Thursday, November 6, 2014

JE WAJUA KITABU CHA UFUNUO KILILETWA KWA YOHANA SIKU YA SABATO TAKATIFU?

Yohana asema, "Nalikuwa katika Roho, Siku ya Bwana." Yeye hapo hataji siku gani ya juma kuwa ndiyo Siku ya Bwana. Katika suala hili yatupasa kulinganisha Maandiko kwa Maandiko, na kuliacha Neno la Mungu lipate kutufafanulia siku gani kuwa ndiyo Siku ya Bwana. Siku ya Bwana ni siku ile ambayo Kristo ndiye Bwana wake. Yeye anatangaza kwamba ndiye Bwana wa Siku ya Sabato (Marko 2:28). Hivyo Sabato yake Kristo inapaswa kuwa ndiyo Siku ya Bwana.
PIA BWANA MWENYEWE AMESEMA KWA KINYWA CHAKE KATIKA ISAYA 58
13 Kama ukigeuza mguu wako usihalifu
sabato, usifanye anasa yako siku ya utakatifu
wangu; ukiita sabato siku ya furaha, na siku
takatifu ya Bwana yenye heshima;
ukiitukuza, kwa kutokuzifanya njia zako
mwenyewe, wala kuyatafuta yakupendezayo,
wala kusema maneno yako mwenyewe;

ANAIITA SIKU YA UTAKATIFU WAKE.
NA BWANA SIO MUONGO WALA MANENO YAKE YALIYOTOKA HAYABADILIKI~Zaburi 89:34
HIVYO YOHANA ALIPEWA MAONO KATIKA SIKU YA SABATO.

No comments: