Sunday, September 16, 2018

MOYO WA SHUKURANI

Kunakisa katika biblia, huwa nashangaa sana..bwana Yesu katika pita pita yake alikutana na watu 10 wenye ukoma wakasimama mbali, wakapaza sauti wakisema Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu! ...akawambia enendeni mkajionyeshe kwa makuhani. Wakiwa njiani ndipo muujiza wa uponyaji ulitimia. Viungo vyao vikarejea sawasawa. 
Luka 17:12-19 
 
Sitaki nielezee saana mtu mwenye ukoma yukoje..nataka tujifunze thamani ya kushukuru. Watu 10 waliponywa ukoma lakini ni mmoja pekee ndiye alikumbuka kurudi kushukuru..! Kitu ambacho kilimshangaza sana Yesu, (..hawakutakaswa wote kumi? Wale tisa wako wapi?) Unaweza kudhani pengine wamesahau maumivu na athali za ugonjwa wa ukoma. 
 
Wapendwa, naomba tujifunze kitu kutoka kwa yule mmoja (msamalia) aliyekumbuka kurudi kushukuru. Kushukuru ni kutambua thamani ya fadhira ulizotendewa..kushukuru ni kumpa moyo yule aliyekusaidia, kushukuru ni kuonyesha utu. Kushukuru ni kutambua msaada uliofanyiwa. 
 
Kumbuka kuwashukuru waliokusaidia ulipoumwa, ulipotingwa na jambo fulani. Kumbuka kuwashukuru waliokulipia ada yako ya masomo hadi ukamaliza masomo yako. 
 
 Kunawatu wamekuwezesha kwenye biashara yako hadi ikasitawi, acha dharau, usiwasahau ukadhani ni kwa juhudi zako, kumbuka kuwashukuru waliokusapoti hadi biashara yako ikasitawi. Hata kwenye familia hatulingani, yupo aliyebeba familia, anajitoa kwa hali na mali..mtieni moyo na kumshukuru. 
 
 Ipo nguvu kwenye kushukuru, tujifunze kushukuru kwa kila jambo.
 


No comments: