Saturday, June 23, 2012

KWA NINI KUNAMAHANGAIKO DUNIANI?


Sehemu ya mwisho.


Wewe nami tumekutwa katikati ya pambano linalochanganya la ulimwengu, ugomvi kati ya mamlaka na uasi, kati ya Muumbaji na Shetani, muasi wa kwanza.! Sisi si watazamaji. Tunahusika, tupende tusipende.
Dhana kwamba Shetani ni hadithi tu ama mvuto fulani tu, hutuacha tukiwa hatukujiandaa kabisa kukabiliana na kiumbe mwenye akili kama alivyo.
Kitabu cha Ufunuo kinasema: Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.! Ufunuo 12:12.
Kwa sababu hiyo, furahini enyi mbingu na vyote vilivyomo ndani yenu. Lakini, ole wenu nchi na bahari, maana Ibilisi amewajieni akiwa na ghadhabu kuu, kwa sababu anajua kwamba siku zake zilizobakia ni chache.
Petro aliandika onyo hili: Muwe na kiasi na kukesha kwa adui, Ibilisi,  mshitaki wenu kama simba angurumaye huzungukazunguka akitafuta mtu ammeze. akitafuta mtu ammeze. 1 Petro 5:8.
Lakini hata ingawa Shetani hutenda ubaya zaidi, Mungu wa uumbaji anao mpango wa kuumba upya ambao umjumuisha Mwana wake Yesu- Mwana wake wa thamani aliyekuwa hiari kufa ili kulipa deni letu ili tuwe na uzima wa milele.
Shetani alitenda kazi kupitia kwa Mfalme Herode ili kumuangamiza mtoto Kristo (Akashindwa).
Shetani alikuja kwa Yesu jangwani, akijifanya kuwa malaika kutoka mbinguni akiwa na majaribu makuu matatu (Akashindwa).
Shetani alichochea halaiki ya watu ili wamwangamize Yesu pale Kalvari (Alikuwa adui aliyeshindwa milele).


Ingawa kulikuwa na Kalvari, kulikuwa pia na ufufuo! Mungu Asifiwe!!
Hivyo ndivyo ilivyokuwa ya kwamba Mungu alimtoa Mwanae; na Mwana akajitoa mwenyewe, ili kubatilisha hatima yako na yangu.! Ilikuwa ni saa ya ushindi, siku ya kutamka uhuru kwa ajili ya wafungwa wote wa mwovu katika Sayari Dunia.
Siku hiyo Shetani akawa adui aliyeshindwa! Kristo kwa mauti yake akapata haki ya kuangamiza uovu wote na mateso.! Paulo aliandika katika Waebrania 2:14: Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi.
Shetani alidhihihirisha mbele ya wenye ufahamu wote wa ulimwengu kuwa yeye ni kiumbe wa jinsi gani. Na bado anaendelea kudhihirisha jinsi ambavyo angeuendesha ulimwengu.! Vimbunga, matetemeko, mafuriko, uhalifu, maradhi, huzuni, na maumivu!! Haya tunayaona Lakini nguvu isimamayo nyuma ya yote haya bila kuonekana kwa macho ni ile kazi ya Shetani ipitayo akili ya mwanadamu.
Haya maafa siyo matendo ya Mungu- haya ni matendo ya mwovu.
Waweza kuwa unashangaa juu ya masikitiko, huzuni, na matatizo katika maisha yako binafsi. Waweza kuwa unashangaa juu ya kifo cha mtoto ama mpendwa na kuuliza Yu wapi Mungu?
Biblia inafundisha ya kuwa Mungu yupo. Yupo katikati ya huzuni zako masikitiko, na matatizo.! Na atakuja muda si kitambo kushughulikia tatizo la dhambi na mateso.
Habari njema ni kwamba sayari hii nzuri, iliyotekwa na Shetani, i karibu kuokolewa.! Ufahamu huu wapaswa kunyamazisha hofu za abiria wenye shauku, juu ya sayari inayokwenda kombo!! Mungu anao mpango wa kumwangamiza Shetani-- mwovu mdanganyifu.
Hebu tuone kile ambacho Biblia inasema juu ya Shetani: .....Nami nimekuangamiza, Ewe kerubi ufunikaye....... Basi nimetokeza moto kutoka ndani yako; nao umekuteketeza, nami nimekufanya kuwa majivu juu ya nchi... Ezekieli 28:16,18! Dhambi na taabu vitapotea milele.
Ndiyo, rafiki, Yesu anakuja upesi! Siyo kama mtu wa chini wa Galilaya, siyo kama aliyetukanwa, aliyetemewa mate, na aliyekataliwa. Siyo kama mtu anayening'inia msalabani, bali kama Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana akiwa na haki ya kutawala! Lazima tuwe tayari kukutana naye maana kama tukikosa hilo, tumekosa kila kitu
Utii wako uko wapi? Swala leo ni, Ni nani tutakayemwamini? Ni nani tutakayemfuata? Mungu mwenye upendo -au malaika aliyeanguka?
Mistari inachorwa;  Ulimwengu nzima unagawanywa katika sehemu
mbili. Wewe uko upande wa nani?
Kwa kila moyo usiotulia, moyo mpweke, kwa kila roho inayoumia, yenye hatia, kwa watoto wake wote katika sayari dunia iliyo katika uasi, Yesu anatoa mwaliko wa upendo:
Njoni kwangu ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Wote anipao Baba watakuja kwangu; ye yote ajaye kwangu, sitamtupa nje kamwe! Yohana 6:37 Je, hii si habari ya ajabu? Mathayo 11:28.
Katikati ya misiba ya maisha, simanzi, huzuni na kukata tamaa, Yesu yuko hapo.! Anaelewa simanzi uliyo nayo sasa hivi. Yesu anaelewa unachokipitia mwili wako unaporaruliwa na ugonjwa. Anajua maumivu. Aliyapitia wakati watu wakatili walipopigilia misumari yenye kukwaruza katika mikono Yake. Anajua upweke Aliupitia wakati aliponing'inia peke yake katika giza msalabani. Anajua umaskini.
Aliupitia alipotembea katika barabara zenye vumbi za Palestina akiwa na chakula kidogo tu huku akiwa hana mahali pa kupaita nyumbani.
Njoo kwake leo.
Atakupatia tumaini jipya na moyo mkuu. Hapa kuna habari nzuri kuliko zote. Siku moja hivi karibuni Yesu huyu atakuja tena na kukomesha taabu zote za maisha. Atakuja tena kuanzisha ulimwengu mpya.  Dhambi na wadhambi wataangamizwa. Hatimaye Shetani, atashindwa kwa ujumla kabisa. Yesu anatamani kukurejesha wewe kwa familia ya Mungu, kukupatia wewe uzima wa milele kwenye sayari iliyofanywa mpya.
Lakini uamuzi lazima ufanyike--Ni nani atakayekuwa Mkuu na Bwana wako ?
Rafiki, uamuzi huu ni swala la kufa na kupona Je, hutachagua sasa hivi kumruhusu Kristo awe Mfalme wako? Anasubiri. Mikono yake imefunguliwa wazi. Anasema, Njoo! Njoo! Njoo!!

Je, waweza kuinamisha kichwa chako tunaposali na kusema, Naam, Yesu, ninakuja.

AHSANTE KWA KUWA PAMOJA NAMI KATIKA MFULULIZO WA MASOMO HAYA.
                    ***MWISHO***


No comments: