Sunday, September 7, 2014

UJUMBE WA MALAIKA WA KWANZA

Ujumbe wa malaika wa kwanza ni wito wa kumwabudu Mungu Muumbaji. Kwa kweli, lugha yenyewe inatukumbusha sisi juu ya maneno yale yaliyotumika katika amri ya nne. Malaika wa kwanza asema hivi: “Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji” (Ufunuo 14:7). Vilevile, amri ya nne yatuambia sisi kumwabudu Mungu kwa sababu yeye ni Muumbaji wa vitu vyote mbinguni, duniani, na baharini. Yatuambia kwamba siku ya pekee ambayo Mungu ameitenga kwa ajili ya ibada ni siku ya saba ya juma - siku ya Sabato yake takatifu (angalia Kutoka 20:8-11).

No comments: