Sunday, April 16, 2017

IJUE VIZURI PASAKA, USITEKWE NA DUNIA

Basi, kabla ya sikukuu ya pasaka ,Yesu,hali akijua kwamba saa yake imefika,atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba,naye amewapenda watu wake katika ulimwengu,aliwapenda upeo,Yesu hali akijua ya kwamba Baba amempa vyote mikononi mwake,na ya kuwa anatoka kwa Mungu naye anakwenda kwa Mungu,aliondoka chakulani,akaweka kando mavazi yake,akatwaa, kitambaa akajifunga kiunoni.Kisha akatia majia katika bakuli,akaanza kuwatawadha miguu na kuifuta kwa kile kitambaa alichojifunga….Basi alipokwisha kuwatawadha miguu, na kuyatwaa mavazi yake, na kuketi tena,akawaambia, Je! Mmeelewa na hayo niliyowatendea? Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu,nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo KUTAWADHANA miguu ninyi kwa ninyi...Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili kama mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo. YOHANA 13:1-151

Bwana Yesu usiku ule aliotolewa alitwaa mkate,Naye akiisha kushukuru akaumega, akasema,Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa UKUMBUSHO wangu. Na vivi hivi baada ya kula akakitwaa kikombe, akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu; fanyeni hivi kila mnywapo, kwa UKUMBUSHO wangu. Maana kila mwulapo mkate huu na kukinywea kikombe hiki, MWAITANGAZA MAUTI YA BWANA HATA AJAPO WAKORINTHO 11:23-26
KUHUSU (EASTER)?

Easter Ni sherehe inayojulikana sana ambayo,inaadhimishwa na makanisa yetu ya siku hizi. Walakini hii pia ilisherehekewa na wapagani muda mrefu kabla ya ufufuo wa Kristo.
Siku zote Pasaka inaangukia Jumapili ya kwanza baada ya mwezi mpevu (full moon) mara tu baada ya jua kuwa kichwani kaskazini ya Ikweta (Equinox ---March 2l).Wapagani wale wa zamani za kale waligundua ya kwamba kila kitu kilionekana kupata uzima mpya mapema katika majira yale ya kuchipua (Spring), mara tu baada ya jua kupita mstari wa ikwinoksi (equinox) kaskazini ya Ikweta. Basi wakachagua siku moja katika majira ya kuchipua [Machi, Aprili, Mei] ili KUMHESHIMU mungu WA KIKE WA UZAZI. Siku ile ikatolewa kwa ISHTA (ISHTAR), mungu wa kike wa uzazi, kwa sababu ya uhai mpya na kukua kwa mimea ya asili.

Neno lilo hilo ISTA (EASTER) limeandikwa kwa herufi nyingine zisizokuwa za lugha yenyewe kutokana na jina la mungu huyo wa kike ISHTA (ISHTAR), ambaye ibada yake iliwekewa ukumbusho wake kwa kutumia sikukuu ya Ista (Easter) [Pasaka]. Mara nyingi Wakristo walei [wa kawaida] wameuliza ya kwamba ule mkate mdogo kama sungura (bunny rabbit) na yai la Ista (Easter egg) vina uhusiano gani na ufufuo wa Kristo. Kusema kweli, havina uhusiano wo wote na [ufufuo] huo. Sungura alichaguliwa kwa sababu alikuwa anazaa sana. Yai pia lilichaguliwa kwa sababu lilikuwa nembo ya kuzaa sana. Hata nembo hizo zenyewe, mkate mdogo kama sungura na mayai, vinatunzwa kama ukumbusho wa asili yake ya kipagani [ya siku hiyo]. Mifano hii imetolewa ili kuonyesha tu jinsi ilivyokuwa rahisi kwa Mwovu kulazimisha mawazo yale ya kipagani juu ya kanisa lile. Swali linakuja mawazoni mwetu, Hivi ni kweli tunaifuata Biblia katika mafundisho yetu yote ya dini? Iwapo MAPOKEO na DESTURI za kipagani zimeweza kuteleza kwa urahisi na kuingia kanisani, ni vipi kuhusu mafundisho mengine ya dini?

Hatuna amri yo yote kuhusu uadhimishaji wa ufufuo au kuzaliwa kwa Kristo. Tunaweza kutafakari juu ya ufufuo Wake na kuzaliwa Kwake kwa wakati wo wote ule na katika siku yo yote ile ya mwaka. Macho yetu na yafumbuke ili tupate kuyatambua mafundisho hayo ya uongo na kuendelea kuwa watiifu kwa ile kweli halisi katika mfumo wake wa asilia.

No comments: