Monday, June 16, 2014

AMRI ZA MUNGU NA SHERIA ZA MUSA



MARA NYINGI WATU WANASHINDWA KUTOFAUTISAHA KATI YA AMRI ZA MUNGU NA SHERIA ZA MUSA ZIFUATAZO NI TOFAUTI
1. ZA MUNGU Ziliandikwa na Mungu mwenyewe Kwa kidole chake [Torati 31:18]
ZA MUSA Ziliandikwa na Musa mwenyewe kwa k wa kidole
2.Ziliandikwa kwenye mbao mbili za mawe yaliyochongwa, Torati 10:1-4
ZA MUSA Ziliandikwa kwenye chuo(kitabu cha dini), Torati 31:24
3., ZA MUNGU Ziliwekwa ndani ya Sanduku la Agano Torati 10:1-4
ZA MUSA Baada ya kuandikwa, ziliwekwa nje pembeni ya Sanduku la Agano,
Torati 31:24-27
4 . Waliozivunja, walionekana kutenda dhambi 1Yoh. 3:4, na iliwapasa kufa. Torati 17:2-5
ZA MUSA Waliozivunja, hawakuonekana na dhambi wala haikuwapasa kufa kwani zilikuwa ni kivuli cha Kristo Wakolosai 2:14-17
5. Yesu alikuja kuzitimiliza wala si ku zitangua. Watu wote wanapaswa kuzifundisha…Mathayo 5:17-19 -
ZA MUSA Yesu aliziondoa pale msalabani maana zilikuwa ni sheria za maa gizo
tu yaliyosimama kama kivuli cha mema yajayo. Kolosai 2:15
6. Sheria(torati) ya Bwana ni takatifu njema na ya haki, nayo yadumu mi lele na milele, Warumi 7:12-
ZA MUSA Zilikuwa ni kivuli cha kazi ya Yesu aliyoifanya msalabani, nazo zilikomea hapo. Ebran. 10:1-12
7. Sheria za Bwana ni kamilifu, za adili, kweli na za milele Zaburi 111:7-8
ZA MUSA Ziliishia pale Kristo alipokufa Msalabani. Waebran. 9:10-12, Luka 22:37
A. Mfano wa sheria ya Musa
1. Kuchinja kondoo kama mbadala wa mdhambi. Kutoka 29…, Walawi, Torati, Nyakati nk
2. Kifo yeyote aliyevunja mojawapo au Amri zote 10 za Mungu
Kutoka 31:14… Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake.
B. Sheria za Mungu, Kutoka 20 :1-17
Hivyo basi Yesu alipokufa Msalabani sheria za kuchinja kondoo tena ziliisha maana mwanakondoo wa Mungu (Yesu) aichukuaye dhambi ya ulimwengu alikuwa ameshachinjwa tayari.
Yohana 1:29 Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!

No comments: