Saturday, November 4, 2017

YESU ANAPITA KWAKO LEO.


LUKA 17:11-14
11. Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, Yesu alikuwa akipita katikati ya Samaria na Galilaya.
12. Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,
13. wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!
14. Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.
Najua Mpo wengi leo mnapitia changamoto za aina mbalimbali.
Nakukumbusha kuwa Yesu anapita kwenye mji wako leo, anapita kwenye biashara yako, anapita kwenye ugonjwa wako, anapita kwenye ndoa yako.

Nishida gani inakusumbua? Mwambie Yesu.
Sema maneno haya EE YESU BWANA MKUBWA UNIREHEMU.

Wale wote waliokucheka kwa sababu ya shida yako sasa jionyeshe kwao, ili nao wasimulie matendo makuu ya Mungu aliyo kutendea.

Bwana akupe hitaji la moyo wako.

No comments: