Tuesday, March 13, 2012

UTANDAWAZI NI NINI? (WHAT IS GROBALIZATION?)

UTANDAWAZI:-
Nimfumo wa ulimwengu wenye lengo la kuinua uchumi, kwa njia ya biashara na mtiririko wa fedha. Ni shughuri za watu (kazi). Maarifa (Teknolojia) zanazofanywa bila kujali mipaka ya mataifa. Mfumo huu unavuka mipaka ya tamaduni, siasa na mazingira.

MITAZAMO YA MATAIFA MBALIMBALI JUU YA UTANDAWAZI.
Mataifa mengine yanauona utandawazi kama mfumo utakaoleta maendeleo na faida, yanauona utandawazi kama ufunguo wa maendeleo ya uchumi wa dunia. Mataifa mengine yanauona utandawazi kama mfumo unaolenga kuyanufaisha mataifa machache, hivyo mataifa haya yameingiwa na woga yakiamini kwamba utaondoa usawa kati ya taifa moja na jingine, utasababisha ajira kuwa ngumu na kuleta ugumu wa maisha. Utafiti unaonyesha kwamba, tangu mwaka 1980. utandawazi ulipoanza kuvuma, mataifa yaliyojiingiza katika mfumo wa utandawazi yanakuwa haraka kiuchumi na kupunguza umasikini. Utandawazi ulipoanza kushamiri, nchi za Latin Amerika, na Afrika zilisita kuingia katika mfumo huu. Uchumi wake ukaanza kudumaa na baadaye kuporomoka. Umasikini ukaanza kuongezeka na thamani ya fedha ikashuka haraka kwa kiwango cha kutisha. Nchi nyingi za Afrika zikawa nahali mbaya. Kadiri nchi hizi zilivyokubali kuingia katika utandawazi, mapato yao yaliongezeka, mabadiliko mengi ya kimaendeleo yakaanza kuonekana. Sasa ulimwengu umehakikisha kwamba, kuruhusu utandawazi ni kuruhusu uchumi kukua, ni kuruhusu maendeleo kupatikana ni kuondoa umaskini na ule ufukara wa kupindukia.
MAENEO MNNE YA UTANDAWAZI.
1. Biashara - Ushirikiano wa uuzaji bidhaa toka nchi moja hadi nchi nyingine utasaidia kuinua uchumi na kuleta maendeleo.  

2. Uwekezaji wa mitaji - (copital Investment). Nchi tajiri na watu wenye uwezo duniani wawekeze mitaji yao katika nchi maskini. 
 3. Uhuru wa kusafiri - Watu waruhusiwe kusafiri kutoka nchi moja hadi nchi nyingine kutafuta kazi na maisha bara.  
4. Kuenea kwa maarifa - (Teknolojia) kuboresha mawasiliano na upashanaji habari.

SERA ZA UTANDAWAZI (Globalization policies)
(a)Uchumi;
Ili kuinua maisha ya watu toka kwenye hali duni, ni lkazima uchumi ushikwe na mataifa tajiri, au makampuni yenye uwezo. Sera ya ubinafsishaji itumike. Wawekezaji waruhusiwe kuwekeza katika nchi maskini. 
 

 Mfumo wa soko huria uimarishwe. Nchi zisiwe na mipaka katika kuuza bidhaa zake. Mfano ni maonyesho ya biashara ya kimataifa Dar es salam. Kuanzishwa kwa maduka ya jumla. Lengo ni kuua biashara ndogondogo. 
Kuanzisha mfumo wa kununua kwa njia ya kadi (Card System) ili kupunguza kasi ya watu kutembea na fedha.
Sheria ya kutokuuza na kutokununua itapitishwa kupitia sera hii.
Mapendekezo ya sera hii ya uchumi ni kwamba siku za ibada na mapumziko zipunguzwe.

Watu wawe na muda mwingi wa kufanya kazi kwa bidii.

Waadventsta Wasabato watakuwa na nafasi ndogo ya kuajiriwa katika karne hii na zile zijazo kwa sababu ya msimamo wa imani yao. Nafasi pekee itakayowawezesha kuishi ni kuwa na ajira binafsi. Tunawashauri Waadventista kuwa na ujuzi zaidi ya mmoja, kuwa na mashamba na kujenga nyumba zao (Mithali 24:27).


Kuwa na sarafu moja, mfano wa nchi za ulaya.


(b) Siasa;

Amani ya ulimwengu haiwezi kupatikana mpaka ul.imwengu umekuwa na Serikali moja.
(A One World Government and One Unit Monetary System..... In the form of feudal system as it was in the middle Ages... The main is nothing less than to create a World System of Financial Control in private hands able to dominate the political system of each Country and the economy of the World as a whole).

Ulimwengu unakabiliwa na vita ya magaid waliotapakaa kila nchi. Maisha ya watu hayawezi kuboreshwa mpaka mataifa yawe na amani.
Suala la magaidi haliwezi kwisha mpaka mataifa yaungane na kuwa na nguvu moja.
Vyombo vinavyoshughulikia umoja kama vile UNO, AU, n.k viimarishwe. Liundwe jeshi la afrika , Ulaya n.k ili kulinda amani ya mataifa. Kuundwe mahakama za kimataifa ili kushughulikia makosa ya wahalifu.
Sheria zitungwe kwa pamoja.
Ndiyo kisa tuna bunge la Afrika Mashariki. Bunge la Afrika la Ulaya n.k.
(All law wil be uniform under a legal system af World Couts praticing the same unified code of laws, backed up by One World Government Policeforce and a One World unifed military to enforce laws in all former Countries where no national boundaries shal laws in all former countries where no national boundaries shall exist... those who are rebellious will simple be starved to death or be declared out lows, thus a target for any one who wishes to kill them).

Kwakuwa Jumapili itafanywa kuwa siku ya pekee ya ibada na mapumziko, watunza Sabato watahesabiwa kuwa wavunja sheria za nchi (Universal law) hivyo wastahili kuuwawa. Passprt zitatengenezwa zinazojumuisha nchi kadhaa pamoja.
  • Uhuru na jamii (Community freedom) 
 
  Utandawazi unadai uhuru wa mtu kutenda jambo bila kuingiliwa na mtu (Conscious freedom).
Hakuna kitu kinachoitwa dhambi ila ni mabadiliko ya jamii (Changes in the Society).
 
Kuoana jinsia moja ni mabadiliko ya jamii, Boy friend/Girl friend. Kumchapa mtoto ni kumdhalilisha n.k. Shetani amesaidia kusambaratisha familia kupitia mfumo wa utandawazi. Familia zikisambaratika hakuna kanisa tena.
 
  • Elimu
Sera ya utandawazi inawataka watu wasome. Mkakati ni kuboresha mashule na kuinua kiwango cha taaluma ya waalimu ili kupata wasomi watakaosimamia utandawazi.
Kwasababu ya kufufua uchumi na mwingiliano wa mataifa mbalimbali, hali ya maisha itapanda. Watakaofaulu kumudu maisha ya utandawazi ni watu waliosoma sana. Wale walio na elimu ndogo wataishi duni wala hawatajulikana kama wako duniani.

  • Mfumo wa maisha
Sera ya utandawazi inakubali mfumo wa maisha wa nchi za Magharibi kuwa ndio mfumo unaopaswa kukubalika katika nchi zote.
Ulimwengu unapaswa kufuata tamaduni za nchi za Magharibi katika mavazi, chakula, mahusiano, muziki n.k.
 
SAYANSI NA TEKNOLOJIA.  
Sera ya utandawazi itahakikisha kuwa sayansi na teknolojia inapenya kila mahali. Hili litasaidia kuufanya ulimwengu uwe kijiji kimoja. Television, simu, Computer, Internet, Satellite n.k. zitapelekwa kila mahali ili kuboresha mawasiliano. Sera hii itarahizisha mawasiliano katika tangazo la jumapili.
 
LUGHA.
Sera hii inakazia kuimarisha lugha tatu, Kingereza, Kiswahili, na Kifaransa.
 
DINI.
Utandawazi unapendekeza kuwepo na dini moja ya ulimwengu na siku moja ya ibada. (Universal Religion/Universal day of worship) Dini hiyo ni Roman Catholic, siku ya jumapili...
 
VYOMBO VINAVYOSIMAMIA UTANDAWAZI
  • Matajiri wenye fedha duniani.
  • Wafamasia wakubwa duniani.
  • Familia ya kifalme ya uingereza.
  • Viongozi wa viwanda vikuu duniani, ambao ni Marekani, Uingereza, Ujerumani, Italia, Australia, Newzealand n.k. (hawa ni wanachama wote wa G8).
  • Hivi karibuni viongozi wa G8 wamekutana uingereza, baadhi ya agenda zao jinsi ya kukabili ongezeko la joto duniani, maana mionzi ya jua inazidi kuharibu Ozone Layer. Mazingira, kusamehe madeni nchi maskini, kusaidia nchi za Afrika, uchumi na n.k.
  • Vyombo hivi vyote vinacheza mpira mmoja, kuhakikisha utandawazi unapindua dunia yote.
  • Yeyote anayeonekana kuwa kinyume na wenzake anauawa. Mifano ya waliouawa ni Rais Kenedy (USA) hivi karibuni Admiral Bhontto (Pakistani), na Aldo Moro Italy (hivi karibuni Admiral Borda na Willam Colby) Wanachama wa utandawazi waliuawa kwa sababu hawakuwa tayari kuendelea kushirikiana na wenzao na wakaanza kuvujisha siri za agenda za utandawazi nje.
*********************************************
VITABU VYA REJEA.
1.  World Economic Outlook, International  Monitary Fund, Washington DC May 2000.
 
2.  Nicholas Crafts Globalization and Growith in the Twentieth Century, IMF Working paper, WP/00/44, Washington DC, April 2000.
 
3.  World Economy Outlook, May 2000 chapter 4 Dr. John Coleman, Conspirators Hierachy. The story of the Committee of 300, Pg 161.  

No comments: