Tuesday, May 2, 2017

MUNGU NI CHEO CHENYE NAFSI 3

MUNGU BABA, MUNGU MWANA NA MUNGU ROHO MTAKATIFU. 

KWA NINI MUNGU MWANA YAANI YESU KRISTO ALIKUFA MSALABANI NA SIYO MUNGU BABA AU MUNGU ROHO MTAKATIFU?
 
1. Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu ni baraza uumbaji ambalo liliamua Mungu Mwana yaani Yesu Kristo awe msemaji na Mtendaji mkuu. Yohana 1:1-3, 14 "Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu. 
 Vyote vilifanyika kwa huyo: wala pasipo yeye hakukufanyika cho chote kilichofanyika... Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu: nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba: amejaa neema na kweli. "
 
Wakolosai 1:14-20 "... ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi: naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana: ikiwa ni viti vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka: vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye. Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa: naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote. Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae: na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake, akisha kufanya amani kwa damu ya msalaba wake:kwa yeye, ikiwa ni vitu vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni.".
 
Yesu ndiye aliyemwambia Adamu, "walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika". Ndiyo sababu Yesu anaitwa Neno. Msemaji mkuu wa serikali ya mbinguni.
Yesu alikufa msalabani kwa niaba ya mwanadamu. Kwa kuwa ndiye aliyesema 'utakufa hakika'. Kama asingekufa na wanadamu wasamehewe basi shetani angedai kuwa Mungu ni mwongo. Ndiyo maana neema na haki zilibusiana msalabani. Yaani neema mwanadamu asamehewe dhambi alipotenda. Haki mwanadamu atii amri na maagizo ya Mungu baada ya kusamehewa dhambi. Yesu alikufa msalabani ili kumtetea mwanadamu asife na pia kutetea maagizo au amri zake zisipuuzwe. Ndiyo maana mtu anapoasi anamrudisha Yesu msalabani. 

Waebrania 6:4-6 "Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa wahirika wa Roho Mtakatifu, na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu... Kwa kuwa wamsulubisha Mwana wa Mungu mara ya pili...".

No comments: