Tuesday, May 27, 2014

UNABII ULIOTIMIA NA UNAOENDELEA KUTIMIA KATIKA SIKU ZETU

 
I. UFALME WA BABELI (606-538 au 605-539 K.K.).
Umewakilishwa na Kichwa cha dhahabu (Dan. 2:37-38). Historia inaunga mkono.
II. UFALME WA WAMEDI NA WAAJEMI (538-331 au 539-331 K.K.).
Uliuangusha Ufalme wa Babeli (Dan. 5:25-31). Unawakilishwa na Kifua na Mikono
ya Fedha (Dan. 2:32a,39a). Historia inaunga mkono. Miaka ni ya kukadiria tu.
III. UFALME WA WAYUNANI (331-168 K.K.)
Ufalme wa Wamedi na Waajemi ulitabiriwa kuwa utaangushwa na Wayunani (Dan.
8:4-7,20-21; 11:1-3). Ufalme wa Wayunani (Wagiriki) unawakilishwa na Tumbo na
Viuno vya Shaba (Dan. 2:32b,39b). Historia inaunga mkono.
IV. UFALME WA WARUMI (168 K.K. - 476 B.K.).
Ufalme wa Warumi unawakilishwa na Miguu ya Chuma. Biblia inaielezea vizuri
Dola ya Warumi kuwa ilikuwa inazivunja-vunja falme zile nyingine kama chuma. Danieli
hakujulishwa jina la Dola hii. Lakini historia inathibitisha kuwa Warumi waliwashinda
Wayunani mwaka ule wa 168 K.K. Wakati Kristo anazaliwa Dola hiyo ilikuwa bado
inatawala dunia pamoja na Palestina chini ya Kaisari Augusto (Luka 2:1-7; Yohana 11:48).

No comments: