujinasua. Hatimaye Samsoni alizidiwa nguvu na mwanamke huyo, akaamua kumfunulia siri ya nguvu zake. “Wembe haukupita kwenye kichwa changu kamwe; maana mimi nimekuwa Mnadhiri wa Mungu, tangu tumboni mwa mama yangu. Nikinyolewa ndipo nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu.”

Mjumbe alitumwa kwa jopo la viongozi wa Wafilisti, akiwahimiza wafike upesi pasipo kukawia. Wakati shujaa amelala, nywele zake nyingi kichwani mwake zilinyolewa. Kama alivyokuwa amefanya mara tatu zilizopita, aliita, “Samsoni, Wafilisti wanakuja!” Kwa haraka akaamka, akidhania kudhihirisha nguvu zake kama ilivyokuwa hapo awali, na kuwaangamiza; ila mikono yake dhaifu ilishindwa kufanya makuu, akatambua “BWANA amemwacha.”

Baada ya kunyolewa, Delila alijaribu kumsumbua ili kujaribu nguvu zake, kwani Wafilisti hawakuthubutu kumsogelea hadi walipojua nguvu zake zimetoweka. Ndipo wakamkamata, wakamng’oa macho, kisha wakamchukua hadi Gaza. Hapa alifungwa kwa minyororo gerezani akitumikishwa kazi ngumu.

Ni aibu iliyoje kwa yeye aliyekuwa Mwamuzi na Shujaa katika Israeli!—sasa yu dhaifu, kipofu, mfungwa, aliyedhalilishwa kutumikia huduma ya kitumwa. Hatua kwa hatua amekaidi masharti ya wito wake mtakatifu. Mungu amemvumilia kwa kipindi kirefu; ila kwa sasa, kwa hiari yake mwenyewe, alipojisalimisha kwenye nguvu za uovu, kwa kufunua siri ya nguvu zake, BWANA alimwacha. Hapakuwepo mwujiza maalumu ndani ya nywele zake, ila zilikuwa ishara ya utii wake kwa Mungu; na alipoisalimisha ishara hiyo ya utii ili kukidhi haja za tamaa zake za mwili; mbaraka huo uliowakilishwa kupitia ishara hiyo nao ukatoweka.

Kama kichwa cha Samsoni kingalinyolewa pasipo kosa kwa upande wake, nguvu zake zingalibakia. Ila mwenendo wake umekuwa ukipingana na mamlaka ya Mungu kana kwamba tayari ameshazikata nywele za kichwa chake. Hivyo Mungu alimwacha avune matokeo ya upumbavu wake.

NINI SIRI?


“Delila akamwambia Samsoni, Tafadhali uniambie asili ya nguvu zako nyingi, na jinsi uwezavyo kufungwa, ili uteswe.” Waamuzi 16:6.

Waisraeli walimweka Samsoni kuwa Mwamuzi juu yao, naye alitawala juu ya Israeli kwa miaka ishirini. Ila kosa moja hufungua njia kwa kosa jingine. Alivutiwa na mihemko ya kianasa iliyomwongoza kwenye anguko. “Alimpenda mwanamke mmoja katika bonde la Soreki,” siyo mbali sana na nyumbani kwao. Jina la mwanamke huyo alikuwa Delila, “mwangamizi.” Wafilisti walitazama kwa makini mwenendo wa huyu adui yao, na alipojidhalilisha mwenyewe kwa kujifungamanisha na mwanamke huyu wa Kifilisti, walinuia, kupitia Delila, kukamilisha mpango wa kumwangamiza.

Jopo la watu wa heshima lenye kuundwa na mtu mmoja mmoja toka kila jimbo la Wafilisti walisafiri hadi bonde la Soreki. Hawakuthubutu kumshambulia akiwa anamiliki hazina ya nguvu zake tele, bali ilikuwa ni mpango wao kujifunza, ikiwezekana, siri ya nguvu zake. Hivyo walimhonga Delila atafute siri ya nguvu za Samsoni kisha awafunulie.

Kadiri msaliti alivyomsonga Samsoni kwa maswali, alimdhihaki kwa kumwambia nguvu zake zaweza kutoweka, awe sawa na watu wengine dhaifu, iwapo mambo fulani yatatendeka. Kila aliloambiwa alijaribisha, ila akagundua ni uongo kwani nguvu zake hazikutoweka. Kisha akamlilia akisema, “Mbona umenidanganya mara zote hizi, ukisema wanipenda, na roho yako haipo pamoja nami?” . . . Mara tatu Samsoni ameona ushahidi dhahiri kuwa Wafilisti wamepanga njama kumwangamiza kupitia huyu mpenzi wake; ila pale mpango huo ulipoonekana kukwama; mwanamke huyo alilia sana akidai amemhadaa, hampendi, naye mumewe akapumbazika asitambue hatari iliyoko mbele yake.
Mwamuzi huyu wa Israeli alitumia saa nyingi mbele ya mwanamke huyu mlaghai, saa ambazo angalizitumia kwa mafanikio na maendeleo ya watu wake. Tamaa hizi zenye kupofusha ziwezazo kumfanya shujaa aonekane dhaifu kabisa, zilikuwa zimeshamtawala akili na dhamiri.

Ukengeufu wa Samsoni ulikuwa taratibu na wa hakika. Mwanzoni hakudhamiria kufunua siri, ila kwa hiari amejitosa mwenyewe ndani ya wavu wa msaliti wa roho, na kamba zangu zilikuwa zikimsonga kutoka kila upande.

SHUJAA DHAIFU


“Naye ataanza kuwaokoa Israeli na mikono ya Wafilisti.” Waamuzi 13:5

Ahadi ya Mungu kwamba Samsoni ataanza “kuwaokoa Israeli na mikono ya Wafilisti” ilitimilika; ila historia ya maisha iligeukaje kuwa giza tupu na ya kutisha kwa yule ambaye alitarajiwa kuwa sifa kwa Mungu na utukufu kwa taifa! Samsoni angalikuwa mwaminifu kwa wito wake wa kimbingu, kusudi la Mungu lingalitimizwa kwa heshima na utukufu wake. Lakini alijisalimisha kwa majaribu na kujithibitisha kutokuwa mtiifu kwa wito aliokabidhiwa, hivyo utume wake ukaishia kwenye kushindwa, gereza, na hatimaye kifo.

Kimwili, Samsoni alikuwa mtu mwenye nguvu kuliko wote duniani; ila katika kujitawala, uadilifu, na msimamo thabiti, alikuwa miongoni mwa walio dhaifu mno duniani. Wengi hudhani kuwa na hisia au tamaa zisizotawalika ni ishara ya nguvu za kitabia; ila ukweli yeye ambaye anatawaliwa na kusukumwa na hisia zake huyo ndiye mtu dhaifu mno. Mtu mkuu shujaa hujulikana kwa jinsi anavyotawala hisia zake; na wala si kwa jinsi anavyoyumbishwa na hisia hizo.

Uongozi wa Mungu na ulinzi wake umekuwa juu ya Samsoni, ili aweze kukamilisha kazi aliyoitiwa. Tangia mwanzo kabisa alizungukwa na mazingira kufanikisha nguvu za kimwili, akili timamu, na uadilifu kiroho. Ila chini ya ushirikiano na marafiki waovu aliachilia kumshikilia Mungu, aliye usalama wake pekee, akaishia kusombwa na mawimbi ya uovu. Wale waliopewa majukumu na Mungu wapatapo majaribu wawe na hakika Mungu atawatunza; ila iwapo kwa hiari yao, kwa jeuri, watajisalimisha chini ya nguvu za mjaribu, wataanguka mapema au baadaye.

Wale Mungu anaokusudia wawe vyombo vyake kwa ajili ya kazi maalumu, Shetani hutumia uwezo wake mkuu kuwapotosha. Anatushambulia katika maeneo yetu ya udhaifu, akitenda kazi kupitia udhaifu wetu wa kitabia kuweza kumtawala mtu katika nyanja zote; naye anajua udhaifu huo wa kitabia iwapo unakumbatiwa, yeye atashinda. Ila hakuna yeyote apaswaye kushindwa. Mwanadamu hakuachwa peke yake kupambana dhidi ya nguvu za uovu. Msaada tele kutoka mkono imara wa Mungu umeahidiwa kwa kila roho yenye shauku kupokea msaada huo.

KABLA MTOTO HAJAZALIWA

📖“Ndipo huyo Manoa akamwomba Bwana, akisema, Ee Bwana, nakuomba, yule mtu wa Mungu uliyemtuma na aje kwetu mara ya pili, atufundishe hayo yatupasayo kumfanyia huyo mtoto atakayezaliwa.” Waamuzi 13:8.

💐Mungu mwenyewe alimtokea mkewe manoa na kumwambia kuwa atakuwa na mtoto mwanamume, na kwamba atakuwa mtu mkubwa atakayekomboa Israeli. Kisha akampatia maelekezo kamili kuhusu namna atakavyomlisha. Hebu tuuchukulie ujumbe huu kama unaotolewa maalumu kwa kila mama hapa duniani. Iwapo unataka watoto wako wawe na akili safi na bora, yakupasa uwe na kiasi katika mambo yote. Hakikisha moyo wako ni safi na akili yako ni timamu, ili kurithisha uzao wako afya bora ya kiakili na kimwili.

💐Kila mama anapaswa kulijua jukumu lake. Apate kujua kuwa tabia ya watoto wake itategemea zaidi mno tabia yake kabla na baada ya kuwazaa, kuliko ilivyo mivuto mingine ya nje iwe mizuri au mibaya. Mama aliye mwalimu bora kwa watoto wake, sharti kabla ya kuwazaa, adumishe mazoea ya kujikana nafsi na kujitawala; kwani huwarithisha sifa zake binafsi za kitabia, ziwe nzuri au dhaifu.
💐Washauri wasiofaa huwahimiza wakina mama umuhimu wa kukidhi kila tamaa na uchu wa chakula, ila ushauri huo ni potofu. Mama kwa agizo la Mungu ameagizwa kudhihirisha kiwango cha juu cha kujitawala. Na akina baba na akina mama wapaswa kujumuika pamoja katika jukumu hili. Wazazi wote wawili, hurithisha tabia zao kwa watoto wao, kiakili, kimwili, kimwenendo na kishauku yao ya ulaji.

💐Wengi huchukulia kimzaha somo la kiasi. Hujidanganya kuwa BWANA hajihusishi na mambo madogo madogo kama vile kula na kunywa. Ila endapo Mungu hajihusishi, mbona akajifunua kwa mkewe Manoa, akitoa maelekezo kamili, akimsisitiza mara mbili awe mwangalifu kutokuyapuuzia.

💐Wazazi wengi huchukulia madhara ya mivuto ya kipindi kabla ya mtoto kuzaliwa ni jambo dogo la kupuuziwa; ila mbingu hazichukulii hivyo. . . . Kwa maneno yaliyoongelewa kwa mama huyu wa Kiebrania, Mungu huongea kwa wakina mama wote wa zama zote.

Tuesday, May 2, 2017

MUNGU NI CHEO CHENYE NAFSI 3

MUNGU BABA, MUNGU MWANA NA MUNGU ROHO MTAKATIFU. 

KWA NINI MUNGU MWANA YAANI YESU KRISTO ALIKUFA MSALABANI NA SIYO MUNGU BABA AU MUNGU ROHO MTAKATIFU?
 
1. Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu ni baraza uumbaji ambalo liliamua Mungu Mwana yaani Yesu Kristo awe msemaji na Mtendaji mkuu. Yohana 1:1-3, 14 "Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu. 
 Vyote vilifanyika kwa huyo: wala pasipo yeye hakukufanyika cho chote kilichofanyika... Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu: nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba: amejaa neema na kweli. "
 
Wakolosai 1:14-20 "... ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi: naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana: ikiwa ni viti vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka: vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye. Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa: naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote. Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae: na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake, akisha kufanya amani kwa damu ya msalaba wake:kwa yeye, ikiwa ni vitu vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni.".
 
Yesu ndiye aliyemwambia Adamu, "walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika". Ndiyo sababu Yesu anaitwa Neno. Msemaji mkuu wa serikali ya mbinguni.
Yesu alikufa msalabani kwa niaba ya mwanadamu. Kwa kuwa ndiye aliyesema 'utakufa hakika'. Kama asingekufa na wanadamu wasamehewe basi shetani angedai kuwa Mungu ni mwongo. Ndiyo maana neema na haki zilibusiana msalabani. Yaani neema mwanadamu asamehewe dhambi alipotenda. Haki mwanadamu atii amri na maagizo ya Mungu baada ya kusamehewa dhambi. Yesu alikufa msalabani ili kumtetea mwanadamu asife na pia kutetea maagizo au amri zake zisipuuzwe. Ndiyo maana mtu anapoasi anamrudisha Yesu msalabani. 

Waebrania 6:4-6 "Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa wahirika wa Roho Mtakatifu, na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu... Kwa kuwa wamsulubisha Mwana wa Mungu mara ya pili...".

Saturday, April 29, 2017

GHARAMA YA UONGO

"Midomo ya uongo ni chukizo kwa Bwana; Bali watendao uaminifu ndio furaha yake" (Mithali 12:22)
 
Kutoka Shekemu, wana wa Israeli walirejea katika kambi lao huko Gilgali. Muda si mrefu walipokuwa hapa walitembelewa na wajumbe wa ajabu, waliotamani kufanya mkataba pamoja nao. Mabalozi hawa walieleza kuwa walitokea nchi ya mbali, na hili lilionekana kuthibitishwa na hali ya mwonekano wao. Mavazi yao yalikuwa makuukuu na yalikuwa yameraruka, viatu vyao vilikuwa vimetobokatoboka, chakula chao kilikuwa kimekauka na kuvunda, na vibuyu vyao vya mvinyo vilikuwa vikuukuu vilivyorarukararuka na kutiwa viraka, kana kwamba vilirekebishwa haraka njiani wakiwa safarini…. Mionekano hii ilifanikiwa kuwashawishi wenyeji…. “Naye Yoshua akafanya amani pamoja nao, na kufanya agano nao, ili kwamba waachwe hai; na wakuu wa mkutano wakawaapia.” Hivyo ndivyo mkataba huu ulivyofanyika….
 
Lakini mambo yangeliwaendea vyema Wagibeoni endapo wangezu-ngumza na Israeli kwa uaminifu. Wakati ambapo kujinyenyekesha kwao na kumfuata Yehova kuliwapatia ulinzi wa maisha yao, udanganyifu wao uliwaletea fedheha na utumwa. Mungu alikuwa ameandaa mpango kwamba wote ambao wangeukana upagani, na kujifungamanisha na Israeli, wangeshiriki baraka za agano lake. Walihusishwa kwa namna hiyo katika masharti yaliyosema, “mgeni akaaye kati yenu,” na isipokuwa mambo mengine machache, wageni hawa walipaswa kupata fadhila na fursa sawa na Israeli. Maelekezo ya Bwana yalikuwa—“Na mgeni akikaa pamoja nawe katika nchi yako, usimdhulumu. Mgeni akaaye pamoja nawe atakuwa kama mzalia kwenu; mpende kama nafsi yako; kwa maana ninyi mlikuwa wageni katika nchi ya Misri; Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu” (Law. 19:33, 34).
 
Hayo ndiyo masharti ambayo kwayo Wagibeoni wangeliweza kupokelewa, kama isingelikuwa ule udanganyifu ambao walikuwa wameutumia. Haikuwa fedheha ndogo kwa raia hao wa “miji ya kifalme,” “tena watu wake wote walikuwa ni mashujaa,” kuwa wapasua-kuni, na wateka-maji kwa ajili ya Israeli wakati wote. Lakini walikuwa wamejitwalia vazi la umaskini kwa ajili ya kusudi la udanganyifu, na lilifungamanishwa juu yao kama nembo ya utumwa wa kudumu. Kwa hiyo katika vizazi vyao vyote hali yao ya utumwa ingeliweza kushuhudia chuki ya Mungu dhidi ya udanganyifu.

Sunday, April 23, 2017

KIZAZI KIPYA!!

Ni dhahiri kweli kizazi kipya kinazidi kuwa na nguvu sana miongoni mwetu hasa miaka ya hivi karibuni, wamekuwa na Television zao, radio zao na kumbi mbalimbali kwa ajili ya matamasha yao mbali mbali.
 
Je umewahi kujiuliza nyuma ya kizazi kipya pamoja na style mbali mbali za uimbaji, mavazi na aina ya maisha waishiyo nani aongozaye????
Leo nitapenda kuongelea aina ya maisha ya kizazi kipya kupitia style mpya ya uvaaji wa vazi la jeans kama wengi walijuavyo japo yako mengi hayo tutazidi kuyaongea kadri Mungu atupatiavyo pumzi ya uhai.

Miaka ya nyuma hasa miaka ya 80 na 90 hapo tulizoea kuwaona watoto ama watu wavaao nguo zilizopasuka matakoni ama magotini ni jamii ya watu maskini sana, lakini leo hizo nguo huvaliwa na watu matajiri sana tena imekuwa kama fasion siku hizi kina kaka na dada uzivaa sana....
Sikia ndugu yangu Shetani ni adui wa mwanadamu amejifunza mbinu nyingi sana na namna ya kukamata mioyo ya watu na kuiongoza apendapo kwa kutumia wasanii na watu maarufu amefanikisha kukamata akili za vijana na wazee wengi nao uiga aina fulani ya maisha ama mavazi kupitia wasanii maarufu huo ni mtego wa adui kuongoza watu kwa siri bila kujua.
Uvaaji huu wa hizi nguo zilizotoboka kwanza zinakushusha heshima na kukuweka mvaaji katika viwango vya chini vya kitabia, pili kwa madada zetu wazivaapo uachia sehemu baadhi ya viungo vyao kuwa wazi kama mapaja na sehemu zingine za siri ambazo hakupaswa mwanamme mwingine kumuona isipokuwa mume wake, kwa njia hiyo Shetani amefanikisha kuwafanya madada wengi kuwa mabango ya kuwafanya wanaume kuingia kwenye tamaa ya ngono kwa aina ya hizo nguo hivyo si salama kwa wale wampendao Mungu kuzivaa....

Television ama runinga.... Shughuli zetu huathiri IQ na EQ zetu. Kadri tunavyoangalia burudani ktk runinga, ndivyo ubunifu unavyoshuka pamoja na alama ktk mitihani. Pamoja na hayo, hushindwa kudhibiti mihemko - pamoja na hayo huwa kuna ongezeko la uhalifu wa kutumia nguvu na wa ngono. Mtandao ya burudani, video na michezo ya video pia vina athari hasi. Kama alivyosema Mtume Paulo; huwa tunabadilishwa kwa kuona. (soma 2 Wakorintho 3:18).

Tuko vitani na uwanja wa mapambano ni ndani ya mioyo yetu ruhusu Roho Mtakatifu akuongoze soma sana neno la Mungu hapo ndipo salama yetu ilipo...


MSAIDIZI ASIYEONEKANA

“Hapatakuwa mtu yeyote atakayeweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako; kama nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe; sitakupungukia wala sitakuacha”(Yoshua 1:5).

Jifunze kwa kina uzoefu wa Israeli katika safari zao kuelekea Kanaani…. Tunahitaji kudumisha moyo na akili katika mafunzo, kwa kurejesha upya kumbukumbu ya masomo ambayo Bwana aliwafundisha watu wake wa zamani. Na hivyo, kama alivyokusudia iwe kwao, mafundisho ya Neno lake yataendelea daima kutuvutia na kuwa na mguso wa pekee kwetu.

Yoshua alipoondoka asubuhi kabla ya kuuhusuru Mji wa Yeriko, palitokea mbele yake shujaa aliyekuwa amejiandaa tayari kabisa kwa ajili ya vita. Na Yoshua akauliza, “Je! Wewe u upande wetu, au upande wa adui zetu? Naye akajibu, La, lakini nimekuja sasa, nili Amiri wa jeshi la Bwana. Kama macho ya Yoshua yangalikuwa yamefumbuliwa kwa jinsi ile ambayo mtumishi wa Elisha alifumbuliwa pale Dothani, na kama angaliweza kustahimili tukio hilo, angaliweza kuwaona malaika wa Bwana wakiwa wamewazunguka wana wa Israeli; kwa maana jeshi imara la mbinguni lilikuwa limekuja ili kupigana kwa niaba ya watu wa Mungu, na Kapteni wa jeshi la Bwana alikuwa hapo ili kuongoza. Yeriko ilipoanguka, hakuna mkono wowote wa mwanadamu uliogusa hizo kuta za mji, kwa maana malaika wa Bwana waliziangusha ngome zake, na kuingia ndani ya maboma hayo ya adui. Hawakuwa Israeli, bali Yule Kapteni wa jeshi la Bwana ndiye aliyeiporomosha na kuitwaa Yeriko. Lakini Israeli ilikuwa na sehemu yake ya kutenda ili kuonesha imani yao kwa Kapteni wa wokovu wao.

Vita vinapaswa kupiganwa kila siku. Pambano kuu linaendelea ndani ya kila roho, kati ya mkuu wa giza na Mkuu za uzima…. Kama mawakala wa Mungu ni sharti mjisalimishe chini Yake, ili aweze kupanga na kuelekeza na kupigana vita kwa ajili yenu, mkishirikiana Naye. Mkuu wa uzima ndiye anayeongoza kazi Yake. Anapaswa kuwa pamoja nanyi katika vita vyenu vya kila siku dhidi ya nafsi, ili mweze kuwa waaminifu na watiifu kwa kanuni; ili tamaa ya mwili, inapopambana ili kutawala, iweze kutiishwa kwa njia ya neema ya Kristo; ili mweze kujitokeza mkiwa zaidi ya washindi kupitia Kwake ambaye ametupenda. 

Yesu amekuwa kwenye eneo hasa la vita. Anajua nguvu ya kila jaribu. Anajua kabisa jinsi ya kukabiliana na kila dharura, na jinsi ya kukuongoza kupitia kila njia ya hatari. Kwa hiyo, kwa nini usimtumaini Yeye?

Friday, April 21, 2017

MAMBO YANAYOONDOA FAHAMU ZA MWANADAMU:

"Imeandikwa hivii; "Uzinzi na Divai na Divai mpya huondoa fahamu za mwanadamu" Hosea 4:11.
 
Dhambi ya uzinzi licha ya kwamba sio uzinzi peke yake utakaowakosesha wengi wasiingie mbinguni; lakini neno la Mungu limeizungumza kwa uchungu madhara yake kama mwanadamu angeliielewa. Paulo katika Wakorintho pia alisema mtu akizini msichangamane naye na kwa baadhi ya makanisa mtu anayefumwa katika uzinzi huondolewa katika ushirika wa kanisa. Dhambi hii ni kweli ni sawa tu na dhambi zingine; lakini imetajwa katika dhambi kuu mbili zinazoondoa fahamu za mwanadamu.
 
Biblia inaelewa kwa uwazi kupitia nabii Hosea kwamba Uzinzi na Divai huundoa fahamu za mwanadamu. Mtumishi wa Mungu Sulemani ingawa aliandika yeye mwenyewe katika Kitabu cha Mithali kwamba; "Mtu aziniye na mwanamke hana akili, afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake" Bado kama mwanadamu anayo historia ya kutenda kosa hilo kwa kuoa akina mama 700+300 masuria jumla akawa na 1,000 wake wa kulala nao kimapenzi.
 
Uzinzi na ulevi ni dhambi kuu zinazovuma na zimeshika nafasi ya kwanza katika ulimwengu wa sasa. Wachungaji, mapadre, maaskofu, watumishi wengi wa Mungu, wainjilisti, wahubiri, na waumini wa madhehebu mbalimbali hatuko nyuma katika kujishughulisha na dhambi ya uzinzi na ulevi( Divai) ingawa dhambi ni dhambi bila kujali ni uongo, majungu, masengenyo, wizi wa zaka, ulawiti, ubakaji, uchonganishi, dharau, kiburi, majivuno na kiola aina ya ubaya unaomwandama mwanadamu; ila katika kuondoa ufahamu wa mwanadamu (yaani anakuwa punguwani asiyejielewa kiroho na kuwa mtumwa wa uovu huo) ni Uzinzi na ulevi kama asemavyo Mungu kupitia nabii Hosea, na mtume Paulo.
 
Angalia mtu akilewa anavyokosa adabu, asivyojiheshimu, anavyopiga kelele, anavyosumbua mke au mme wake, anavyotishia watu, anavyopiga mke, anavyopiga mume, anavyopiga watoto! Je, ulevi na kunywa japo kidogo mbele za Mungu ni halali? imeandikwa nini katika Isaya 28:7? ni kosa kumpa mtu kileo. Katika Biblia yaani maandiko matakatifu hakuna fungu linalosema kunywa kidogo ila usilewe, halipo ila ni fundisho miongoni mwa mafundisho ya shetani kwamba watu wanywe kidogo ila wasilewe!
 
Niliwahi kuona mtu mmoja aliyejiita mtumishi wa Mungu akiwa amevalia kanzu akienda katika tukio la ujenzi wa makaburi akawa akizibariki pombe! wakati huo nikiwa gizani kama yeye niliona ni jambo jema; baada ya kupata mafunuo ya Mungu kupitia neno lake nikagundua yule alikuwa mtumishi wa shetani aliyevaa kanzu ya kondoo.
Ulevi umekatazwa kabisa; wapendwa wakristo wenzangu; Uzinzi na ulevi tumwombe Mungu atusaidie dhambi hizi zinaondoa fahamu za mwanadamu; na ujue ya kwamba Fahamu za mtu zikiondoka mtu huyo huitwa mwendawazimu. Soma tena Hosea 4:11 ujue mambo yanayoondoa fahamu za mwanadamu. Mungu halazimishi, ila anaonya ili isiwe siku ya kutupwa katika ziwa la moto ukamlaumu kwamba hukumu zake si za haki. Ni lazima siku zote Mungu aonye ukatae ili siku ya hukumu maneno yaleyale uliyoyakataa yawe sheria mbele zake ya kukugeuka. Amua leo kumtii Mungu katika kila jambo ili uwe salama. Haleluya!

Tuesday, April 18, 2017

WAWILI WANAOFANANA

“Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uhai wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo”
(Luka 12:15, Biblia Habari Njema)..

Laana ambayo Balaamu hakuwa ameruhusiwa kuitamka dhidi ya watu wa Mungu, hatimaye alifanikiwa kuwasababishia kwa kuwashawishi waingie dhambini..
Balaamu alishuhudia mafanikio ya njama zake za kishetani. Aliona laana ya Mungu ikipatilizwa kwa watu Wake, na maelfu wakianguka chini ya hukumu Zake; lakini haki ya Mungu iliyoadhimu dhambi katika Israeli haikuwaruhusu wale wajaribu kusalimika. Katika vita Israeli ya dhidi ya Wamidiani, Balaamu aliuawa kwa upanga….
Mauti ya Balaamu yalikuwa yanafanana na yale ya Yuda, na tabia zao hubeba ufanano bayana kabisa wa mmoja kwa mwenzake. Watu hawa wawili walijaribu kuunganisha utumishi wa Mungu na mali, na wakashindwa vibaya sana. Balaamu alimkiri Mungu wa kweli, na akadai kumtumikia; Yuda alimwamini Yesu kama Masihi, na akaungana na wafuasi Wake. Lakini Balaamu alitafuta kuufanya utumishi wa Yehova kuwa kama njia ya kujipatia utajiri na heshima ya kidunia; na aliposhindwa katika hili, alijikwaa na kuanguka na akavunjika. Yuda alitegemea kwamba katika kujihusianisha na Kristo angejipatia mali na kupandishwa hadhi ya juu katika ufalme huo wa kiulimwengu, ambao, kama alivyoamini, Masihi alikuwa akielekea kuuanzisha. Kushindwa kutimia kwa matarajio yake kulimsukuma kwenda katika uasi na uangamivu. Balaamu na Yuda walikuwa wamepokea nuru kuu na walifurahia fadhila maalumu, lakini dhambi moja iliyoendekezwa iliharibu kabisa tabia yote na kusababisha uangamivu wao….
Dhambi moja ambayo mtu hataki kuiacha, kidogo kidogo, huhafifisha tabia, ikisababisha uwezo wake wote wa uadilifu kutawaliwa na shauku zake ovu. Kuondolewa kwa ulinzi mmoja toka katika dhamiri, uendekezaji wa tabia moja ya uovu, upuuziaji mmoja wa madai ya juu ya wajibu, huvunja ulinzi wa roho na humfungulia Shetani njia ya kuingia ndani na kutuongoza kwenye ukengeufu. Njia pekee salama ni kuyafanya maombi yetu yamiminike kila siku kutoka katika moyo mnyofu, kama alivyofanya Daudi, “Zishikilie nyayo zangu katika njia Zako, ili hatua zangu zisiteleze” (Zaburi 17:5, NKJV).

Monday, April 17, 2017

WAJIBU AU SHAUKU

“Bali mmebatilisha shauri Langu, Wala hamkutaka maonyo Yangu” (Mithali 1:25).

Wakati wa usiku malaika wa Mungu alimjia Balaamu akiwa na ujumbe, “Usiende pamoja nao; wala usiwalaani watu hawa, maana wamebarikiwa.”…
Kwa mara ya pili Balaamu alijaribiwa tena. Katika kujibu ushawishi wa wale wajumbe alidai kuwa makini na mwenye uadilifu mkubwa mno, akiwahakikishia kwamba hakuna kiasi chochote cha dhahabu na fedha ambacho kingeweza kumshawishi kwenda kinyume na mapenzi ya Mungu. Lakini alitafuta kukubaliana na ombi la mfalme huyo; na licha ya kwamba alikuwa amedhihirishiwa bayana mapenzi ya Mungu, aliwahimiza wale wajumbe wangoje, ili aweze kuulizia tena kwa Mungu; kana kwamba Yeye Asiye na Ukomo alikuwa mwanadamu, awezaye kughilibiwa.
Wakati wa usiku Bwana alimtokea Balaamu na kusema, «Kwa kuwa watu hawa wamekuja kukuita, enenda pamoja nao; lakini neno lile nitakalokuambia ndilo utakalolitenda, basi.» Huo ndio umbali ambao Bwana angeliweza kumruhusu Balaamu ayafuate mapenzi yake mwenyewe, kwa sababu alikuwa amedhamiria juu ya hilo. Hakutafuta kuyatenda mapenzi ya Mungu, bali alichagua njia yake mwenyewe, na kisha akajitahidi kujipatia kibali cha Bwana.

Wapo maelfu hivi leo wanaoenenda katika njia ya namna hiyo. Wasingeliweza kuwa na ugumu wowote wa kuuelewa wajibu wao kama ungelipatana na mielekeo yao. Umeleezwa bayana mbele yao katika Biblia au umeoneshwa waziwazi kwa mazingira na mawazoni. Lakini kwa sababu ushahidi huu hupingana na shauku na mielekeo yao mara kwa mara wanauweka pembeni na kuthubutu kumwendea Mungu ili kutafuta kujua wajibu wao. Kwa uangalifu mkubwa unaoonekana dhahiri wanaomba kwa muda mrefu na kwa bidii ili wapate nuru. Lakini Mungu hatadhihakiwa. Kwa kawaida huwaruhusu watu wa namna hiyo wafuate shauku zao wenyewe na kukabiliana na matokeo husika…. 

Mtu anapouona wajibu wake bayana, hebu asithubutu kumwendea Mungu akiwa na ombi kwamba asamehewe ili asiufanye. Badala yake anapaswa, kwa roho na unyenyekevu na kujisalimisha, aombe nguvu na hekima ya kimbingu ili kutimiza madai yake.

Sunday, April 16, 2017

MIPANGO YA AMANI NA MAANDALIZI YA VITA

Tunaishi katika ulimwengu huu wa ajabu. Kila mmoja anaafiki kwamba tungeipatia nafasi amani; lakini basi, zile chuki zilizokandamizwa kwa kipindi cha karne fulani zilizopita, zinalipuka na kuwa vita ya wazi. Nabii Mika na Yoeli walitabiri kwamba wakati ule ule mataifa yatakapokuwa yanasema juu ya shauku yao ya kuwa na amani (Mika 4:1-3) WATALAZIMIKA KUJIANDAA KWA VITA...kutokana na shauku yao waliyo nayo dhidi ya majirani zao (Yoeli 3:9-13).....

Marekani imefanya shambulizi la makombora takriban 50 ,yalipigwa katika kambi ya jeshi la anga mjini Homs nchini Syria.
Awali maafisa wa Marekani walisema wana mpango wa kuchukua hatua za kijeshi baada ya Syria kushutumiwa kutumia silaha za kemikali katika mji unaodhibitiwa na waasi, ambapo watu kadhaa wamepoteza maisha.Rais wa Marekani Donald Trump amesema ameamuru kutekelezwa kwa mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Syria huku akitoa wito kwa mataifa yote yaliyostaarabika kukomesha vitendo vya mauaji na umwagaji damu nchini humo
URUSI YACHUKIZWA NA MAREKANI KUISHAMBULIA SYRIA
Urusi imechukizwa na uamuzi wa Marekani wa kuishambulia kambi ya jeshi la anga mjini Homs nchini Syria kwa makombora.Urusi inaunga mkono serikali ya Rais Bashar al-Assad[SYRIA] na imekashifu shambulizi hilo ambalo linadaiwa kuua watu sita.

CHINA,KOREA KUSINI zimeionya kuiadhibu Pyongyang iwapo itarusha kombora lolote
Mataifa mawili ya bara Asia, yametoa onyo kali dhidi ya utawala wa Pyongyang, kwamba itaadhibiwa vikali, iwapo itadhubutu tena kufanyia majaribio zana zake za kinuklia.

Mataifa hayo, Korea Kusini na China, yamekiri kuchukua hatua kali dhidi ya Korea Kaskazini, ikiwa tena itafanyia majaribio zana zake za kitonoradi zinazovuka mipaka ya kimataifa.

MAREKANI YATISHIA kuiadhibu Korea KaskaziniTrump: "tutaidhibiti Korea Kaskazini".." HATUTAIVUMILIA KOREA KASKAZINI"
Rais Trump amesema kuwa Marekani imejiandaa kibinafsi kukabiliana na tishio la nyuklia linaloletwa na Korea Kaskazini.
KOREA KASKAZINI : Tutatumia ''silaha kali'' kujilinda dhidi ya US

Korea Kaskazini imesema kuwa itajitetea kwa kutumia silaha kali ili kujibu hatua ya Marekani kupeleka wanamaji wake katika rasi ya Korea.
Wizara ya maswala ya kigeni ilinukuu shirika la habari la serikali KCNA lililosema kuwa hatua hiyo ya Marekani inaonyesha uvamizi wa kijinga uliofika awamu yenye hatari kubwa.

Jeshi la Marekani katika maeneo ya Pacific limesema kuwa hatua hiyo inalenga kuonyesha Marekani imejiandaa kwa lolote lile.
Zamani sana Biblia ilionyesha picha hii ya mgogoro wetu wa sasa wa kuwa na AMANI au VITA, kisha ikatangaza kwamba amani ya kudumu itatawala katika dunia hii wakati ule tu YESU ATAKAPOKUJA.

Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi ya vita; angalieni, msitishwe; maana hayo hayana budi kutukia; lakini ule mwisho bado.
- Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.Mathayo 24 :6- 7
Luka 21 : 28 - Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.

IJUE VIZURI PASAKA, USITEKWE NA DUNIA

Basi, kabla ya sikukuu ya pasaka ,Yesu,hali akijua kwamba saa yake imefika,atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba,naye amewapenda watu wake katika ulimwengu,aliwapenda upeo,Yesu hali akijua ya kwamba Baba amempa vyote mikononi mwake,na ya kuwa anatoka kwa Mungu naye anakwenda kwa Mungu,aliondoka chakulani,akaweka kando mavazi yake,akatwaa, kitambaa akajifunga kiunoni.Kisha akatia majia katika bakuli,akaanza kuwatawadha miguu na kuifuta kwa kile kitambaa alichojifunga….Basi alipokwisha kuwatawadha miguu, na kuyatwaa mavazi yake, na kuketi tena,akawaambia, Je! Mmeelewa na hayo niliyowatendea? Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu,nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo KUTAWADHANA miguu ninyi kwa ninyi...Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili kama mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo. YOHANA 13:1-151

Bwana Yesu usiku ule aliotolewa alitwaa mkate,Naye akiisha kushukuru akaumega, akasema,Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa UKUMBUSHO wangu. Na vivi hivi baada ya kula akakitwaa kikombe, akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu; fanyeni hivi kila mnywapo, kwa UKUMBUSHO wangu. Maana kila mwulapo mkate huu na kukinywea kikombe hiki, MWAITANGAZA MAUTI YA BWANA HATA AJAPO WAKORINTHO 11:23-26
KUHUSU (EASTER)?

Easter Ni sherehe inayojulikana sana ambayo,inaadhimishwa na makanisa yetu ya siku hizi. Walakini hii pia ilisherehekewa na wapagani muda mrefu kabla ya ufufuo wa Kristo.
Siku zote Pasaka inaangukia Jumapili ya kwanza baada ya mwezi mpevu (full moon) mara tu baada ya jua kuwa kichwani kaskazini ya Ikweta (Equinox ---March 2l).Wapagani wale wa zamani za kale waligundua ya kwamba kila kitu kilionekana kupata uzima mpya mapema katika majira yale ya kuchipua (Spring), mara tu baada ya jua kupita mstari wa ikwinoksi (equinox) kaskazini ya Ikweta. Basi wakachagua siku moja katika majira ya kuchipua [Machi, Aprili, Mei] ili KUMHESHIMU mungu WA KIKE WA UZAZI. Siku ile ikatolewa kwa ISHTA (ISHTAR), mungu wa kike wa uzazi, kwa sababu ya uhai mpya na kukua kwa mimea ya asili.

Neno lilo hilo ISTA (EASTER) limeandikwa kwa herufi nyingine zisizokuwa za lugha yenyewe kutokana na jina la mungu huyo wa kike ISHTA (ISHTAR), ambaye ibada yake iliwekewa ukumbusho wake kwa kutumia sikukuu ya Ista (Easter) [Pasaka]. Mara nyingi Wakristo walei [wa kawaida] wameuliza ya kwamba ule mkate mdogo kama sungura (bunny rabbit) na yai la Ista (Easter egg) vina uhusiano gani na ufufuo wa Kristo. Kusema kweli, havina uhusiano wo wote na [ufufuo] huo. Sungura alichaguliwa kwa sababu alikuwa anazaa sana. Yai pia lilichaguliwa kwa sababu lilikuwa nembo ya kuzaa sana. Hata nembo hizo zenyewe, mkate mdogo kama sungura na mayai, vinatunzwa kama ukumbusho wa asili yake ya kipagani [ya siku hiyo]. Mifano hii imetolewa ili kuonyesha tu jinsi ilivyokuwa rahisi kwa Mwovu kulazimisha mawazo yale ya kipagani juu ya kanisa lile. Swali linakuja mawazoni mwetu, Hivi ni kweli tunaifuata Biblia katika mafundisho yetu yote ya dini? Iwapo MAPOKEO na DESTURI za kipagani zimeweza kuteleza kwa urahisi na kuingia kanisani, ni vipi kuhusu mafundisho mengine ya dini?

Hatuna amri yo yote kuhusu uadhimishaji wa ufufuo au kuzaliwa kwa Kristo. Tunaweza kutafakari juu ya ufufuo Wake na kuzaliwa Kwake kwa wakati wo wote ule na katika siku yo yote ile ya mwaka. Macho yetu na yafumbuke ili tupate kuyatambua mafundisho hayo ya uongo na kuendelea kuwa watiifu kwa ile kweli halisi katika mfumo wake wa asilia.

TOKA KABURI HADI UTUKUFU

“Nikamnyenyekea Bwana wakati huo, nikamwambia,… Nami nakuomba nivuke, nikaione hiyo nchi nzuri iliyoko ng’ambo ya Yordani, mlima ule mzuri, na Lebanoni. Lakini Bwana alikuwa amenikasirikia kwa ajili yenu, asinisikize; Bwana akaniambia, Na ikutoshe, usinene nami zaidi jambo hili”
(Kumbukumbu 3:23-26).

Kamwe haikuwahi kutokea, hadi pale vilipodhihirishwa katika kafara ya Kristo, ndipo ambapo haki na upendo wa Mungu vilioneshwa kwa kiwango kikubwa sana kuliko katika kushughulika Kwake na Musa. Mungu alimzuia Musa asiingie Kanaani, ili afundishe somo ambalo kamwe halipaswi kusahaulika—kwamba Yeye anahitaji utii kamili, na kwamba wanadamu wanapaswa kujihadhari ili wasijitwalie utukufu unaomstahili Muumba wao. Asingeweza kujibu ombi la Musa aliposihi apewe nafasi ya kushiriki urithi wa Israeli, lakini Mungu hakumsahau wala kumwacha mtumishi Wake. Mungu wa mbinguni alielewa mateso ambayo Musa alikuwa ameyastahimili; alikuwa ametazama kila tendo la utumishi wenye uaminifu katika miaka hiyo yote ya mapambano na majaribu. Juu ya Mlima Pisga, Mungu alimwita Musa kuingia katika urithi mtukufu sana usio na ukomo ukilinganishwa na ule wa Kanaani ya duniani..

Katika ule mlima ambako Yesu alibadilikia sura, Musa alikuwepo pamoja na Eliya, waliokuwa wamehamishwa kwenda mbinguni. Walitumwa kama wabeba-nuru na utukufu kutoka kwa Baba hadi kwa Mwanawe. Kwa hiyo, dua ya Musa, iliyotamkwa karne nyingi hapo kabla, hatimaye ilijibiwa. Alisimama kwenye “mlima ule mzuri,” ndani ya urithi wa watu wake….

Musa alikuwa mfano wa Kristo…. Mungu aliona vyema kumfunza Musa katika shule ya mateso na umaskini kabla hajaandaliwa kuliongoza jeshi la Israeli hadi Kanaani ya duniani. Israeli wa Mungu, wanaosafiri kuelekea Kanaani ya mbinguni, wanaye Amri Jeshi asiyehitaji mafundisho ya wanadamu ili kumwandaa kwa ajili ya utume Wake kama kiongozi wa kimbingu; hata hivyo alikamilishwa kupitia mateso; na “kwa kuwa [Yesu] Mwenyewe aliteswa alipojaribiwa, aweza kuwasaidia wao wanaojaribiwa” (Ebr. 2:10, 18). Mkombozi wetu hakuonesha udhaifu au kasoro yoyote ya kibinadamu; hata hivyo alikufa ili kutununulia sisi urithi wa kuingia katika ile Nchi ya Ahadi.

“Na Musa kweli alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu kama mtumishi,… bali Kristo, kama mwana, juu ya nyumba ya Mungu; ambaye nyumba Yake ni sisi, kama tukishikamana sana na ujasiri wetu na fahari ya taraja letu mpaka mwisho” (Ebr. 3:5, 6).

UNABII WA UJIRA

“Wakiiacha njia iliyonyoka, wakapotea, wakiifuata njia ya Balaamu, mwana wa Beori, mtu ambaye hakuwa na kipingamizi chochote kwa uovu ilimradi ungelimpatia ujira” (2 Petro 2:15, Fasiri ya Phillips).

Wakati fulani Balaamu alikuwa mtu mwema na pia nabii wa Mungu; lakini sasa alikuwa ameasi, na alikuwa amejiingiza katika tamaa; hata hivyo bado alidai kuwa mtumishi wa Mungu Mkuu. Hakuwa mtu asiyejua utendaji wa Mungu kwa ajili ya Israeli; na wale wajumbe walipomweleza ujumbe waliokuja nao, alifahamu vyema kuwa ulikuwa wajibu wake kukataa zawadi za Balaki na kuwaondosha hao mabalozi. Lakini alithubutu kuchezacheza na majaribu, akawahimiza wajumbe hao wakae pamoja naye usiku huo, huku akitamka kuwa asingeliweza kutoa jibu lolote la hakika hadi atakapokuwa ameomba mashauri ya Bwana. Balaamu alijua kuwa laana yake isingeweza kuwadhuru Israeli. Mungu alikuwa katika upande wao, na kadiri walivyodumu kuwa waaminifu Kwake hakuna uwezo wowote mwovu wa kidunia au jehanamu ambao ungeweza kuwashinda. Lakini kiburi chake kilidanganywa kwa maneno ya wale wajumbe, “Yeye umbarikiye hubarikiwa, na yeye umlaaniye hulaaniwa.” Rushwa ya zawadi za thamani na matarajio ya kutukuzwa viliamsha tamaa yake. Alikubali kwa ulafi hazina zilizoahidiwa kwake, na kisha, wakati akidai kuwa mtii kamili kwa mapenzi ya Mungu, alijaribu kukubaliana na matakwa ya Balaki….
Dhambi ya tamaa ya mali, ambayo Mungu anaitaja kama ibada ya sanamu, ilikuwa imemfanya kuwa mhanga wa mazingira, na kupitia kosa hili moja Shetani alipata nafasi ya kumtawala kabisa. Hili ndilo lililosababishia uangamivu wake. Daima yule mjaribu anaendelea kuwasilisha manufaa na heshima za kiulimwengu ili kuwashawishi watu waache utumishi wa kazi ya Mungu. Anawaambia kwamba uangalifu wao uliopita kiasi ndio unaowazuia wasipate mafanikio. Kwa namna hiyo wengi wanashawishika ili kuthubutu kutoka kwenye njia ya uadilifu kamili. Hatua moja mbaya huifanya nyingine kuwa rahisi zaidi, na huendelea kuwa na ufidhuli zaidi na zaidi. Watafanya na kuthubutu mambo ya kutisha sana mara wanapokuwa wamejiingiza mara moja chini cha utawala wa ulafi na tamaa ya ukuu. Wengi hujidanganya kwamba wanaweza kutoka kwenye uadilifu kamili kwa muda fulani,… na baada ya kufanikisha lengo lao, wanaweza kubadilisha mwenendo wao wakati watakapoona kuwa vyema. Watu wa namna hiyo wanajifunga wenyewe katika mtego wa Shetani, na ni kwa nadra kwamba watajinasua.