Wednesday, May 10, 2017

NINI SIRI?


“Delila akamwambia Samsoni, Tafadhali uniambie asili ya nguvu zako nyingi, na jinsi uwezavyo kufungwa, ili uteswe.” Waamuzi 16:6.

Waisraeli walimweka Samsoni kuwa Mwamuzi juu yao, naye alitawala juu ya Israeli kwa miaka ishirini. Ila kosa moja hufungua njia kwa kosa jingine. Alivutiwa na mihemko ya kianasa iliyomwongoza kwenye anguko. “Alimpenda mwanamke mmoja katika bonde la Soreki,” siyo mbali sana na nyumbani kwao. Jina la mwanamke huyo alikuwa Delila, “mwangamizi.” Wafilisti walitazama kwa makini mwenendo wa huyu adui yao, na alipojidhalilisha mwenyewe kwa kujifungamanisha na mwanamke huyu wa Kifilisti, walinuia, kupitia Delila, kukamilisha mpango wa kumwangamiza.

Jopo la watu wa heshima lenye kuundwa na mtu mmoja mmoja toka kila jimbo la Wafilisti walisafiri hadi bonde la Soreki. Hawakuthubutu kumshambulia akiwa anamiliki hazina ya nguvu zake tele, bali ilikuwa ni mpango wao kujifunza, ikiwezekana, siri ya nguvu zake. Hivyo walimhonga Delila atafute siri ya nguvu za Samsoni kisha awafunulie.

Kadiri msaliti alivyomsonga Samsoni kwa maswali, alimdhihaki kwa kumwambia nguvu zake zaweza kutoweka, awe sawa na watu wengine dhaifu, iwapo mambo fulani yatatendeka. Kila aliloambiwa alijaribisha, ila akagundua ni uongo kwani nguvu zake hazikutoweka. Kisha akamlilia akisema, “Mbona umenidanganya mara zote hizi, ukisema wanipenda, na roho yako haipo pamoja nami?” . . . Mara tatu Samsoni ameona ushahidi dhahiri kuwa Wafilisti wamepanga njama kumwangamiza kupitia huyu mpenzi wake; ila pale mpango huo ulipoonekana kukwama; mwanamke huyo alilia sana akidai amemhadaa, hampendi, naye mumewe akapumbazika asitambue hatari iliyoko mbele yake.
Mwamuzi huyu wa Israeli alitumia saa nyingi mbele ya mwanamke huyu mlaghai, saa ambazo angalizitumia kwa mafanikio na maendeleo ya watu wake. Tamaa hizi zenye kupofusha ziwezazo kumfanya shujaa aonekane dhaifu kabisa, zilikuwa zimeshamtawala akili na dhamiri.

Ukengeufu wa Samsoni ulikuwa taratibu na wa hakika. Mwanzoni hakudhamiria kufunua siri, ila kwa hiari amejitosa mwenyewe ndani ya wavu wa msaliti wa roho, na kamba zangu zilikuwa zikimsonga kutoka kila upande.

No comments: