Sunday, February 19, 2012

PAPA AAGIZA KUUNDWA SERIKALI MOJA DUNIANI.
  • Asema itaanza na UN kisha kukabidhiwa dini
  • Lengo ni kulinda mataifa masikini duniani
  • Yahofiwa kuwa mwanzo wa Mpinga kristo
Wakati dunia nzima ikikabiliwa na migogoro ya kisiasa na mitikisiko ya kiuchumi, kiongizi wa Katoloki duniani, Papa Benedict wa XVI, amesema suluhiso la hayo yote ni kuundwa upesi kwa serikali moja ya kidunia, itakayoongozwa kwa muda na Umoja wa Mataifa (UN), lakini baadaye itaachiwa huru ijiendeshe yenyewe.
  Waraka rasmi wa kanisa Katoliki, ulitolewa na mamlaka ya Vaticani (makao makuu ya kanisa hilo) hivi karibuni, umemkariri Papa   akieleza kua kwa hali iliyofikia sasa dunia inahitaji kua na mfumo mpya wa serikali moja "a supranational authority" utakaotoa mwongozo katika masuala ya uchumi na siasa.
  Ili kuharakisaha uundwaji wake serikali hiyo, ataanzishwa na kusimamiwa na umoja wa mataifa kwa muda, lakini baadaye utajitegemea na kua serikali huru, na itakua na nguvu za kuhakikisha kua mataifa yaliyo endelea hayabani mataifa yaliyo masikini kwakutumia mabavu kupita kiasi.
  Waraka wa Vatican unasema ; Katika roho moja na nia moja, tukiwa wamoja Papa Benedict wa XVI anaona kuwa nilazima sasa kuharakisha kuundwa  kwa mfumo, (serikali) moja ya kisiasa duniani kote. Hili ni suala endelevu liloshughulikia  na kutatua matatizo ya ulimwengu wote kwa pamoja.
  Fikiri, kwa  mfano; hitaji kubwa la dunia kwa sasa ni amani na usalama, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kudhibiti silaha kali, kutetea na kulinda haki za msingi za binadamu, utawala wa uchumi na uratibu wa sera, wimbi la uhamiaji na usalama wa chakula na mazingira. Mambo haya yanapaswa yasimamiwe kwa pamoja na serikali moja ya dunia. Kimsingi hatuwezi kupata suluhisho la mambo yote haya, bila dunia kua kitu kimoja, yaani kuunganisha serikali zote na dini zote kua na mamlaka moja yenye nguvu na mamlaka ya kushughulikia kikamilifu na kwa nguvu kubwa.
  Kiukweli mamlaka ya Vatican inakerwa na tabia iliyoanzishwa na serikali za mataifa ya Magharibi ya kuzuiya wahamiaji kutoka mataifa maskini (dunia ya tatu) katika kambi ya watakatifu (Jean Rapsail), tulioamua kua kinyume na Magharibi katika suala la kuwatenga wahamiaji wanaotoka katika eneo la dunia ya tatu. Tunaunga mkono uingiaji wa wahamiaji hao wanao vamia mataifa tajiri.
  Kwa baraka zote, imeidhiniswa kuwa makasisi wa kanisa katoliki waunge mkono misafara ya wahamiaji wanaoingia nchi za Magharibi kwa kuwa Papa yuko kinyume na msimamo na mataifa ya ulaya na Afrika wa kupiga marufuku wahamiaji.
   Kimsingi  mamlaka ya Vatican inapendekeza serikali hiyo moja iwe na fedha yake, itakayotumiwa na watu wote, benki kuu moja, na mamlaka kamili ya dunia ambayo itatoa ruhusa kwa wanadamu, kuingia taifa lolote atakalo kuishi.
   Tayari vikao vimekaa mjini Vatcan na kushirikisha madhehebu kadhaa, ambayo yamekubali mpango huo wa kufaa, serikali moja ya dunia itakayokua mwalubaini wa matatizo na migogoro iliyopo sasa duniani. 
   Kwa mujibu wa Papa, kuundwa kwa serikali moja ya dunia itakayokuwa na mamlaka itakua ni hatua ya kwanza ya kuufikia umoja wa kiimani, aliagiza Bwana Yesu wa kukusanya pia makanisa yote  ya kikristo na kua na umoja wa dunia kidini.
  Mpango huu wa Vatican, ulitangiliwa na ule wa kuiunganisha dunia katika Teknolojia ya juu sana ya upachikaji wa chip maalumu kwenye mkono wa kulia au paja la uso, ambazo zinaweza kutoa taarifa zote za mwanadamu na kumtambulisha anachofanya na mahali alipo.
  Tayari majaribio kadhaa yamefanyika, ikiwa ni pamoja na kutumika katika mataifa ya Austrelia ambapo mwanasheria mkuu wa serikali amepachikwa kifaa hicho, na juhudi za kuwapachika wengine ziko mbioni.
  Kwakupitia mfumo wa chip, mwanadamu mmoja anaweza kutawala dunia yote kwa urahisi kuliko mfumo mwingine wowote. Inaelezwa kuwa, mfumo huo huu ukishashika kasi utaelekeza taifa kwenye mfumo mwingine unaitwa 'cashlesss' ambapo wanadamu wataondokana na matumizi ya fedha tasilimu na badala yake watatumia kadi iliyopachikwa mwilini.
  Mchakato wa masuala hayo yote  yameibua hisia tofauti, kwa baadhi ya waumini wa Protestant kuwa huenda hii ikawa ni mwanzo wa kuingia kwa Mpinga kristo duniani.

Imenukuliwa toka Gazeti la JIBU LA MAISHA la Jumapili, Februari 12 - 18, 2012.

Majibu ya mambo hayo hapo juu kwa msaada zaidi tafuta kanisa la Wa Sabato ndilo pekee lililojaliwa kujua unabii na vipindindi vyote hadi mwisho wa dunia.
Taarifa hizi kwao ni matayarisho ya kwenda mbinguni, maana Yesu karibu kuja, sio muda mrefu tutamwona mawinguni. Wito mpokeeni Yesu awe mwkozi wa maisha yenu, shikeni amri zake zote ikiwemo na sabato, ambayo wengi wameikataa, na kwasababu hiyo hawatafikia kipeo cha kweli yote maana wameikataa tabia ya Mungu.

Mungu akubariki unapofanya uamuzi.  
 

No comments: