Monday, June 4, 2012

KUJIFUNZA MAANDIKO MATAKATIFU.


Fungu la tafakari: “Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutayari ukitumia kwa halali neno la kweli” 2Timotheo 2:15.

Makusudi ya somo hili: Kusisitiza kuwa kusudi letu ni kujifunza neno la Mungu kwa uaminifu, na kulinganisha maandiko kwa maandiko.


UTANGULIIZI..

Inaonekana wazi kuwa majibu ya kweli ya matatizo makubwa ya ulimwengu yanapatikana katika neno la Mungu. Mambo mengi yamefichwa katika kitabu cha ukumbusho (Biblia). Kama Maandiko yanavyotueleza. Nilazima yasomwe.

Sifa za Mwanafunzi mzuri wa Biblia.

Naam, ukiita busara, Na kupaza sauti yako upate ufahamu;
Ukiutafuta kama fedha, Na kuutafutia kama hazina iliyositirika;
Ndipo utakapofahamu kumcha Bwana, Na kupata kumjua Mungu. Mithali 2:3 – 5

Kuuelewa ukweli wa Biblia hakutegemei sana uwezo mkubwa wa akili katika kazi ya utafiti, bali kunategemea mwelekeo ulionyoka kwenye lengo na kusudi moja, shauku ya dhati ya kutafuta haki.


Maandiko yanapaswa kuchunguzwa kila siku, kwa uelekevu wa moyo. Ukifundishwa neno lazima uthibitishe kwenye maandiko kujua ndivyo lilivyo?

Matendo 17:11, ........ “kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.”

Siku zote tamani kujifunza maandiko na mtu aliye komaa yuaani mwenye uelewa mpana juu ya maandiko.

Kanuni ya kujifunza maandiko inapatikana Isaya 28:9,10 Soma huku kidogo na huku kidogo yaani pata ufafanuzi zaidi wa fungu unalolisoma, kwenye mafungu mengine yenye mada kama usomayo.

Japokuwa Biblia iliandikwa na waandishi mbalimbali ni Mungu ndiye aliwaongoza wote hao kuandika; kwa hiyo, maandiko yao yanakubaliana. Basi, ili kuelewa fungu moja ni vizuri kulinganisha na mafungu mengine ya wandishi wengine yanayogusia jambo hilo hilo.


Pamoja na hayo lakini bado kuna baadhi ya mafungu ni vigumu kuyaelewa, unahitaji mwalimu akueleweshe, vinginevyo unaweza kutoka na maana isiyo sahihi. Na huo utakuwa ndo mwanzo wa kupotoa maandiko, Leo unaona kunamadhehebu mengi sababu kubwa iliyofanya kuwe na madhehebu mengi ni kutoelewa vizuri maandiko. Unahitaji mtu mwenye hekima ya mungu na ujuzi wa neno la Mungu. Waebrania 5:12-15; 2Petro 3:15-16.


Msaada pekee kutoka Mbinguni ni Roho mtakatifu yeye anayajua hata mafumbo ya Mungu. 1Wakorintho 2:10; Yohana 14:26. ..”Yeye atawafundisha yote na kuwakumbusha yote niliyo wambia.”


Kusoma kwingi Biblia bila Maombi ni hatari, Lazima tuelekeze mawazo yetu na upendo kwa Mungu, au kulingana na mapenzi yake,

Unaposoma Biblia ukiwa na mashaka, huamini kama ni neno la Mungu, kutoamini kunatiwa nguvu. Wakati wowote mtu anapoacha kutafuta kufanana na Mungu kwa usemi na matendo, basi, bila kujali amesoma kiasi gani, ana hatari ya kukosea kuyaelewa Maandiko. Usichunguze Biblia kwa kuangalia kasoro, utakosa utambuzi wa kiroho, utakuwa kipofu.

Kujifunza Biblia kutakupa hekima hata utapata wokovu kwa imani katika Yesu Kristo. 2Timotheo 3:15.


Hebu mwanafunzi aichukue Biblia kama kiongozi wake na kusimama kama mwamba imara kwa kanuni........ Kadri wema Wake, neema Yake na upendo Wake unapofikiriwa, wazi na wazi zaidi utakuwa na utambuzi wa ukweli; shauku yako ya usafi wa moyo na usafi wa mawazo itakuwa juu zaidi na takatifu zaidi.


WITO: “LAKINI IWENI WATENDAJI WA NENO, WALA SI WASIKIAJI TU.. Yakobo 1:22 – 25.


Mungu akubariki na akusaidie kuelewa neno lake.

No comments: