Wednesday, May 10, 2017

UTAVUNA ULICHOPANDA


📖Mwanangu, wenye dhambi wakikushawishi, Wewe usiku-bali.” Mithali 1:10

👉🏼Samsoni wakati wa matatizo makuu yaliyomsibu alikuwa na chimbuko lile lile la nguvu kama ilivyokuwa kwa Yusufu. Angaliweza kuchagua jema au baya kama apendavyo. Badala ya kushikilia nguvu za Mungu, aliruhusu tamaa yake mbaya imtawale. Uwezo wa kufikiri ulipotoshwa, uwezo wa kimaadili ulichafuliwa. Mungu alikuwa amemwita Samsoni kwa wadhifa wa jukumu kubwa, heshima, na manufaa; ila kwanza angalipaswa kujua uongozi kwa kujifunza utii kwa sheria za Mungu.

👉🏼Yusufu alikuwa mtu huru mwenye maamuzi huru. Mema na mabaya yalikuwa mbele yake. Angaliweza kuchagua njia ya usafi, utakatifu, heshima, au njia ya uasherati na vitendo vya aibu. Alichagua njia sahihi, naye Mungu alitukuzwa. Samsoni, chini ya majaribu ya jinsi iyo hiyo, ambayo alijisababishia yeye mwenyewe, alijiachia akatekwa na tamaa mbaya. Njia aliyoichagua ilimfanya aishie kwenye aibu, majanga, na hatimaye kifo. Kuna utofauti gani ukilinganisha na maisha ya Yusufu.

👉🏼BWANA katika Neno lake alikuwa ameweka wazi kuwa watu wake hawapaswi kujifungamanisha na wale wasiompenda au kumcha. Watu wa jinsi hiyo hawataridhika kupewa heshima na upendo ule waustahilio pekee. Bali watadumu kutafuta kupata kutoka kwa mke au mume mcha Mungu upendeleo maalumu utakaohusika kupotoka na kuyaacha mapenzi ya Mungu.

👉🏼Kwa mwanamume mcha Mungu, na kwa kanisa alilojifungamanisha nalo, mke au rafiki wa kidunia ni mpelelezi kwenye kambi hiyo, ambaye atakuwa akitafuta daima kila fursa kusaliti mtumishi wa Kristo, na kumfichua kwa mashambulizi ya adui.

👉🏼Historia ya Samsoni hutoa fundisho kwa wale ambao tabia zao hazijaundwa, ambao hawajaingia kwenye jukwaa la maisha ya shughuli. Vijana wanaoingia kwenye shule zetu na vyuo watapata kila darasa la kuulisha ubongo. Iwapo wanatamani michezo na mizaha; iwapo wanachagua kuacha mema na kukumbatia uovu, wanayo fursa hiyo. Dhambi na utakatifu vipo mbele yao, na uchaguzi ni wao. Ila hebu wakumbuke kuwa “Kile mtu apandacho, ndicho atakachovuna.”

No comments: