Saturday, August 19, 2017

YEREMIA, MSEMAJI WA MUNGU

Ni vema mtu autarajie wokovu wa Bwana Na kumngojea kwa utulivu. Maombolezo 3:26.

Kati ya wale waliotumaini kuwa na uamsho wa kudumu wa kiroho ikiwa matokeo ya matengenezo chini ya Yosia alikuwa Yeremia, aliyeitwa na Mungu ili aingie katika nafasi ya kuwa nabii akiwa bado kijana…
Ndani ya kijana Yeremia, Mungu aliona mtu ambaye angeaminika na ambaye angesimama katika haki dhidi ya upinzani mkubwa… Bwana akamwambia mjumbe wake aliyemchagua; “Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru.”….
Kwa miaka arobaini ilimpasa Yeremia kusimama mbele za taifa kama shahidi ya ukweli na uadilifu. Katika wakati wa uasi usio na kifani ilimpasa aoneshe ibada ya Mungu pekee wa kweli katika mfano wa maisha na tabia. Wakati wa utekwaji wa kutisha wa Yerusalemu ilimpasa awe msemaji wa Yehova.
Akiwa kwa asili na silika ya kuwa mwoga na mwenye kunywea, Yeremia alitamani amani na utulivu wa maisha ya kujitenga, ambapo asingelazimika kushuhudia maendeleo ya mioyo migumu ya taifa lake alilolipenda. Moyo wake ulikamuliwa kwa maumivu kutokana na uharibifu ulioletwa na dhambi….
Uzoefu aliopitia Yeremia siku za ujana wake na pia katika siku za mbeleni za huduma yake, ulimpa fundisho kwamba “njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu. Ee Bwana, unirudi kwa haki; si kwa hasira yako, usije ukaniangamiza” (Yeremia 10:23, 24).
Alipoitwa kukinywea kikombe cha mateso na huzuni na alipojaribiwa wakati wa shida yake kusema, “Nguvu zangu zimepotea, na tumaini langu kwa Bwana,” alikumbuka majaliwa ya Mungu kwa ajili yake na kwa kushangilia akasema, “Ni huruma za Bwana kwamba hatuangamii, kwa kuwa rehema zake hazikomi…Bwana ndiye fungu langu, husema nafsi yangu, kwa hiyo nitamtumaini yeye.”

No comments: