Sunday, April 23, 2017

KIZAZI KIPYA!!

Ni dhahiri kweli kizazi kipya kinazidi kuwa na nguvu sana miongoni mwetu hasa miaka ya hivi karibuni, wamekuwa na Television zao, radio zao na kumbi mbalimbali kwa ajili ya matamasha yao mbali mbali.
 
Je umewahi kujiuliza nyuma ya kizazi kipya pamoja na style mbali mbali za uimbaji, mavazi na aina ya maisha waishiyo nani aongozaye????
Leo nitapenda kuongelea aina ya maisha ya kizazi kipya kupitia style mpya ya uvaaji wa vazi la jeans kama wengi walijuavyo japo yako mengi hayo tutazidi kuyaongea kadri Mungu atupatiavyo pumzi ya uhai.

Miaka ya nyuma hasa miaka ya 80 na 90 hapo tulizoea kuwaona watoto ama watu wavaao nguo zilizopasuka matakoni ama magotini ni jamii ya watu maskini sana, lakini leo hizo nguo huvaliwa na watu matajiri sana tena imekuwa kama fasion siku hizi kina kaka na dada uzivaa sana....
Sikia ndugu yangu Shetani ni adui wa mwanadamu amejifunza mbinu nyingi sana na namna ya kukamata mioyo ya watu na kuiongoza apendapo kwa kutumia wasanii na watu maarufu amefanikisha kukamata akili za vijana na wazee wengi nao uiga aina fulani ya maisha ama mavazi kupitia wasanii maarufu huo ni mtego wa adui kuongoza watu kwa siri bila kujua.
Uvaaji huu wa hizi nguo zilizotoboka kwanza zinakushusha heshima na kukuweka mvaaji katika viwango vya chini vya kitabia, pili kwa madada zetu wazivaapo uachia sehemu baadhi ya viungo vyao kuwa wazi kama mapaja na sehemu zingine za siri ambazo hakupaswa mwanamme mwingine kumuona isipokuwa mume wake, kwa njia hiyo Shetani amefanikisha kuwafanya madada wengi kuwa mabango ya kuwafanya wanaume kuingia kwenye tamaa ya ngono kwa aina ya hizo nguo hivyo si salama kwa wale wampendao Mungu kuzivaa....

Television ama runinga.... Shughuli zetu huathiri IQ na EQ zetu. Kadri tunavyoangalia burudani ktk runinga, ndivyo ubunifu unavyoshuka pamoja na alama ktk mitihani. Pamoja na hayo, hushindwa kudhibiti mihemko - pamoja na hayo huwa kuna ongezeko la uhalifu wa kutumia nguvu na wa ngono. Mtandao ya burudani, video na michezo ya video pia vina athari hasi. Kama alivyosema Mtume Paulo; huwa tunabadilishwa kwa kuona. (soma 2 Wakorintho 3:18).

Tuko vitani na uwanja wa mapambano ni ndani ya mioyo yetu ruhusu Roho Mtakatifu akuongoze soma sana neno la Mungu hapo ndipo salama yetu ilipo...


No comments: