Sunday, November 23, 2014

WAISLAM WASALI PAMOJA NA WAKRISTO MJINI WASHINGTON

WAISLAMU WASALI IBADA YA JUMAPILI KANISANI MJINI WASHNGTON, VITENDO KAMA HIVI VINAKUFUNDISHA NINI ?
MIUNGANO YA MADHEHEBU YA JUMAPILI, UPAPA/RC, DINI ZA UPAGANI NA UISLAMU KUSALI SIKU MOJA VINAKUPA ISHARA GANI?
Miaka129 iliyopita Mama White alioneshwa haya “Waprotestanti … wanafungua mlango kwa upapa kupata tena katika Marekani ya Kiprotestanti mamlaka ambayo uliyoyapoteza katika Ulimwengu wa Zamani…Waprotestanti wa Marekani watakuwa mstari wa mbele katika kunyosha mikono yao juu ya shimo kubwa na kuushika mkono Umizimu; watanyosha mikono juu ya shimo kubwa na kushikana mikono na Mamlaka ya Rumi; na chini ya uongozi wa muungano huo wa utatu [Uprotestanti, Umizimu, na Ukatoliki], nchi hii itafuata katika nyayo za Rumi kwa kukandamiza uhuru wa dhamiri” (GC 
                        MUNGU AKUBARIKI SANA

Saturday, November 22, 2014

THE JESUITS

Shirika la Jesuits lilianzishwa na Ignatius Loyola aliyezaliwa mwaka 1491 na kufariki Julai 31, 1556. Sherehe ya Ignatius.
Loyola hufanyika kila ifikapo Julai 31 ya kila mwaka, siku aliyokufa. Mkuu wa shirika la Jesuit anaitwa “Black Pope” yaani “Papa Mweusi.” 
Hapa haimaanishi kuwa mkuu huyo anatakiwa awe wa rangi nyeusi yaani mwafrika bali neno ‘black’ linamaanisha ‘asiyeonekana,’ na kwa maana hiyo Jesuit Society wanafanya kazi za siri, zisizoonekana, tena za giza ambazo ni kinyume na nuru ya neno la Mungu.
Shirika hili lilianzishwa ikiwa ni matokeo ya kanisa Katoliki kupiga vita uprotestant.
Kujitoa kwa Loyola katika kulitumika kanisa kunaweza kuonekana kwenye kanuni 13 za shirika la Jesuits zinazolihusu kanisa; “Rules for thinking with the church” anaposema “I will believe that the white that I see is black if the hierarchical Church so defines it”.
Kwamba “nitaamini rangi nyeupe ninayoiona kuwa
ni nyeusi kama mfumo wa uongozi wa kanisa utatafsri hivyo.” Na ndivyo ilivyo katika shirika hili ya kwamba mtu anapaswa kuamini na kufanyia kazi kile anachofundishwa na kanisa hata kama dhamira yake inamwambia kuwa hicho si sahihi. Hebu soma
nukuu hizi ili tuone chanzo cha chama cha Jesuits:
“Kuinuka kwa dhama za giza kulitokana na kuruhusu Biblia ipatikane kwa urahisi hata kwa watu wa kawaida na mafundisho ya waprotestant wanamatengenzo. Mafundisho haya yalikuwa na msingi wa kutafsiri unabii kutokana na historia; yaani kuwakilisha siku 1260 za Danieli na Ufunuo kuwa miaka 1260.
Viongozi wa matengenezo kama Luther, Calvin, Huss, Wycliff, Knox, Latimer, Cranmer, Ridley, Hooker, Sir isaack Newton na wengine waliamini hivyo na kufundisha.” Ibid p 7.
“Kwa kutumia mbinu hii ya kutafsiri unabii, kanisa
la Roma lilionekana wazi kuhusika na unabii huu wa pembe ndogo katika Daniel 7, na mnyama wa Ufunuo 13:1, mwanamke wa Ufunuo 17, ikiwa ni pamoja na kichwa cha kanisa kuwakilisha Mtu wa Kuasi wa 2 Wathesalonike 2. Kadri mafundisho haya yalivyozidi, kanisa la Roma lililazimika kujilinda dhidi ya kuongezeka kwa ushahidi wa unabii wa Biblia kulihusisha kanisa hilo.
Hivyo upapa ukaanza kuweka mipango ya kuwapinga waprotestant kwa kuanzisha ‘Jesuit society’ ili kisaidie kufundisha mafundisho ya kanisa na kuharibu mafundisho na vitabu vyote vilivyokuwa kinyume na kanisa na kuanzisha “Holy Office of the Inquisition” maalumu kwa ajili ya kuwatesa hata kuwaua wapinzani wa kanisa.” Ibid. pp 126, 127.
Kati ya mwaka 1524 na mwaka 1537 Loyola alisomea Theology huko Hispania na Ufaransa. Mwaka 1534 alifika Ufaransa wakati wa kipindi cha mapambano dhidi ya uprotestant, mapambano ambayo yalimfanya John Calvin akimbie kutoka Ufaransa.
Mwaka 1539, Loyola akiwa na wenzake walifanikiwa kuanzisha muungano na kuuita ‘Society of Jesus’. Mwaka uliofuata yaani 1540 chama hicho kikapewa baraka na Papa Yohana III na ilipofika mwaka 1548 Papa huyo akatoa kibali kwa Society of Jesus ili kiweze kushughulika na maswala ya kiroho.
Loyola alikufa mnamo Julai 31, 1556 na akabarikiwa na Papa Paul V mwaka Julai 27, 1609, akapewa hadhi ya utakatifu Machi 12, 1622 na Papa Gregory XV na akatangazwa kuwa kiongozi wa maswala la kiroho mwaka 1922 na Papa Pius XI.
Jina kamili la Loyola lilikuwa ni Íñigo akiwa ni mtoto wa mwisho kati ya watoto 13.
Baada ya kifo cha mama yake mwaka 1506 Íñigo alichukua jina la mwisho “de Loyola” kutokana na jina la mji ulioitwa Loyola ambako alizaliwa. 
Akaamua kutumia jina la “Ignatius of Loyola” yaani Ignatius anayetokea mji wa Loyola.
Mwaka 1534 aliwakusanya marafiki zake sita ambao alikutana nao chuo kikuu wakiwa ni wanafunzi wenzake ambao ni Francis Xavier, Alfonso Salmeron, Diego Laynez na Nicholas Bobadilla wote wakiwa ni Wahispania; Peter Faber akiwa ni Mfaransa; na Simao Rodrigues aliyekuwa Mreno. Asubuhi ya tarehe 15 Agust 1534, katika kanisa la Our Lady of the Martyrs huko Montmartre, Loyola akiwa na wenzake sita ambapo mmoja wa marafiki hao alikuwa ni padre, waliapa kutumika maisha yao yote. Ignatius akawa ndiye kiongozi mkuu (Superior General) wa chama cha Yesu – Society of Jesus.
Yeye ndiye aliyetunga katiba ya chama hicho mwaka 1540. Nukuu muhimu tunayoweza kuichukua kutoka kwa Ignatius wa Loyola ni hii: “That we may be altogether of the same mind and in conformity with the Church herself, if she shall have defined anything to be black which appears to our eyes to be white, we ought in like manner to pronounce it to be black.
For we must undoubtingly believe, that the Spirit of our Lord Jesus Christ, and the Spirit of the Orthodox Church His Spouse, by which Spirit we are governed and directed to Salvation, is the same.” [Ignatius Loyola, Spiritual Exercises, Rule 13 Henry Bettenson, ed., Documents of the Christian Church, 2nd ed. (London: Oxford University Press, 1963), p. 260.]
“Kwamba wote tuwe na nia moja na kukubaliana na kanisa, kama limetafsiri kitu chochote kuwa ni cheusi wakati kinaonekana machoni mwetu kuwa ni cheupe, tunapaswa kukitangaza kuwa ni cheusi. Maana bila shaka
tunapaswa kuamini, kwamba roho wa bwana wetu Yesu kristo, na roho wa kanisa la Orthodox ndugu yake, roho ambaye anatuongoza katika wokovu, ni yule yule.” [Ignatius Loyola, Spiritual Exercises, Rule 13 Henry Bettenson, ed., Documents of the Christian Church, 2nd ed. 
(London: Oxford University Press, 1963), p. 260.]
Kwa mujibu wa Ignatius Loyola, kanisa Katoliki na
kanisa la Orthodox ni ndugu mmoja na wote wanaongozwa na roho mmoja.
Lakini pia tunaweza kujiuliza kwa nini Loyola atumie rangi nyeusi hata kama ni nyeupe? Jibu ni kwamba alikuwa anaongelea kiongozi mkuu wa chama hicho cha Jesuits ambaye anaitwa ‘black Pope’ yaani Papa mweusi. 
Lakini pia Loyola aliweka kanuni 13 za kuongoza chama cha Jesuits.

JE AMRI KUMI ZIMEANZIA MLIMA SINAI AU KABLA YA SINAI?

Kuna kuchanganyikiwa kukubwa kuhusu Amri hizo Kumi hivi leo
katika mazingira ya kidini. Wengine bila kufikiri hata kidogo
wanasema kuwa Amri Kumi zilianza na Musa na kukoma Yesu
alipokufa [pale msalabani].
Sheria ya Mungu, ambayo watu wote
huiita Amri Kumi, kimsingi ni ya milele kama Mungu mwenyewe
alivyo. Umilele wake unashuhudiwa na Maandiko hayo
yaliyovuviwa. Amri Kumi KATIKA MFUMO WAKE WA ANDIKO juu ya mawe
huanzia Sinai. Lakini Amri zile [Kumi] zilikuwako muda mrefu
sana kabla ya Mlima Sinai, kama vile Kristo alivyokuwako kabla
ya kuja kama mwanadamu hapa duniani.

Kuthibitisha neno hilo
----- yaani, kujua kama Amri Kumi zilikuwako kabla tu ya
kutokea tukio lile lililouzunguka Mlima Sinai ----- unapaswa
kujiuliza tu swali hili:

"Je! dhambi [uvunjaji wa Amri Kumi]
ilikuwako kabla ya wakati ule?"

Na wewe, bila shaka, utapaswa
tu kuuliza swali hilo ili kupata jibu lako hili

. "Dhambi
[uvunjaji wa Amri Kumi] haihesabiwi isipokuwapo Sheria [Amri
Kumi]." Warumi 5:13. "Maana pasipokuwapo Sheria [Amri Kumi],
hapana kosa [dhambi]." Warumi 4:15. "Kwa kuwa singalijua
kutamani, kama torati [Amri Kumi] isingalisema, Usitamani
[Kutoka 20:17]." Warumi 7:7.

Je, hivi Adamu alitenda dhambi [alivunja Amri Kumi - Yak.
2:10-12]?

Biblia inasema hivi:
"Kwa hiyo kama kwa mtu mmoja
dhambi [uvunjaji wa Amri Kumi] iliingia ulimwenguni, na kwa
dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa
sababu wote wamefanya dhambi [wamevunja Amri Kumi]." Warumi
5:12.Fungu hili linazungumza juu ya Adamu.

Je, Kaini alitenda
dhambi [alivunja Amri Kumi]? Soma Mwanzo 4:7.

"Kama ukitenda
vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko [uvunjaji
wa Amri Kumi upo], inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe,
walakini yapasa uishinde."

Kwa nini Mungu aliuangamiza
ulimwengu wote wa kizazi kile kabla ya Gharika? Kwa sababu ya
dhambi [uvunjaji wa Amri Kumi - Mwa. 6:1-8]. Kwa ukware wao
[uasherati wao mkubwa], na ukatili wao wa kinyama, daima
walikuwa wameivunja Sheria yake [Amri Kumi].

BIBLIA HUTOA MAANA YA NENO DHAMBI
"Dhambi ni
uvunjaji wa Sheria [Amri Kumi]." 1 Yohana 3:4, AJKK. Mahali
pale ilipo dhambi, Sheria ya Mungu [Amri Kumi] ipo.

IBRAHIMU alizijua SHERIA, AMRI NA MAAGIZO YA MUNGU[Mwanzo 26;5] miaka mingi kabla ya kizazi cha israeli.
wanawaisraeli WALIZIJUA AMRI KUMI, SHERIA ZA MUNGU NA AMRI YA SABATO kabla hawajafika mlima sinai walipopewa MBAO MBILI ZA AMRI KUMI[kutoka 16;28-32]

Thursday, November 6, 2014

JE WAJUA KITABU CHA UFUNUO KILILETWA KWA YOHANA SIKU YA SABATO TAKATIFU?

Yohana asema, "Nalikuwa katika Roho, Siku ya Bwana." Yeye hapo hataji siku gani ya juma kuwa ndiyo Siku ya Bwana. Katika suala hili yatupasa kulinganisha Maandiko kwa Maandiko, na kuliacha Neno la Mungu lipate kutufafanulia siku gani kuwa ndiyo Siku ya Bwana. Siku ya Bwana ni siku ile ambayo Kristo ndiye Bwana wake. Yeye anatangaza kwamba ndiye Bwana wa Siku ya Sabato (Marko 2:28). Hivyo Sabato yake Kristo inapaswa kuwa ndiyo Siku ya Bwana.
PIA BWANA MWENYEWE AMESEMA KWA KINYWA CHAKE KATIKA ISAYA 58
13 Kama ukigeuza mguu wako usihalifu
sabato, usifanye anasa yako siku ya utakatifu
wangu; ukiita sabato siku ya furaha, na siku
takatifu ya Bwana yenye heshima;
ukiitukuza, kwa kutokuzifanya njia zako
mwenyewe, wala kuyatafuta yakupendezayo,
wala kusema maneno yako mwenyewe;

ANAIITA SIKU YA UTAKATIFU WAKE.
NA BWANA SIO MUONGO WALA MANENO YAKE YALIYOTOKA HAYABADILIKI~Zaburi 89:34
HIVYO YOHANA ALIPEWA MAONO KATIKA SIKU YA SABATO.

Sunday, September 7, 2014

UJUMBE WA MALAIKA WA KWANZA

Ujumbe wa malaika wa kwanza ni wito wa kumwabudu Mungu Muumbaji. Kwa kweli, lugha yenyewe inatukumbusha sisi juu ya maneno yale yaliyotumika katika amri ya nne. Malaika wa kwanza asema hivi: “Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji” (Ufunuo 14:7). Vilevile, amri ya nne yatuambia sisi kumwabudu Mungu kwa sababu yeye ni Muumbaji wa vitu vyote mbinguni, duniani, na baharini. Yatuambia kwamba siku ya pekee ambayo Mungu ameitenga kwa ajili ya ibada ni siku ya saba ya juma - siku ya Sabato yake takatifu (angalia Kutoka 20:8-11).

UJUMBE WA MALAIKA WA PILI

Ujumbe wa malaika wa pili ni huu: “Umeanguka, umeanguka Babeli, mji ule ulio mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake” (Ufunuo 14:8). Babeli lilikuwa ni taifa katika Agano la Kale ambalo liliishambulia Israeli, yaani, watu wa Mungu, na kuwachukua mateka. Babeli lilikuwa ni taifa lililojaribu kuifutilia mbali ibada ya Mungu wa kweli wa mbinguni na mahali pake kuweka miungu ya kipagani. Na hivyo Babeli ikawa ishara iliyowakilisha majeshi yote yatakayowapinga watu wa Mungu katika siku za mwisho. Kwa hiyo malaika huyu wa pili anasema kwamba Babeli umeanguka kwa sababu umeyafanya mataifa yote ya dunia kunywa mvinyo ya uasherati wake, yaani, hiyo ni njia ya kusema kwamba majeshi yanayopigana na Mungu katika siku hizi za mwisho yatajaribu kumlazimisha kila mmoja kutoa utii wake kwa majeshi hayo kuliko kwa Mungu. Imewakilishwa kama “uasherati,” au uzinzi. Kutokumtii Mungu kunaonyeshwa katika Biblia kama uzinzi wa kiroho, jambo hili lote linatufikisha kwenye hoja ya utii.
 

UJUMBE WA MALAIKA WA TATU

Malaika wa tatu anatangaza hivi: “Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake, yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo” (Ufunuo 14:9,10). Maneno haya machache ni onyo muhimu kabisa ambalo Mungu amepata kulitoa katika Biblia. Anatuonya sisi dhidi ya kuisujudu mamlaka hii ambayo inapingana naye, naye anatuonya sisi tusipokee chapa yake. Mamlaka hii ni nani au ni kitu gani na alama yake ni alama gani?
Je umewahi kumuomba MUNGU akufunulie ili uweze kuepukana na mapigo 7?
Tafakari.
 

Saturday, August 16, 2014

MBARIKIWE SANA

Nawatakieni maisha mema jamazangu na rafiki zangu wote mnaotembelea Blog hii. Bwana awajalie kila lililo heri.

Monday, June 16, 2014

HIVI MWISHO WA DUNIA UTAKUWAJE?



DANIEL NA SIKU ZETU

                (SOMA DANIELI 12 YOTE)

Yapo mawazo mengi wanayosema watu kuhusu mwisho wa dunia. Wengine wanasema watakatifu watanyakuliwa kwenda mbinguni na waovu wote wataangamizwa; dunia itabaki tupu. Wengine wanasema kanisa peke yake ndilo litanyakuliwa; watu waliobaki wataendelea kuishi duniani, na injili itahubiriwa kwa Wayahudi; ndipo Mpinga Kristo atakuja na kufanya mambo yake. Wengine wanasema mbinguni watakwenda tu wale 144,000, watu wengine wote waliobaki makao yao ni hapa duniani; na ya Kwamba dunia hii haiwezi kuharibiwa. Kwa hiyo wanaangalia majengo mazuri na kusema moyoni "Nitarithi jumba hili". Je! Biblia inatupa picha gani juu ya mwisho wa dunia? Na tunaposema tunaishi siku za mwisho tuna maana gani? Zilianza lini kuhesabiwa? Hebu Danieli atuambie katika Sura hii ya 12.
Mwanzo wa siku za mwisho (Dan. 12:5-7): Tunaona kipindi kile kile cha Danieli 7:25 kinatajwa hapa tena na "mtu yule aliyevikwa nguo za kitani" [Kristo] anayeonekana pia katika Ufu. 10:1-7. Soma pia Mt. 17:1,2; Mk. 9:2,3. Anasema hivi, "Itakuwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati; tena watakapokuwa wamekwisha kuvunja nguvu za hao watu watakatifu, ndipo mwisho wa mambo hayo yote yatakapotimizwa" (fungu la 7). Maneno hayo aliyatoa akijibu swali la mmoja aliyemwuliza, "Je! itakuwa muda wa miaka
mingapi hata mwisho wa mambo haya ya ajabu? (fungu la 6). "Mambo ya ajabu" ni mauaji yaliyofanywa na Upapa katika Zama zile za Giza ulipoua zaidi ya watakatifu milioni 50, ambayo yalimshangaza pia hata Yohana (Ufu. 17:6). Kanisa kuua kanisa ni ajabu kuu!
Litakwenda mbingu ya nani? Nyakati 3 1/2 ni miaka 3 1/2 au miezi 42 au siku 1260 za unabii ambazo ni miaka 1260 ya Ufalme wa Papa wa Awamu ya Kwanza (538-1798). Kipindi hicho kimetajwa tena na tena katika unabii (Dan. 7:25; Ufu. 12:6,14; 13:5; 11:2,3; Mt. 24:21,22). Katika Dan. 11:33,34 anasema, "... wataanguka kwa upanga, na kwa moto, na kwa kufungwa, na kwa kutekwa nyara, siku nyingi [538-1798]. Upapa ulitumia upanga, moto, kifungo, kuteka nyara kama unabii unavyosema katika kuwaua watakatifu. Mateso yalikuwa mabaya mno kuliko ya watu wasiomjua Mungu. Ufalme wa Papa ulioitawala dunia (Ulaya Magharibi) ulivunjwa na Wafaransa mapema mwaka 1798. Kuanzia hapo fungu la Dan. 12:4 likaanza kutimia. Maarifa ya kidini, kisayansi na kiteknolojia yaliongezeka kasi kwa namna ya ajabu. Zama za Giza hazikuwa na maendeleo yo yote. Wana-sayansi na Wanadini waliofuata Biblia walikuwa wanauawa. Mwaka 1798 ndio mwanzo wa "Siku za Mwisho". Mwisho wake utakuwa katika Awamu ya Pili inayokuja ya Ufalme wa Papa ----- "tena watakapokuwa wamekwisha kuvunja nguvu za hao watu watakatifu" (Dan. 12:7). Historia inajirudia yenyewe. Mateso na mauaji ya watakatifu yatakuja tena atakapotawala Papa (Ufu. 6:9-11) ----- "wakaambiwa wastarehe bado muda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao." Wengi hawaamini maneno hayo; lakini wanapaswa kungoja mpaka yatakapotimia ndipo watakapoamini (Yoh. 14:29).
Kusimamishwa kwa Chukizo la Uharibifu au Mwanzo wa Ufalme wa Papa (Upapa):
Rumi ya Kipagani iliangushwa na makabila ya kipagani ya Ulaya Kaskazini mwaka 476 B.K. Tangu siku za Mfalme Konstantino, mwaka 330, Askofu wa Roma au Papa aliachiwa kutawala mji wa Roma. Kwa hiyo Dola ya Magharibi ya Rumi ilipoanguka, Papa aliendelea kutawala mji ule. Alishika hatamu za utawala juu ya Ulaya Magharibi kuanzia mwaka 538 baada ya kuzing'oa falme tatu - Waheruli (493), Wavandali (534), na Waostrogothi (mapema 538).
Mataifa yale mengine ya Ulaya yalipokea Ukatoliki kwa upanga wa Mfalme Clovis wa Ufaransa. Kwa hiyo, yakajikuta yako tena chini ya Papa, (538-1798). Clovis alifanikiwa kuyafanya Wakatoliki mwaka 508 (Dan. 12:11,12). Kuanzia mwaka huo wa 508 zinahesabiwa siku au miaka 1290 na 1335. Chukizo la Uharibifu lilisimamishwa [lilitawala] kuanzia 538 - 1798 (yaani, miaka 508 + 1290 = 1798 barabara). Mwaka ule wa 1798 ukawa ndio mwanzo wa siku za mwisho. Hukumu ikawekwa mbinguni kumpimia adhabu yake mwaka 1844, yaani, mwisho wa miaka ile 2300 ya Dan. 8:14 (yaani, miaka 508 + 1335 = 1843-1844). Mwaka ukianza tarehe 2 Januari unamalizika katika mwaka unaofuata.
Kuna heri gani kwa watu watakaoufikia mwaka 1844, mwaka ambao Hukumu ilianza mbinguni? Wale walio na hekima "watajitakasa na kujifanya weupe" (Dan. 12:3,9,10); tena watasimama kama Danieli katika "kura" yao, yaani, majina yao yatabaki katika Kitabu cha Uzima mbinguni pamoja na watakatifu wote waliotangulia (Dan. 12:13). Isitoshe heri nyingine ni ile ya kufufuliwa katika ufufuo wa pekee (Dan. 12:2; Ufu. 14:13) kwa wale wote walioshiriki kuihubiri Injili ya Milele kwa uaminifu (Ufu. 14:6-12). Injili hiyo inayoitwa "Ujumbe wa Malaika Watatu" ilianza kuhubiriwa 1840-1844 na bado inahubiriwa. Ufufuo wa watakatifu wote utafuata mara tu baada ya ufufuo huo wa mseto utakaokuwa na wale waliomchoma pamoja na wale waliowatesa sana watu wa Mungu (Ufu. 1:7; 1 The. 4:16,17[18]).

MWISHO WA DUNIA UTAKUWAJE?
 Tumeona jinsi Ufalme wa Papa ulivyotawala katika Awamu ya Kwanza (538-1798) na ya kwamba unakwenda kutawala dunia tena. Hiyo itakuwa ni awamu yake ya pili na ya mwisho. Maangamizi ndiyo yatakayokuwa mwisho wa Ufalme huo. Mfuatano wa matukio ni huu ----- Papa atawala awamu ya pili, mateso na mauaji ya watakatifu yaanza tena kwa kipindi kifupi sana, Kristo, Kuhani wetu Mkuu, anamaliza kazi yake ya Maombezi katika Hekalu la Mbinguni na kuufunga mlango wa kutubu au wa rehema kwa tamko la Ufu. 22:11. Watu wa Mungu wametiwa muhuri wa Mungu katika vipaji vya nyuso zao; na watu wa Mnyama wamepata alama ya mnyama vipajini mwao na katika mikono yao. Wakati wa taabu unaanza (Dan. 12:1) Mikaeli (Kristo) anapotawazwa (anaposimama) katika Jiji la Yerusalemu juu; pepo za vita zilizozuiwa zaachiliwa na vita inatapakaa kila mahali ikileta maafa mengi(Ufu. 7:1-4), vimbunga na maafa mengine yanatokea, ndipo silaha ya Mungu ya kutisha sana kwa wale walioikanyaga Sabato yake itakapotumika (Mapigo 7 ya Ufunuo 16). Wale wote watakaomfuata Papa majina yao yataondolewa katika kitabu cha uzima (Kut. 32:32,33; Ufu. 13:8). Mtihani wa siku za mwisho ni Amri ya Nne [Sabato](Ufu. 3:10; 14:9,10).
Mchezo wa kuiweka Jumapili badala ya Sabato [Jumamosi] utakuwa na athari mbaya mno kwa dunia nzima (Isa. 24:1-6,19,20; Ufu. 19:11-21). Ole kwa wafalme wa dunia hii! Ole kwa kila mtu asiyesimama upande wa Yesu Kristo katika Pambano hili Kuu! Karibu sana litafikia mwisho wake. Watoto wa Mungu wamechoka na dunia hii wanataka kwenda kupumzika mbinguni kwa miaka 1000, na Yesu anasema. " Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo" (Ufu. 22:11). Je! u tayari kumlaki Bwana? Je! utasimama imara hata kama mbingu zikianguka, na kuiinua juu Bendera ya Imanueli [Kristo] iliyoandikwa "Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao Amri [Kumi] za Mungu, na Imani ya Yesu" (Ufu. 14:12). Hivi karibuni dunia hii itabaki tupu, ndugu yangu. Kuanzia leo chagua kuingia Paradiso pamoja na Kristo (Luka 23:42,43; 2 Kor. 6:2). Huenda usisikie mwito mwingine kama huu. Amua leo!


AMRI ZA MUNGU NA SHERIA ZA MUSA



MARA NYINGI WATU WANASHINDWA KUTOFAUTISAHA KATI YA AMRI ZA MUNGU NA SHERIA ZA MUSA ZIFUATAZO NI TOFAUTI
1. ZA MUNGU Ziliandikwa na Mungu mwenyewe Kwa kidole chake [Torati 31:18]
ZA MUSA Ziliandikwa na Musa mwenyewe kwa k wa kidole
2.Ziliandikwa kwenye mbao mbili za mawe yaliyochongwa, Torati 10:1-4
ZA MUSA Ziliandikwa kwenye chuo(kitabu cha dini), Torati 31:24
3., ZA MUNGU Ziliwekwa ndani ya Sanduku la Agano Torati 10:1-4
ZA MUSA Baada ya kuandikwa, ziliwekwa nje pembeni ya Sanduku la Agano,
Torati 31:24-27
4 . Waliozivunja, walionekana kutenda dhambi 1Yoh. 3:4, na iliwapasa kufa. Torati 17:2-5
ZA MUSA Waliozivunja, hawakuonekana na dhambi wala haikuwapasa kufa kwani zilikuwa ni kivuli cha Kristo Wakolosai 2:14-17
5. Yesu alikuja kuzitimiliza wala si ku zitangua. Watu wote wanapaswa kuzifundisha…Mathayo 5:17-19 -
ZA MUSA Yesu aliziondoa pale msalabani maana zilikuwa ni sheria za maa gizo
tu yaliyosimama kama kivuli cha mema yajayo. Kolosai 2:15
6. Sheria(torati) ya Bwana ni takatifu njema na ya haki, nayo yadumu mi lele na milele, Warumi 7:12-
ZA MUSA Zilikuwa ni kivuli cha kazi ya Yesu aliyoifanya msalabani, nazo zilikomea hapo. Ebran. 10:1-12
7. Sheria za Bwana ni kamilifu, za adili, kweli na za milele Zaburi 111:7-8
ZA MUSA Ziliishia pale Kristo alipokufa Msalabani. Waebran. 9:10-12, Luka 22:37
A. Mfano wa sheria ya Musa
1. Kuchinja kondoo kama mbadala wa mdhambi. Kutoka 29…, Walawi, Torati, Nyakati nk
2. Kifo yeyote aliyevunja mojawapo au Amri zote 10 za Mungu
Kutoka 31:14… Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake.
B. Sheria za Mungu, Kutoka 20 :1-17
Hivyo basi Yesu alipokufa Msalabani sheria za kuchinja kondoo tena ziliisha maana mwanakondoo wa Mungu (Yesu) aichukuaye dhambi ya ulimwengu alikuwa ameshachinjwa tayari.
Yohana 1:29 Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!

HIVI KWELI KIFO CHA YESU MSALABANI KILIIONDOA SABATO YA AMRI YA NNE?

EBU TUANGALIE MITUME WA YESU KAMA WALIENDELEA KUISHIKA SABATO BAADA YA YESU KUFA NA KUPAA MBINGUNI AU HAWAKUISHIKA?
Matendo ya Mitume 13:14 Lakini wao wakatoka Perge, wakapita kati ya nchi, wakafika Antiokia, mji wa Pisidia, wakaingia katika sinagogi siku ya sabato, wakaketi.
Matendo ya Mitume 13:27 Kwa maana wakaao Yerusalemu, na wakuu wao, kwa kuwa hawakumjua yeye, wala maneno ya manabii yanayosomwa kila sabato, wameyatimiza kwa kumhukumu.
Matendo ya Mitume 13:42 Na walipokuwa wakitoka, wakawasihi waambiwe maneno haya sabato ya pili.
Matendo ya Mitume 13:44 Hata sabato ya pili, watu wengi, karibu mji wote, wakakusanyika walisikie neno la Mungu.
Matendo ya Mitume 15:21 Kwa maana tangu zamani za kale Musa anao watu wahubirio mambo yake; katika kila mji husomwa kila sabato katika masinagogi.
Matendo ya Mitume 16:13 Hata siku ya sabato tukatoka nje ya lango, tukaenda kando ya mto, ambapo tukadhani ya kuwa pana mahali pa kusali; tukaketi, tukasema na wanawake waliokutana pale.
Matendo ya Mitume 17:2 Na Paulo, kama ilivyokuwa desturi yake, akaingia mle walimo, akahojiana nao kwa maneno ya maandiko sabato tatu,
Matendo ya Mitume 18:4 Akatoa hoja zake katika sinagogi kila sabato, akajaribu kuwavuta Wayahudi na Wayunani.
• Paulo bado anasisitiza
Waebrania 4:9 Basi, imesalia raha ya sabato kwa watu wa Mungu.
• Isaya anasema hadi mbinguni, tutaitunza Sabato ya Bwana
Isaya 66 :22 Kama vile mbingu mpya na nchi mpya, nitakazofanya, zitakavyokaa mbele zangu, asema Bwana, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa. 23 Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana.
Kwani siku ya Sabato in Ipi ??
Mathayo 28:1 Hata sabato ilipokwisha, ikipambazuka siku ya kwanza ya juma, Mariamu Magdalene, na Mariamu yule wa pili, walikwenda kulitazama kaburi.
Marko 16:2 Hata alfajiri mapema, siku ya kwanza ya juma, wakaenda kaburini, jua lilipoanza kuchomoza;
Marko 16:9 Naye alipofufuka alfajiri siku ya kwanza ya juma, alimtokea kwanza Mariamu Magdalene, ambaye kwamba alimtoa pepo saba.
Luka 24:1 Hata siku ya kwanza ya juma, ilipoanza kupambazuka, walikwenda kaburini, wakiyaleta manukato waliyoweka tayari.
Yohana 20:1 Hata siku ya kwanza ya juma Mariamu Magdalene alikwenda kaburini alfajiri, kungali giza bado; akaliona lile jiwe limeondolewa kaburini.
Yohana 20:19 Ikawa jioni, siku ile ya kwanza ya juma, pale walipokuwapo wanafunzi, milango imefungwa kwa hofu ya Wayahudi; akaja Yesu, akasimama katikati, akawaambia, Amani iwe kwenu.
Yesu alifufuka siku ya jumapili ambayo Biblia inaiita kuwa ni siku ya kwanza ya juma. Kama Yesu alifufufuka siku ya kwanza ya juma(jumapili), Sabato itakuwa lini??
Jibu: Jumamosi
Karibu tujiunge kwenye kundi dogooo. Kundi dogo liendalo Uzimani.
Matt 7:13 Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo.
14 Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.
 
MWENYE MASIKIO NA ASIKIE.

Tuesday, May 27, 2014

UNABII ULIOTIMIA NA UNAOENDELEA KUTIMIA KATIKA SIKU ZETU

 
I. UFALME WA BABELI (606-538 au 605-539 K.K.).
Umewakilishwa na Kichwa cha dhahabu (Dan. 2:37-38). Historia inaunga mkono.
II. UFALME WA WAMEDI NA WAAJEMI (538-331 au 539-331 K.K.).
Uliuangusha Ufalme wa Babeli (Dan. 5:25-31). Unawakilishwa na Kifua na Mikono
ya Fedha (Dan. 2:32a,39a). Historia inaunga mkono. Miaka ni ya kukadiria tu.
III. UFALME WA WAYUNANI (331-168 K.K.)
Ufalme wa Wamedi na Waajemi ulitabiriwa kuwa utaangushwa na Wayunani (Dan.
8:4-7,20-21; 11:1-3). Ufalme wa Wayunani (Wagiriki) unawakilishwa na Tumbo na
Viuno vya Shaba (Dan. 2:32b,39b). Historia inaunga mkono.
IV. UFALME WA WARUMI (168 K.K. - 476 B.K.).
Ufalme wa Warumi unawakilishwa na Miguu ya Chuma. Biblia inaielezea vizuri
Dola ya Warumi kuwa ilikuwa inazivunja-vunja falme zile nyingine kama chuma. Danieli
hakujulishwa jina la Dola hii. Lakini historia inathibitisha kuwa Warumi waliwashinda
Wayunani mwaka ule wa 168 K.K. Wakati Kristo anazaliwa Dola hiyo ilikuwa bado
inatawala dunia pamoja na Palestina chini ya Kaisari Augusto (Luka 2:1-7; Yohana 11:48).

SHERIA YENYE REHEMA NA NEEMA

Ingawa sheria ya Mungu ni sheria ya rehema na neema ..hatimaye Mungu anaitumia kama kiwango au sababu ya kuhukumu...  Matokeo ya sheria yanakuwa hasi au chanya kutokana na mshika sheria mwenyewe anavyoiendea... sheria kazi yake ni kuonyesha dhambi sasa kama umeishika alafu hujaiendea neema ya Yesu ikusafi na kukusamehe,basi sheria hiyo itadai Ufe.. pia kristo anasema kuwa hukumu haitoki kwake- bali kwamba mwenye dhambi asiyetubu anajihukumu mwenyew pale anapokataa kusikiliza sheria(amri za mungu)...
hivi karibuni kabla au baada ya mlango wa rehema kufungwa tangazo litasikika "mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu,mwenye uchafu na azidi kuwa uchafu na azidi kuwa mchafu, mwenye haki na azidi kutenda haki, na mtakatifu na kutakaswa,(ufunuo 22:11)......
sheria kama kiwango cha hukumu pia ni kipimo cha upendo kwa Mungu ndani yako.. so shika kikamilifu cheria ya Mungu kwa upendo uliokisiri ndani yako juu ya YESU na neema yake itakuhesabia haki....

Tuesday, February 25, 2014

AMRI YA JUMAPILI KWA ULIMWENGU MZIMA

 Biblia inasemaje juu ya kuinuka tena ulimwenguni kote kwa uongozi ule wa Roma ya Kikatoliki kabla ya mwisho wa wakati? Ufunuo 13:3,8.
  1. Ni Taifa gani lililopata upendeleo litakaloongoza katika kulazimisha utunzaji wa Jumapili?

a. "Kundi lilo hilo lilitoa madai yake ya kwamba kuenea haraka kwa ufisadi kwa sehemu kubwa kulichangiwa na kuinajisi ile wanayoiita 'Sabato ya Kikristo,' na ya kwamba kule kulazimisha utunzaji wa Jumapili kungeyaboresha sana maadili ya jamii. Madai hayo yanasisitizwa hasa katika Amerika, ambako fundisho la Sabato ya Kweli limehubiriwa karibu kwa mapana yake yote." GC 587.

b. "Mataifa ya kigeni yatafuata mfano wa Marekani. Japokuwa Taifa hili linaongoza, hata hivyo hatari iyo hiyo itawajia watu wetu katika sehemu zote za ulimwengu." 6T 395.

2. Ni mataifa mangapi yatakayofuata mfano huo wa Marekani?

a. "Amerika, nchi yenye uhuru wa dini, itakapoungana na upapa katika kuzitenda jeuri dhamiri za watu na kuwalazimisha watu kuiheshimu sabato hiyo ya uongo [Jumapili], hapo ndipo watu wa kila nchi ulimwenguni watakapoongozwa kufuata mfano wake." 6T 18 (Angalia GCB 1-28- 1893).

b. " '[A]liwanywesha Mataifa yote mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake [mafundisho yake potofu]' Ufunuo 14:6-8. Hii inakuwaje? Kwa kuwalazimisha watu kuikubali sabato bandia [Jumapili]." 8T 94.
c. "Suala hili la Sabato ndilo litakuwa hoja kuu katika Pambano Kuu la mwisho ambalo kwalo ulimwengu wote utakuwa na sehemu yake ya kufanya." 6T 352.

4. Ni dini gani hasa ya ulimwengu mzima inayohusika na kulazimisha utunzaji huu wa Jumapili?

a. "Kwa vile Sabato imekuwa jambo la pekee la mabishano katika Mataifa ya jamii za Kikristo, na wenye mamlaka ya dini [ya Muungano] na serikali wameungana katika kulazimisha utunzaji wa Jumapili, basi, wale walio wachache sana watakaoendelea kukataa kukubaliana na madai hayo yanayopendwa na wengi watakuwa watu wa kuchukiwa mno ulimwenguni kote." GC 615.

b. "Jamii yote ya Kikristo itagawanyika katika makundi makuu mawili, wale wanaozishika amri [kumi] za Mungu na imani ya Yesu, na wale wanaomsujudu mnyama na sanamu yake, na kuipokea chapa yake." GC 450; 9T 16; 2SM 55.

5. Ni jambo gani litakalowapata Waadventista Wasabato ambao hawawezi kukubaliana na Amri hiyo ya Jumapili?

a. "Amri ile itakayoitia nguvu ibada ya siku hii [ya Jumapili] itatangazwa ulimwenguni kote.... Maonjo na mateso yatawajia wale wote ambao, kwa kulitii Neno la Mungu, watakataa kuisujudu sabato hiyo ya uongo [Jumapili]." 7BC 976.
b. "Ulimwengu wote utachochewa kuwa na uadui dhidi ya Waadventista Wasabato, kwa sababu hawatakubali kumsujudu papa kwa njia ya kuiheshimu Jumapili, siku iliyowekwa na mamlaka hiyo ya Mpinga Kristo. Ni kusudi lake Shetani kusababisha wafutiliwe mbali duniani, ili ukuu wake humu duniani usipate kupingwa." TM 37; RH 8-22-1893.

c. "Mamlaka za ulimwengu huu, zikiwa zimeungana pamoja kuzipiga vita Amri [Kumi] za Mungu, zitatangaza amri kwamba 'wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini na walio huru kwa watumwa' (Ufunuo 13:16), watafuata kwa lazima desturi za kanisa kwa kuitunza sabato hiyo ya uongo [Jumapili]. Wale wote watakaokataa kutii watakabiliwa na adhabu kutokana na sheria za serikali zao, na hatimaye itatangazwa kwamba wanastahili kifo." GC 604.

6. Ni athari gani zitakazoletwa na uamsho huo wa bandia juu ya karibu wote wanaojiita Wakristo kwa jina tu?

"Wakatangaza ya kwamba wao walikuwa na ile kweli; ya kwamba miujiza ilitendeka kati yao; ya kwamba uwezo mkuu na ishara na maajabu yalitendeka miongoni mwao; na ya kwamba hiyo ilikuwa ndiyo ile Milenia [miaka elfu moja] waliyokuwa wanaingojea kwa muda mrefu sana. Ulimwengu wote uliongolewa na kuafikiana na Amri ile ya Jumapili." Letter 6, 1884. 7.

Ni alama gani mbili zinazopingana zitapokewa na makundi hayo mawili ya watu katika ulimwengu huu hapo Jumapili itakapotiwa nguvu kwa kuitungia sheria?

a. "Wakati utunzaji wa sabato hiyo ya uongo [Jumapili] kwa kuitii amri ya serikali, kinyume na amri ile ya nne, utakuwa ni kiapo cha utii kwa mamlaka ile inayopingana na Mungu, utunzaji wa Sabato ya Kweli, kwa kuitii Sheria ya Mungu [Amri Kumi], ni ushahidi wa utii kwa Muumbaji. Wakati kundi moja, kwa uikubali alama ya utii kwa mamlaka za duniani, linapokea Alama (chapa) ya Mnyama, lile jingine, kwa kuichagua ishara ya utii kwa Mamlaka ile ya Mbinguni, litapokea Muhuri wa Mungu." GC 605.

c. "Matokeo ni ya kuogofya ambayo kwayo ulimwengu huu utakabiliwa nayo. Mamlaka za ulimwengu huu, zikiwa zimeungana pamoja kuzipiga vita Amri [Kumi] za Mungu, zitatangaza amri kwamba 'wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa,' (Ufunuo 13:16), watafuata kwa lazima desturi za kanisa kwa kuitunza sabato hiyo ya uongo [Jumapili]. Wale wote watakaokataa kutii watakabiliwa na adhabu kutokana na sheria za serikali zao, na hatimaye itatangazwa kwamba wanastahili kifo.

Kwa upande mwingine, Sheria ya Mungu [Amri Kumi] inayoamuru Siku ya Mapumziko iliyowekwa na Muumbaji inataka watu wote waitii na kutishia ghadhabu dhidi ya wote wanaozivunja amri zake [kumi]. "Jambo hilo likiwa limewekwa wazi hivyo mbele yake [kila mtu], hapo ndipo ye yote atakayeikanyaga sheria ya Mungu chini ya miguu yake ili kuitii amri ile iliyotungwa na binadamu atapokea Alama ya Mnyama...." GC 604.
http://api.ning.com/files/RuWbev-xAt8JOWYH*2QzHqULqrczY2cTkdyS0lJKMUhqFz9Rg-cE2jJFBpnzpe*o6DssmOLFnoQgOcJGwwDFZncTvV721K8a/Supermarket2.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhQzRe_8yyusGYhl4BbiDAvXDY03cKFoX0RhNoj8OTYXE03ri0ELrai_zW-ZoC6V9RYBRqprQqDkuTQ7nuYvl2Lvk6jO_a5NvpZ8bsjVXm4bXvbIkSKoVlxiSahbk-OKJHPw1j27_PJE8Y/s1600/otmmktcra.jpg

WATU WANNE WAPO KATIKA HALI MBAYA NA WENGINE 7 WAMEJERUHIWA BAADA YA LORI SCANIA KUGONGANA USO KWA USO NA BASI DOGO LA ABIRIA


Picha juu ni baadhi ya abiria wakiwa kwenye hali  baada ya lori scania namba T653 BFD  (scania 380) kugongana uso kwa uso na baso dogo la abiria Toyota Hiace T613 CPG iliyokuwa inatoka mbagala kwenda mkuranga jana

WATU wanne wapo katika hali mbaya na wengine saba wamejeruhiwa baada ya lori scania namba T653 BFD  (scania 380) kugongana uso kwa uso na baso dogo la abiria Toyota Hiace T613 CPG iliyokuwa inatoka mbagala kwenda mkuranga.

Kwa mujibu wa shuhuda ya ajali hiyo iliyotokea Mwandege, Dominic Kubhota, ameiambia blogu hii usiku huu kwamba chanzo cha ajali hiyo ni ovateki isiyotumia akili ya lori hilo . Majeruhi hao wamefikishwa katika hospitali ya Mkuranga, lakini muda mfupi baadaye walianza kukimbizwa kuleta dare s salaam kw amatibabu zaidi.

Abiria wawili waloikuwa mbele  ya daladala walikatika miguu.

Majeruhi wengine walioweza kuzungumza ni: Mustafa mfungapoa wa mkuranga Abdul Ally wa mwandege Ramadhani rajab Theofrida Mwinuka (alikuwa mbele amevunjika miguu)Jamal  mbaraka (aliyekwanguka ngozi ya kichwa) Abraham Mohamed

Swalehe salum

KITUNGUU SWAHUMU KINGA YA KUDUMU YA MARADHI

http://api.ning.com/files/DQZ40zyDI503SCBB5Kds6P0bF98gDD0SAqjStbxo8M1xcM6cbTGJ1fow-E2nKzgU6e30R91hE1HyF2RaX6ZN4jStXu5FQPZ7/jinsiulivyo.jpg
 Tafiti nyingi zimeshafanyika duniani kuhusu faida za kitunguu swaumu ambazo zimethibitisha kuwa mtu akitafuna na kumeza hata punje moja tu ya kitunguu swaumu kila siku asubuhi, basi mtu huyo atakuwa amejitengenezea kinga ya mwili ya kudumu itakayomlinda na maradhi mbalimbali, yakiwemo maradhi sugu yaliyoshindikana hospitalini.   
 Kitunguu swaumu kimegundulika kuwa rafiki wa damu mwilini, kwani kinapoliwa, huenda moja kwa moja kutoa sumu zote kwenye damu na kuipa damu vitamin na huongeza uwezo wa damu kusafiri vyema katika mishipa hivyo kumfanya mtu ajisikie mwenye afya njema kila siku.
Aidha, kitunguu swaumu kimegundulika kuwa na uwezo mkubwa wa kuzuia magonjwa ya moyo kwa kupenya katika mishipa ya damu na kuvunja-vunja Cholestrerol zote ili kupisha njia ya damu iwe safi na wazi kutokana na ‘antibiotic’ iitwayo ‘Allicin’ iliyomo kwa wingi katika chakula hiki.
China na India zinaaminika kuwa ni nchi ambazo wakazi wake ni watumiaji wakubwa wa kitunguu swaumu katika milo yao ya kila siku. Tabia hii imewasaidia sana kujikinga na maradhi mengi yanayoweza kuzuilika. Bila shaka hata Watanzania tukiamua kutumia kwa wingi kitunguu hiki katika milo yetu ya kila siku, tutajikinga na maradhi mengi na hata  uwezo wa kufikiri (Extra clear thinking capacity) utaongezeka, kwani kitunguu huongeza akili pia.
Ili nawe kujiepusha na maradhi na pengine kuyatibu yale ambayo umeshayapata kwa kutumia njia asilia, tafadhali anza sasa utaratibu wa kutafuna na kumeza angalau punje moja tu ya kitunguu swaumu kila siku asubuhi kabla ya kula chochote, fanya kuwa utaratibu wako wa kila siku. Ili kuondoa harufu mdomoni, tafuna kwanza kisha kapige mswaki na kuendelea na mlo wako wa kawaida.
Kuna jambo ambalo linaweza kuwakatisha tamaa ya kupona baadhi ya watu watakaotumia kitunguu swaumu kama dawa. Tafiti zimeonyesha kuwa upo uwezekano wa baadhi ya vitunguu swaumu kutokuwa na virutubisho vinavyotakiwa. Hii inatokea, na inahusisha sana aina ya udongo uliyopo mahali kilipooteshwa kitunguu hicho na kwa akili ya kawaida, utakubali kuwa kile kilichoota kwenye udongo wa mfinyanzi hakitakuwa na ladha sawa ya kile kilichoota kwenye mchanga.
Kwa kutambua hilo, watafiti waliamua kutengeneza vidonge vya vitunguu swaumu ambavyo tayari vimepitishwa katika maabara kuhakiki ubora kabla ya kusindikwa na kutengezwa vidonge vyenye uhakika wa tiba. Vidonge hivyo vipo madukani na ukivihitaji utapewa maelekezo ya kuvipata kwa kuwasiliana na mwandishi wa makala haya.
                   Global Publishers

Monday, February 24, 2014

KANISA LA MWISHO LA KRISTO

Ukweli uo huo umeelezwa wazi katika Agano Jipya pamoja nalile la Kale. 
Katika maono yake matakatifu Mtume Yohana, akiwa kisiwani Patmo, aliruhusiwa kuangalia mpaka mwisho wa karne za Kipindi cha Kikristo. Analiona Kanisa la Mwisho la Kikristo, yaani, Kanisa ambalo litamlaki Bwana atakapokuja mara ya pili.
Naye Yohana analieleza hivi kanisa hilo.
"Joka akamkasirikia yule mwanamke [kanisa],
akaenda afanye vita juu ya wazao wake WALIOSALIA, WAZISHIKAO AMRI ZA MUNGU, na KUWA NA USHUHUDA WA YESU" (Ufunuo l2:17). "JOKA" hapa anamwakilisha Shetani. "MWANAMKE" analiwakilisha Kanisa la Kristo.
"WAZAO WAKE WALIOSALIA" huhusu Kanisa mpaka mwisho kabisa wa dunia, Kanisa litakalokuwako wakati wa kuja mara ya pili kwa
Kristo.
 Hapa Kanisa linaonyeshwa kuwa lina tabia za pekee mbili: 
Kwanza, LINASHIKA AMRI ZA MUNGU; pili, LINA KARAMA YA UNABII [ROHO YA UNABII]  ambayo ndiyo USHUHUDA WA YESU
(Ufunuo 19:10).
 
Kanisa hili la mwisho litakuwa ni KANISA LINALOSHIKA SABATO, kwa maana kwa kweli isingeweza kusemwa kamwe juu ya kanisa lo lote ambalo halishiki Sabato kuwa lilizishika amri za Mungu. 
Kanisa linalozishika amri za Mungu tisa tu ni kanisa
linalovunja amri za Mungu.
Kanisa hilo la mwisho ni Kanisa lishikalo amri zote 10, ikiwemo na Sabato.
Tena Yohana, akiangalia mbele kupita karne zote, anauona ujumbe ule wa mwisho wa injili ukihubiriwa kwa '"Kila taifa na kila kabila na lugha na jamaa."
Anaueleza ujumbe huo katika sura ile ya kumi na nne ya Ufunuo. 
Ujumbe huo ni wa aina tatu, na hapo utakapotimizwa, ndipo Kristo ATAKAPOONEKANA akija na mawingu ya mbinguni kuvuna mavuno ya nchi (Ufunuo 14:14,15). 
Kwa hiyo huo lazima uwe ni ujumbe wa mwisho kutolewa kwa wanadamu.
Yohana pia anawaona watu wale watakaoutoa ujumbe huo, naye anaeleza hivi habari zao: "Hapa ndipo penye subira ya WATAKATIFU, hao WAZISHIKAO AMRI ZA MUNGU na
IMANI YA YESU" (Ufunuo 14:l2).
Kwa hiyo katika Agano la Kale na Jipya Mungu anaonyesha wazi kwa mwanafunzi wa Biblia ya kwamba KILA MKRISTO ANAWAJIBIKA KUSHIKA KILA SEHEMU YA SHERIA YAKE TAKATIFU.
Katika siku hizi za mwisho Sheria hii itakuwa KIPIMO CHA IMANI ya watu wa Mungu. 
Na wale ambao kwa uaminifu WATASHINDA katika jaribio [Kipimo] hilo wanapewa ahadi hii: "Heri wale wazishikao amri Zake, wawe na haki kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake" (Ufunuo 22:14, Tafsiri ya King James Version)

Sunday, February 23, 2014

JE! MBINGUNI WANAABUDU SIKU GANI?

Tumeona kuwa watu wengi wamekuwa wakitumia siku mbalimbali kwajili ya ibada Ijumaa, Jumamosi, Jumapili, Jumatano na nyingine nyingi. Lakini swali ni hili, je tutakapoenda mbinguni ni siku gani tutakayoabudu kati ya hizi? Je, Biblia inasemaje kuhusu hili? Isaya. 66:22,23 “Kama vile MBINGU MPYA NA NCHI MPYA, nitakazofanya, zitakavyokaa mbele zangu asema BWANA, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa. 
Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na SABATO hata SABATO, WANADAMU WOTE WATAKUJA KUABUDU MBELE ZANGU ASEMA BWANA.” 

Mungu anasema katika Neno lake kuwa katika mbingu ambayo ameifanya kwajili ya watakatifu wake WOTE, kwamba watakuwa WANAMWABUDU katika kila siku ya SABATO yaani siku ya Jumamosi.
Ni ukweli kuwa Mungu atakuja kuchukua watakatifu wake “hao wazishikao AMRI za Mungu na imani ya Yesu”.
Ufunuo.14:12 Kamwe hakuna mwenye dhambi hata mmoja atakayeingia katika ufalme wa mbinguni. 

Si ndiyo? Sasa biblia inatoa maana rasmi ya neno dhambi katika 1 Yoh3:4, “Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwakuwa DHAMBI NI UASI.”
Hivyo dhambi ni uasi wa sheria za Mungu, yaani waasi wote wa sheria hawataingia mbinguni.
Pia amri kumi za Mungu zapaswa kushikwa kwa ukamilifu wake zote kama zinavyoelezwa katika Kutoka. 20:3-17. Na kuvunja amri moja tu, ni sawasawa umevunja amri zote kumi. Yakobo2:10,11 inasema “Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote.
Maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue.
Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekua mvunja sheria.” 

Yaani ukishika amri za Mungu tisa tu, ukaacha kuishika sabato ya Jumamosi UMEKUA MVUNJA SHERIA.
Na kwa wale ambao wanashika sabato tu na kuvunja zingine amekuwa mvunja sheria pia bali usalama upo katika kushika amri zote za Mungu ikiwemo sabato.
Kurani nayo inasema katika suratun Nahl(16) kifungu cha 124 kuwa, “Hakika (adhabu ya kuvunja taadhima ya) Jumamosi iliwekwa juu ya wale waliohitilafiana kwa ajili ya hiyo (Jumaamosi), na kwa yakini Mola wako atahukumu baina yao siku ya kiama katika yale waliyokuwa wakihitalifiana .” 

Hivyo hata kurani inatoa onyo kwa wavunja sheria ya Mungu hasa wavunja sabato ya BWANA yaani siku ya Jumamosi. 
Je wavunja sabato ya BWANA wote watapotea hata wanaovunja sabato wakati wanatenda miujiza? Yesu alisema “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. 
Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwajina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo NITAWAAMBIA DHAHIRI, SIKUWAJUA NINYI KAMWE; ONDOKENI KWANGU NINYI MTENDAO MAOVU.” 
Mungu anasema kwamba kuna watu watamwendea wakimsihi waingie katika ufalme wake lakini atawakataa kwa maana hata wakati wanatenda miujiza hiyo hakuwajua maana hawakutii mapenzi ya Mungu.
Lakini tumaini lipo, Yesu alisema “Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akisikia sautiyangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, nay eye pamoja name.” 


Ufunuo.3:20 Pia alisema kwakua “Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na SAUTI YANGU WATAISIKIA; KISHA KUTAKUWA NA KUNDI 1 NA MCHUNGAJI MMOJA