Sunday, April 16, 2017

MIPANGO YA AMANI NA MAANDALIZI YA VITA

Tunaishi katika ulimwengu huu wa ajabu. Kila mmoja anaafiki kwamba tungeipatia nafasi amani; lakini basi, zile chuki zilizokandamizwa kwa kipindi cha karne fulani zilizopita, zinalipuka na kuwa vita ya wazi. Nabii Mika na Yoeli walitabiri kwamba wakati ule ule mataifa yatakapokuwa yanasema juu ya shauku yao ya kuwa na amani (Mika 4:1-3) WATALAZIMIKA KUJIANDAA KWA VITA...kutokana na shauku yao waliyo nayo dhidi ya majirani zao (Yoeli 3:9-13).....

Marekani imefanya shambulizi la makombora takriban 50 ,yalipigwa katika kambi ya jeshi la anga mjini Homs nchini Syria.
Awali maafisa wa Marekani walisema wana mpango wa kuchukua hatua za kijeshi baada ya Syria kushutumiwa kutumia silaha za kemikali katika mji unaodhibitiwa na waasi, ambapo watu kadhaa wamepoteza maisha.Rais wa Marekani Donald Trump amesema ameamuru kutekelezwa kwa mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Syria huku akitoa wito kwa mataifa yote yaliyostaarabika kukomesha vitendo vya mauaji na umwagaji damu nchini humo
URUSI YACHUKIZWA NA MAREKANI KUISHAMBULIA SYRIA
Urusi imechukizwa na uamuzi wa Marekani wa kuishambulia kambi ya jeshi la anga mjini Homs nchini Syria kwa makombora.Urusi inaunga mkono serikali ya Rais Bashar al-Assad[SYRIA] na imekashifu shambulizi hilo ambalo linadaiwa kuua watu sita.

CHINA,KOREA KUSINI zimeionya kuiadhibu Pyongyang iwapo itarusha kombora lolote
Mataifa mawili ya bara Asia, yametoa onyo kali dhidi ya utawala wa Pyongyang, kwamba itaadhibiwa vikali, iwapo itadhubutu tena kufanyia majaribio zana zake za kinuklia.

Mataifa hayo, Korea Kusini na China, yamekiri kuchukua hatua kali dhidi ya Korea Kaskazini, ikiwa tena itafanyia majaribio zana zake za kitonoradi zinazovuka mipaka ya kimataifa.

MAREKANI YATISHIA kuiadhibu Korea KaskaziniTrump: "tutaidhibiti Korea Kaskazini".." HATUTAIVUMILIA KOREA KASKAZINI"
Rais Trump amesema kuwa Marekani imejiandaa kibinafsi kukabiliana na tishio la nyuklia linaloletwa na Korea Kaskazini.
KOREA KASKAZINI : Tutatumia ''silaha kali'' kujilinda dhidi ya US

Korea Kaskazini imesema kuwa itajitetea kwa kutumia silaha kali ili kujibu hatua ya Marekani kupeleka wanamaji wake katika rasi ya Korea.
Wizara ya maswala ya kigeni ilinukuu shirika la habari la serikali KCNA lililosema kuwa hatua hiyo ya Marekani inaonyesha uvamizi wa kijinga uliofika awamu yenye hatari kubwa.

Jeshi la Marekani katika maeneo ya Pacific limesema kuwa hatua hiyo inalenga kuonyesha Marekani imejiandaa kwa lolote lile.
Zamani sana Biblia ilionyesha picha hii ya mgogoro wetu wa sasa wa kuwa na AMANI au VITA, kisha ikatangaza kwamba amani ya kudumu itatawala katika dunia hii wakati ule tu YESU ATAKAPOKUJA.

Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi ya vita; angalieni, msitishwe; maana hayo hayana budi kutukia; lakini ule mwisho bado.
- Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.Mathayo 24 :6- 7
Luka 21 : 28 - Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.

No comments: