Saturday, February 18, 2012

NI AKINA NANI PEKEE WATAKAO SIMAMA IMARA KATIKA PAMBANO KUU LA MWISHO?

"Ni wale tu walioimarisha akili zao kwa kweli za Biblia ndio watakaoweza kusimama imara katika pambano kuu la mwisho"

"Jifunze Biblia yako kwa namna ambayo hujawahi kamwe kujifunza siku za nyuma. Isipokua unainuka na kufikia kiwango cha juu cha utakatifu katika maisha yako ya dini, utakua tayari kwaajiri ya kufunuliwa kwa Bwana wetu"

 "Ni wale tu ambao wamekua wanafunzi wenye bidii wa Maandiko, na ambao wameipenda hiyo kweli, watakaolindwa dhidi ya madanganyo yenye nguvu yatakayouteka ulimwengu wote"

 "Tunazikaribia nyakati za dhoruba ... Kila msimamo wa imani yetu utachunguzwa; na ikiwa sisi si wanafunzi kamili wa Biblia, tuliothibitika, tulioimarishwa, na kutulia katika ukweli, basi, hekima ya watu mashuhuri wa ulimwengu huu itatufanya tupotee"         Dhiki kuu inakuja lakini kunatumaini, uk 15



No comments: