Saturday, November 4, 2017

THAMANI YAKO IPO TU UKIWA HAI..

Kwakuwa lipo tumaini kwa yule aliyeambatana na wote walio hai; (maana ni afadhali mbwa aliye hai kuliko simba aliyekufa);
 Mhubiri 9:4

Kwa maana linalowatukia wanadamu linawatukia wanyama; jambo moja lawatukia; anavyokufa huyu ndivyo anavyokufa huyu; naam, wote wanayo pumzi moja; wala mwanadamu hana kitu cha kumpita mnyama; kwa maana yote ni ubatili.
 Mhubiri 3:19

MUHIMU: Kuishi sawa sawa na neno la Mungu..maana uhai wa kila kiumbe upo mikononi mwake.

ZINGATIA: Mwanadamu anakufa sawa sawa na mnyama ila liko tumaini kwa mwadamu ikiwa tu atayatoa maisha yake kwa Yesu.. Huyu Yesu ndo mwenye uwezo wa kukufanya uishi tena baada ya kifo inamaana yeye ni ufufuo na uzima.

KUMBUKA: Mwanadamu anamzidi mnyama kwa kuwa amenunuliwa kwa damu ya thamani ya Yesu Kristo.. Mchague Yesu sasa na umfanye kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako.

HAKIKA: UTAISHI TENA.

YESU ANAPITA KWAKO LEO.


LUKA 17:11-14
11. Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, Yesu alikuwa akipita katikati ya Samaria na Galilaya.
12. Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,
13. wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!
14. Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.
Najua Mpo wengi leo mnapitia changamoto za aina mbalimbali.
Nakukumbusha kuwa Yesu anapita kwenye mji wako leo, anapita kwenye biashara yako, anapita kwenye ugonjwa wako, anapita kwenye ndoa yako.

Nishida gani inakusumbua? Mwambie Yesu.
Sema maneno haya EE YESU BWANA MKUBWA UNIREHEMU.

Wale wote waliokucheka kwa sababu ya shida yako sasa jionyeshe kwao, ili nao wasimulie matendo makuu ya Mungu aliyo kutendea.

Bwana akupe hitaji la moyo wako.

KIBONZO


Dawa ya nguvu za kiume hii hapa👇🏻👇🏻 Sasa wewe endelea kuzurura kutwa nzima kuwatafuta wamasai na waganga ili wakupatie dawa ya nguvu za kiume.
Ukiona mke wako anakwambia huna nguvu za kiume ujue mfuko umetoboka😁😁😁hakuna upungufu wa nguvu za kiume kwenye pesa na hakuna dawa ya kuongeza nguvu za kiume duniani..my friend utamaliza soli ya kiatu bure kwa kuwatafuta wamasai badala yake fanya kazi kwa bidii ili ule chakula chenye rishe kamili, pia itakupunguzia mawazo na msongo wa maisha.
Na nyie akina mama mmmmmh Mungu anawaona, punguzeni midomo, kumsakama mtoto wa mwanamke mwenzako kutwa nzima, badala uwe faraja kwake wewe unakuwa chanzo cha stress.
Kama pesa ni rahisi kuipata mbona wewe huna? Kutwa nzima unamsumbua mbaba wa watu kwa nini asipate upungufu wa nguvu za kiume..

Mawazo + kukosa hela/maisha magumu = upungufu wa nguvu za kiume.