Wednesday, June 13, 2012

KWA NINI KUNA MAHANGAIKO DUNIANI?


Yawezekanaje Mungu wa upendo akayaruhusu?

SEHEMU YA 1.
Clara Anderson alikuwa mjakazi jijini San Francisco, na Clara alikuwa mwanamke muungwana sana - na pia mwaminifu sana.! Siku moja baada ya kuwa mtendakazi kwa muajiri mmoja kwa miaka 15, alitoweka.! Muajiri wake hakujua alipokwenda. Alikuwa tu kama aliyetokomea toka machoni pa watu.! Kisha kwa namna ya ajabu, baada ya siku za kutafuta, idara ya jiji ya ustawi wa jamii ikampata.! Clara alikuwa katika mpango wa 'mgomo wa kula hadi kufa' katika kificho cha mlima nje ya San Fransisco. Akasema, Nataka kufa. Niacheni. Wakati mwandishi wa habari aliyemkuta alipomhoji, Clara
alisema,! Tazama , hakuna anayenijali. Mimi ni kijakazi tu - mmoja tu kati ya maelfu katika jamii watendao kazi za kinyonge. Maisha yangu hayana thamani. Sina ndugu wa karibu, sina jamaa, sina marafiki. Mimi ni mpweke kiasi kwamba sihitaji kuishi. Hakuna ninaye mdhani kuwa wa karibu nami - sina niwezaye kuzungumza naye, hayupo niwezaye kufungua moyo wangu kwake. Hivyo niacheni tu nife, kwa sababu hakuna kwa kweli anayejali.

Hakuna anayejali! ndicho kilio cha wanaume na wanawake katika sayari iliyo pweke.!
Hivi karibuni katika utafiti kuhusu Mungu, watu waliulizwa, Kama ungemuuliza Mungu swali moja, hilo swali lingelikuwa lipi?!
Vipi wewe? Kama ungemuuliza Mungu swali moja, lingelikuwa lipi? Tazama jinsi ambavyo mamilioni wangeuliza:! Mungu , je, kweli unanijali? Kama wewe ni mwema hivyo, kwa nini kuna maradhi mengi kiasi hiki? Mbona mahangaiko na mauti duniani?! Mbona kuna kuvunjika moyo hivi na huzuni?! Mbona kuna njaa, mafuriko, maafa yatokanayo na nguvu za asili, na vita?

Tuanatazama mazingira na tunatambua nguvu za kiovu zilizomo duniani.!
Kila mahali kuna maafa ya kutisha yanayotokea kila siku.

Ni nani anayewajibika kwa sababu ya maafa, shida, na taabu katika dunia?! Watu wengi humlaumu Mungu kwa matatizo wanayopitia.! Mara kwa mara utawasikia wakiuliza swali, Kwa nini Mungu alitenda hivi kwangu?
Hebu tutizame kile ambacho Biblia inasema juu ya pambano kuu linaloendelea kati ya nguvu za wema na zile za uovu.! Waweza kuuliza, Kama Mungu haleti shida zote hizi na huzuni duniani, ni nani anayewajibika kwa maafa yote haya tunayoyashuhudia?

Biblia inasonda kundi lenye makosa!! Yesu alieleza 
kisa juu ya mkulima alliyepanda mbegu ndani ya shamba, lakini mimea ilipokua, kulikuwa na magugu ndani ya shamba. (Fungu: Mathayo 13:27) !
Watumishi wa yule mwenye shamba wakamwendea, wakamwambia, "Mheshimiwa, bila shaka ulipanda mbegu nzuri katika shamba lako.
Sasa magugu yametoka wapi?" ! Walitaka kujua, magugu yalitokea wapi.

(Fungu: Mathayo 13:37) ! Yesu akawaambia, Mpanzi wa zile mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
Lile shamba ni ulimwengu. Zile mbegu nzuri ni watu wale ambao ufalme wa mbinguni ni wao,lakini yale magugu ni wale watu wa yule mwovu. Adui aliyepanda yale magugu ni ibilisi.
Mathayo 13:37-39! Mavuno ni mwisho wa nyakati na wavunaji ni malaika.

Unaona, wakati Mungu anapojaribu kuonyesha wema kwa kila mmoja, kuna nguvu nyingine itendayo kazi duniani iletayo maafa, misiba, mauti, na maradhi kwa maisha ya wana wa Mungu.

Kitabu cha mwisho cha Biblia, Ufunuo, kinatuambia jinsi mambo yalivyoanza ili tuwe na ukweli hakika juu y kile kilichotokea mbinguni na kusababisha taabu kubwa namna hii katika Sayari Dunia.! Tutagundua chanzo cha uovu. Waweza kushangaa,lakini kulipata kuwa na vita mbinguni!

Kisha kukazuka vita mbinguni: Mikaeli na malaika wake walipigana na hilo joka, nalo likawashambulia pamoja na malaika wake. na joka hilo halikuweza kuwashinda, na hatimaye hapakuwa na nafasi tena juu mbinguni kwa ajili yake na malaika wake.
Basi joka hilo kuu likatupwa nje. Joka hilo ndiye yule nyoka wa kale ambaye huitwa pia ibilisi au shetani. Ndiye anayeudanganya ulimwengu wote;
Naam, alitupwa duniani, na malaika wake pamoja naye.! Ufunuo 12:7-9.
Sasa, tazama jinsi huyu joka, au mwovuanavyotambulia katika Ufunuo 12:3,4:

Ishara nyingine ikatokea mbinguni: joka kubwa jekundu na lenye pembe kumi na vichwa saba; na kila kichwa kilikuwa na taji.
Joka hilo liliburuta kwa mkia wake theluthi moja ya nyota za anga na kuzitupa duniani...
Ni wazi kwamba theluthi moja ya malaika wa mbinguni walimfuata mdanganyifu katika uasi wake dhidi ya Mungu.!
Lakini hebu tuchunguze zaidi juu ya huyu malaika aliyeanguka aitwaye Lusifa.! Katika Agano la Kale anatajwa kama Mfalme wa Tiro, na yasema hivi juu yake: Ni wazi kwamba theluthi moja ya malaika wa mbinguni walimfuata mdanganyifu katika uasi wake dhidi ya Mungu.! Lakini hebu tuchunguze zaidi juu ya huyu malaika aliyeanguka aitwaye Lusifa.! Katika Agano la Kale anatajwa kama Mfalme wa Tiro, na yasema hivi juu yake: (Fungu: Ezekieli 28:12 -14)!
Bwana MUNGU asema hivi: Wewe wakitia muhuri kipimo, umejaa hekima, na ukamilifu wa uzuri.! Ezekieli 28:12.

Ulikuwa ndani ya Adeni, bustani ya Mungu; kila jiwe la thamani lilikuwa kifuniko chako....! Ezekieli 28:13.
Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye...ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu; umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto.! Ezekieli 28:14

Lusifa alikuwa malaika mkamilifu, aliyeumbwa kwa ukamilifu kwa namna zote.! Alikuwa malaika aliyesimama mbele za Mungu kama kerubi afunikaye.

Lusifa alishikilia nafasi iliyotukuka huko mbinguni. Katika pande zote mbili za kiti cha rehema au cha enzi cha Mungu kulikuwa na malaika wawili-mmoja kulia na mmoja kushoto. Mmoja wa hawa alikuwa Lusifa.
Hakuridhika kwa kuwa karibu hivyo na Mungu.! ALITAKA KUWA MUNGU!! Kitu kilitokea kwa Lusifa katika uhusiano wake wa karibu na Mungu. Mungu alimwambia Lusifa, (Fungu: Ezekieli 28:15)!
Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako.! Ezekieli 28:15. (Fungu: Ezekieli 28:17).
'Moyo wako uliinuka kwa sababu ya uzuri wako; umeiharibu hekima yako kwa sababu ya mwangaza wako...;! Ezekieli 28:17.

Huyu malaika mzuri, aliyetukuka akajipenda nafsi. Alitamani utukufu na heshima iliyomstahili Mungu pekee. Akawa na uchu wa madaraka. Akawa na ujasiri wa kumpa changamoto Muumbaji hata katika swala la utawala wa ulimwengu! Sikiliza kwa makini: Fungu: Isaya 14:12-14)!
Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa..........

Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu... .....Nitafanana na Yeye Aliye juu.! Isaya 14:12-14.

Maneno haya ya kiburi yalipoendelea kumiminika toka midomoni mwa Lusifa, upendo ulio kamili na amani ya mbinguni vikavunjwa vunjwa katika mamilioni ya vipande vidogo vidogo vya uchoyo.

Haikuchukua muda hadi Lusifa alipoanza kusambaza roho ya kutoridhika kati ya malaika wengine.! Pole pole bali kwa uhakika, aliharibu upendo wa Mungu na haki yake.


Kama tunda lililooza kwenye tenga, uasi wake ulienea kwa malaika wengine mbinguni.!
Pengine unashangaa kwa nini Mungu hakumuangamiza Shetani wakati ule.! Mungu angeweza kuwaangamiza Lusifa na malaika
waliojiunga naye katika uasi kwa muwako mmoja tu wa kupofusha, lakini kama angefanya hivyo, viumbe wote wangemtumikia kwa hofu.
Mungu ni Mungu wa upendo. Aweza tu kuwa na furaha katika mahusiano ya upendo na viumbe Vyake ambapo wanamwabudu kwa sababu wanampenda na kumuamini.
Shetani alikuwa ametoa changamoto kwa sheria za Mungu na haki yake, lakini Mungu hakuwa ameweka sheria hizi kwa mabavu ili aonyeshe ni nani aliye mkubwa! Aliziweka kulinda viumbe Wake,
kuhakikisha amani yao na furaha.

Sheria zake ni kama taa na alama zionyeshazo mwendo kasi ulio salama vyote vikiwa vimepangwa kwa ajili ya usalama wetu na kwa ubora wetu.! Bali huyu aliyeheshimika kati ya malaika wote alidhani ya kwamba angeweza kuendesha ulimwengu kwa ubora kuliko Mungu Muumbaji wake!

Shetani, adui wa Mungu , alijifanyia 'mwovu' ndani yake!






ITAENDELEA KATIKA SOMO LIJALO...............

No comments: