Tuesday, May 27, 2014

UNABII ULIOTIMIA NA UNAOENDELEA KUTIMIA KATIKA SIKU ZETU

 
I. UFALME WA BABELI (606-538 au 605-539 K.K.).
Umewakilishwa na Kichwa cha dhahabu (Dan. 2:37-38). Historia inaunga mkono.
II. UFALME WA WAMEDI NA WAAJEMI (538-331 au 539-331 K.K.).
Uliuangusha Ufalme wa Babeli (Dan. 5:25-31). Unawakilishwa na Kifua na Mikono
ya Fedha (Dan. 2:32a,39a). Historia inaunga mkono. Miaka ni ya kukadiria tu.
III. UFALME WA WAYUNANI (331-168 K.K.)
Ufalme wa Wamedi na Waajemi ulitabiriwa kuwa utaangushwa na Wayunani (Dan.
8:4-7,20-21; 11:1-3). Ufalme wa Wayunani (Wagiriki) unawakilishwa na Tumbo na
Viuno vya Shaba (Dan. 2:32b,39b). Historia inaunga mkono.
IV. UFALME WA WARUMI (168 K.K. - 476 B.K.).
Ufalme wa Warumi unawakilishwa na Miguu ya Chuma. Biblia inaielezea vizuri
Dola ya Warumi kuwa ilikuwa inazivunja-vunja falme zile nyingine kama chuma. Danieli
hakujulishwa jina la Dola hii. Lakini historia inathibitisha kuwa Warumi waliwashinda
Wayunani mwaka ule wa 168 K.K. Wakati Kristo anazaliwa Dola hiyo ilikuwa bado
inatawala dunia pamoja na Palestina chini ya Kaisari Augusto (Luka 2:1-7; Yohana 11:48).

SHERIA YENYE REHEMA NA NEEMA

Ingawa sheria ya Mungu ni sheria ya rehema na neema ..hatimaye Mungu anaitumia kama kiwango au sababu ya kuhukumu...  Matokeo ya sheria yanakuwa hasi au chanya kutokana na mshika sheria mwenyewe anavyoiendea... sheria kazi yake ni kuonyesha dhambi sasa kama umeishika alafu hujaiendea neema ya Yesu ikusafi na kukusamehe,basi sheria hiyo itadai Ufe.. pia kristo anasema kuwa hukumu haitoki kwake- bali kwamba mwenye dhambi asiyetubu anajihukumu mwenyew pale anapokataa kusikiliza sheria(amri za mungu)...
hivi karibuni kabla au baada ya mlango wa rehema kufungwa tangazo litasikika "mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu,mwenye uchafu na azidi kuwa uchafu na azidi kuwa mchafu, mwenye haki na azidi kutenda haki, na mtakatifu na kutakaswa,(ufunuo 22:11)......
sheria kama kiwango cha hukumu pia ni kipimo cha upendo kwa Mungu ndani yako.. so shika kikamilifu cheria ya Mungu kwa upendo uliokisiri ndani yako juu ya YESU na neema yake itakuhesabia haki....