Sunday, September 7, 2014

UJUMBE WA MALAIKA WA PILI

Ujumbe wa malaika wa pili ni huu: “Umeanguka, umeanguka Babeli, mji ule ulio mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake” (Ufunuo 14:8). Babeli lilikuwa ni taifa katika Agano la Kale ambalo liliishambulia Israeli, yaani, watu wa Mungu, na kuwachukua mateka. Babeli lilikuwa ni taifa lililojaribu kuifutilia mbali ibada ya Mungu wa kweli wa mbinguni na mahali pake kuweka miungu ya kipagani. Na hivyo Babeli ikawa ishara iliyowakilisha majeshi yote yatakayowapinga watu wa Mungu katika siku za mwisho. Kwa hiyo malaika huyu wa pili anasema kwamba Babeli umeanguka kwa sababu umeyafanya mataifa yote ya dunia kunywa mvinyo ya uasherati wake, yaani, hiyo ni njia ya kusema kwamba majeshi yanayopigana na Mungu katika siku hizi za mwisho yatajaribu kumlazimisha kila mmoja kutoa utii wake kwa majeshi hayo kuliko kwa Mungu. Imewakilishwa kama “uasherati,” au uzinzi. Kutokumtii Mungu kunaonyeshwa katika Biblia kama uzinzi wa kiroho, jambo hili lote linatufikisha kwenye hoja ya utii.
 

No comments: