Habari nyingine

FREEMASON NA VIONGOZI WA TANZANIA

Sir Andy Chande akiwa na Rais Jakaya Kikwete.
Andy Chande akiwa na Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa.
 
...Andy akiwa na Mzee Mwinyi.
 
 
...Chande na Karume.
 
 
....Chande na Sumaye.
 
 
 
Na Elvan Stambuli---Wa Gazeti la Uwazi.

JAMII ya Siri (Secret Society), Freemason, imedaiwa 
kuwa na siri nzito na viongozi wakuu wa nchi yetu, 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Madai hayo, 
yametokana na kile kinachoonekana kwamba Kiongozi 
Mkuu wa Freemason, Afrika Mashariki, Sir Andy 
Chande, amekuwa akijiweka karibu na viongozi wakuu 
wa nchi hii kila awamu, hivyo kuonesha kuwa kuna 
kitu 
anakitafuta. Kikubwa kinachodaiwa ni kuwa Chande 
anatumiwa na Freemason kuhakikisha kwamba kila 
kiongozi wa nchi hii anakuwa karibu na jamii hiyo ya 
siri.
 
Inazidi kudaiwa kuwa Freemason inafanya njama za 
hali ya juu kujiweka karibu na Ikulu, ikiwa na mpango 
wao wa muda mrefu wa kusimika rais ambaye ni 
memba wa jamii hiyo katika awamu zinazokuja.

Uchunguzi wa Uwazi umeonesha kuwa Chande 
amekuwa karibu na Ikulu tangu Awamu ya Kwanza 
chini ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere 
na amedumu kujiweka karibu na viongozi wa nchi 
mpaka awamu hii ya nne chini ya Rais Jakaya Kikwete. 
Wakati inabainishwa hivyo nchini, wachambuzi wa 
mambo ya jamii za siri, ikiwemo Illuminati na Skull & 
Bones, wamekuwa wakiitaja Freemason kuwa na njama 
za kuitawala dunia kwa kuhakikisha kwamba kiongozi 
mkuu wa kila nchi duniani anakuwa memba wa jamii 
hiyo.
 
MKAPA 
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa Rais Mstaafu, 
Benjamin Mkapa alipokuwa madarakani aliwahi 
kualikwa akiwa na mkewe katika shughuli ya 
Freemasons kutimiza miaka 100 nchini, sherehe 
iliyojumuisha wageni waalikwa 350 kutoka nchi 
mbalimbali duniani japokuwa hapa nchini haikutangazwa sana.
 
Kwa mujibu wa Sir Andy Chande katika mahojiano yake 
na mwandishi mkongwe nchini, Ernest C. Ambali wa 
Gazeti la The Guardian, lililokuwa mitaani Oktoba 8, 
2004 alitaja waziwazi kuwa mgeni rasmi katika 
shughuli yao ni Rais Benjamini Mkapa na mkewe Mama 
Anna Mkapa. Katika shughuli hiyo pia walikuwepo 
wafanyabiashara wakubwa,wanadiplomasia, mawaziri n.k.
NYERERE
 
Sir Andy Chande akiwa nchini India katika Mji wa 
Chennai kuzindua hekalu lao la East Star, alieleza 
kwamba marais wawili wa kwanza wa Tanzania 
hawakuwa Freemasons lakini walifahamu taasisi hiyo ni 
nini na inafanya nini katika nchi hii. Aidha, aliwahi 
kuweka wazi kuwa hata Rais wa Kwanza wa Tanzania, 
Mwalimu Julius Nyerere alikuwa akiijua taasisi hiyo na 
aliwahi kuikingia kifua ilipotaka kunyang’anywa jengo 
lao ambalo lipo Sokoine Drive, katikati ya Jiji la Dar es 
Salaam linalofahamika kama Freemasons Hall. 
Uchunguzi umeonesha kuwa viongozi wengi wakuu wa 
serikali wanafahamu shughuli za taasisi hiyo, hali 
iliyothibitishwa na kiongozi wa Freemasons, Sir Chande 
ambaye amekuwa akipiga nao picha mara kwa mara 
wakati wa hafla. Viongozi wengine wa nchi waliowahi 
kualikwa au kumualika kiongozi wa taasisi hiyo ni Rais 
Jakaya Kikwete, Rais Mstaafu wa Zanzibar, Amani 
Karume, Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye na 
Rais Mstaafu, Sheikh Ally Hassan Mwinyi.

KITABU CHAKE 
Rais mstaafu, Mkapa katika kitabu cha Sir Andy 
 
Chande kiitwacho ‘Shujaa wa Afrika, Safari kutoka Bukene’ ameandika utangulizi akisema Chande alikuwa 
 
akijulikana kama JK na alifahamiana naye baada ya 
 
kumuingiza katika bodi ya Shule ya Shaaban Robert. 
 
Mkapa amesema Sir Chande ametambuliwa na kupewa 
 
heshima na vyombo vya taifa na vya kimataifa, 
 
heshima ambayo anaistahili kabisa. “Mimi nafurahi kuhusishwa 
 
na kutambuliwa kwa sifa na heshima anayopewa,” 
 
alisema Mkapa katika maandishi yake. Mnajimu 
 
maarufu nchini, Maalim Hassan Yahya Hussein ambaye 
 
amekuwa akiandika makala za Freemasons katika 
 
gazeti hili, alipohojiwa na mwandishi wetu kama 
 
viongozi hao wanafahamu taasisi hiyo inajishughulisha 
 
na nini, alisema japokuwa hakuna anayejua 
 
wanachokifanya wanachama wa Freemasons huku 
 
uraiani lakini anaamini kuwa viongozi wakuu wa nchi 
 
wanajua kila kitu. 
 
“Kwa kawaida huwezi kualikwa katika chama au taasisi 
 
fulani bila kujua shughuli zao hasa kwa viongozi 
 
wakuu kama hawa, sasa kama waheshimiwa Mkapa, 
 
Mwinyi, Sumaye, Karume na Kikwete waliwahi kualikwa 
 
au kumualika Sir Andy Chande ni wazi kuwa 
 
wanafahamu shughuli zake na taasisi yake,” alisema 
 
Maalim Hassan.
 
KIMATAIFA 
 
Hivi karibuni, nchini Kenya, aliyekuwa Waziri wa 
 
Usalama, Profesa George Saitoti aliyefariki kwa ajali ya 
 
helikopta, kifo chake kimehusishwa na Freemasons 
 
kwa kudaiwa kuwa alipokuwa Makamu wa Rais wa Kenya 
 
wakati wa utawala wa Daniel Arap Moi, aliwahi kupiga 
 
marufuku makanisa au dini zinazojihusisha na imani za kishetani.
 
Imeelezwa kuwa wengi wanadhani kuwa angeweza 
 
kuwa Rais wa Kenya iwapo angegombea hivyo 
 
kurejesha amri yake ya kupiga marufuku imani 
 
ambayo yeye haiamini.
 
Aidha kuna baadhi ya viongozi duniani wanahusishwa 
 
na Freemasons baada ya kuonekana picha zao 
 
wakionesha alama za taasisi hiyo, baadhi yao ni Rais 
 
Barack Obama, George Bush, Sadam Hussein na 
 
Muammar Ghaddafi.






WANAFUNZI WA SHULE YA MPECHI NA SABASABA, WAKIWA KATIKA MAANDAMANO


Wanafunzi wa Shule za Mpechi na Sabasaba, wakiwa katika maandamano baada ya mwanafunzi mwenzao kugongwa na Tax, na kupoteza maisha yake, katika eneo la Ofisi za Halmashauri ya Wilaya. walikuwa wakitoa wito kwa madereva kuwa makini, aidha waliomba serikali ijemge matuta katika eneo hilo.
                                             Picha na Jonas Tave




Moto mkubwa ulioteketeza sako la sido mkoani Mbeya vibanda vingi viliteketea.
Lakini Biblia inasemaje? Mathayo 24....     Hizi ni kengele za kutushitua tujue kua tunaishi nyakati za mwisho,

1 comment:

Anonymous said...

Watoto, ni wakati wa mwisho; kama vile mlivyosikia kwamba mpinga kristo yuaja, hata sasa wapinga kristo wengi wamekwisha kuwepo. kwasababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho, 1 Yohana 2:18

Adui anajiandaa kwa ajili ya kampeni yake ya mwisho dhidi ya kanisa. Amejificha sana asionekane na watu kiasi kwamba wengi hawafikiri ya kwamba anishi, na vivyo hivyo, wengi hawatambui shughuli na ukubwa wa uwezo wake.

Mwanadamu ni mateka wa Shetani na kwa asili anafuata mapendekezo yake na matashi yake. Ndani yake hakuna nguvu ya kupinga na kuukataa uovu. Ni pale tu Kristo anapokua ndani yake kwa imani iliyo hai. Namna yoyote nyingine yakujilinda haifai kabisa. Ni kupitia kwa Kristo peke yake ndipo uwezo wa Shetani unazuiwa. Huu ni ukweli wa muhimu sana ambao wote wanapaswa kuuelewa. Shetani anashughulika sana kila wakati, akienda huku na kule, akipanda na kushuka duniani, akitafuta mtu ammeze. Lakini ombi la dhati la imani litachanganya jitihada zake hata zile zenye nguvu sana...

Shetani anategemea kuwashinda watu wa Mungu kwa ujumla katika maangamizi yanayokuja katika dunia. Wakati kuja kwa Kristo kunapokaribia, yeye (Shetani) atazidisha azma yake na uthabiti katika jitihada ya kuwaangusha. Wanaume kwa wanawake watainuka wakidai kuwa na nuru mpya au ufunuo mpya ambao kwa kawaida unavuruga imani ambayo imekuwepo katika msingi imara siku zote. Hata ingawa mafundisho yao hayatakuwa na vithibitisho vya neno la Mungu, bado bado roho zitadanganywa. Taarifa za uongo zitasambazwa na baadhi watanaswa katika mtego huu... Hatuwezi kuwa wazembe katika kuangalia aina yoyote ile ya makosa, kwani Shetani anadumu kutafuta namna ya kuwavuta watu toka katikz kweli...

Wapo watu ambao hawako imara kitabia. Wako kama donge la tope la udongo wa mfinyanzi ambalo laweza kuumbwa katika mwonekano wowote... Udhaifu huu. kukosa maamuzi, kutokuwajibika, vyapaswa vishindwe. Katika tabia ya kweli ya Ukristo ipo hali ya ujasiri usuo wa kawaida ambao hauwezi kutengenezwa au kushushwa hata hali iwe mbaya kiasi gani. Watu wanapaswa kuwa na msimsmo katika maadili, unyofu ambao hauwezi kubezwa, kuhongwa au kutishwa.

Mungu ameweka mipaka ambayo shetani hawezi kupita. Imani yetu iliyo takatifu sana ndiyo mipaka; na kama tutajijenga wenyewe zaidi katika imani, basi tutakuwa salama katika utunzaji unaotoka kwa Mwenyezi.

Mungu akubariki sana unapotafakari ujumbe huu.